Precision Air yatangaza hasara ya Bilioni 30.4 kwa mwaka 2012


Mwaka haujafika wewe. Sauda ameingia PW mwaka huu mwanzoni.
Sasa mwaka upo wapi hapo?
 

Technical answer. Safi sana mkuu
 


  • Idadi ya abiria imeongezeka kwa asilimia 9.5

  • Total revenue nayo imeongezeka kwa asilimia 8.2
  • Mwaka 2011 kampuni hii ilitangaza faida

Mkuu, kwa taarifa hizi ni wazi kuwa kwa mtu yeyote anaeangalia hili atakwambia faida lazima itokee. Lakini cha kushangaza kwenye hii industry direct operating costs ziko juu sana na isitoshe the change of management this year imeonyesha jinsi CEO aliyepita ambavyo hakuwa makini na masuala ya fedha. Yawezekana alipika data wakati alivyokuwepo ili ionekane kila kitu kipo sawa wakati uhalisia haukuwa hivyo. Waliokuwa wanaidai kampuni wameongezeka sana baada ya uongozi kubadilika na inawezekana labda walikuwa wamesha write bad debts kwenye vitabu vyao.
haya yote yamechangia kupatikana kwa hasara iliyohabarishwa.
 
Wakati Precision wanatangaza kuuza hisa zao mwaka juzinilijua tu shirima biashara imemshinda na anataka kurudisha mtaji wake asepezake awekeze kwenye biashara nyingine. Kwa tunaomjua shirima tunajua analink nawatu wenye mitaji mikubwa ambao kama kweli biashara ya Aviation inalipa walawasingeshindwa kuwekeza mihela yao. Kuna wakubwa wengi serikalini nawafanyabiashara wakubwa ambao wamezificha hela zao nje ya nchi na wanatafutabiashara halali za kuwekeza hawazipati.

Kwa kitendo cha shirima kutangaza kuuza hisa, nilijuasomething fishy is coming and poor people and naive low income earners willcarry this burden. Watanzania wengi either wamesoma kwenye masomo ya biasharaau wamesikia au kuona jinsi watu huko ulaya na marekani wanavyoendesha maishayao kwa kutegemea kuuza na kununua hisa kwenye masoko ya mitaji. Wasichojua kuwahiyo theory hapa kwetu haiwezekaniki ni kuwa makampuni na biashara zote zenyerekodi ya faida kubwa (super profit) hisa zake zinashikiliwa na wajanjawachache (wengi wao wahindi) na hazijasajiliwa kwenye soko la mitaji la dsm (DSE).Ukiona kampuni inasajiliwa DSE ujue either inaelekea kufa kwa hiyo wenyekampuni wanasambaza risk kwa watu wengu au hiyo kampuni faida yake ni ndogo mnokiasi kwamba kwa gawio la kawaida ambalo mtu atalipata kwa mwaka linawezaku-break even na rate of inflation.

Ukitaka kuthibitisha haya angalia bishara zenye faida10 (10 most profitable businesses) halafu uliza shareholders ni kina nani? Kwakuanzia anza na makampuni ya simu.

Nashukuru rafiki zangu niliowaonya kuhusu kununua hisa za precision walinisikia.
 

Kununua hisa hapa Tanzania ni kujitafutia hasara, kupoteza muda na fedha. Kuna baadhi ya makampuni yanatoa gawio dogo kuliko hata RIBA ambayo ungeweza kupata ukiweka hiyo hela kwenye fixed account. Mfano CRDB...

Mbaya zaidi regulatory authority ni kama vile iko bongolala au incompetence, nina uhakika wakifanya uchunguzi Precision Air lazima watakuta kuna something fishy, na huenda Alfonse Kioko aliondoka kwa ajili ya mpango maalum. We cheki jinsi wanavyokandia Boeing kwenye report yao kuwa kuzimaintain ni very expensive ili hali wakati wanazilte walikuwa na mbwembwe kibao. Kampuni nyingi zinatumia Boeing 737 na profit kibao...
 
Mwaka haujafika wewe. Sauda ameingia PW mwaka huu mwanzoni.
Sasa mwaka upo wapi hapo?

Lakini mwaka huu ndio cancellation of flight imekuwa kubwa kuliko miaka yote na pia shirika linafanya kazi kishkaji kuliko wakati mwingine. Yule mkenya hata kama alikuwa na mapungufu au fisadi anaonekana alikuwa na akili sana kiasi cha kuacha BUBBLE ambayo hawakuiona na sasa imempasukia Saida. Uzuri naye ni mtanzania halisi, kila kitu analalamika kuwa kimesababishwa na mtangulizi wake...

Mfano wiki iliyopita mimi Ulukolokwitanga nilikuwa naenda Mwanza kwa ticketi ya kuondoka saa 12 jioni lakini kufika tu airport saa tisa na nusu wakanidaka na kunipandisha ndege tukaondoka saa 10 kamili. Kwa akili ya kawaida nikajua hawa jamaa wanaiga mashirika ya ki-Nigeria kwa usanii
 
Kikubwa ni kwamba Serikali isiingize mkono wake hapa, na isinunue share hata kidogo kama kufa acha wafe hawakujipanga washenzi hawa, Fast Jet kawagusa kidogo tu wamefika kileleni.
kuinvest ama kui-bailout Precision kutategemea mambo mengi, sio kweli kwamba kwa vile wamechemka leo basi hawawezi kuinuka tena. Ukiangalia vizuri ni kuwa challenges inayopitia precision inahusu industry nzima ya aviation, ndio maana kuna hivo vipengele ambavyo unaona ni positive lakini wamepata hasara, hata hao FastJet juzi tu wametangaza kupunguza wafanyakazi, na vile vile utakumbuka hata baadhi ya route walizifuta. Sasa kwa PA ambayo inaendeshwa na mikopo mikubwa lazima itikisike.
siitetei PA, kama wamefanya blunders katika management poa wacha wafe, lakini lazima tukubaliane kwamba PA ndio defacto national airline kwa sasa ni bora PA mara mia ya ATC. Wengine tunadhani bora serikali inunue share PA iachane na ATC.
 
kama kuna expenses zimeongezeka leo bei za mafuta n.k?
 

Kaka habari ya pale kubwa ni madeni. Madeni makubwa sana. Unaposhindwa kumanage vizuri direct operating supplies kama mafuta lazima ikusumbue. Deni la wese liko juu na supplier amekomaa hamna kujaza wese mpaka wameshika hela mkononi. Hiyo ndo inasababisha uchelewaji wa ndege kwa sasa ukilinganisha na zamani ambapo walikua wananunua wese on credit basis.
 
Utakuta akina Sauda wanamsingizia Kioko hata kuhusu kuwa na deni kubwa. Bodi ya wakurugenzi ni ile ile, Mwenyekiti ndio mwenye biashara yake kwa asilimia kubwa sitegemei kuwa alikuwa mbumbumbu kiasi cha kuburuzwa na yule mkenya.
Naunga mkono ombi lao hawa PW kusaidiwa na serikali, lakini kwa operational costs peke yake lakini sio ku-service madeni yao, wakati wanafanya maamuzi ya kijinga kukopa au kukodi yale ma Boeing mawili walijisifia kuwa watakuwa very competent kwenye soko.

All in All PW ndio shirika letu kwa sasa, hatuna National Airline ila PW inatutoa kimasomaso kuwa Tanzania kuna shirika la ndege.
 

Kuongeza mitambo mipya si rahisi kuongeza hasara kwani mara nyingi hiyo ni capital expenditure, labda kufanya ujanja wa hizo capital expenditure kuzi-expense as revenue expenditure. Hii in the short run unakwepa kodi lakini in future kodi itarudi palepale.
Nakubalina nawe juu ya kuongezeka kwa gharama hasa baada ya kuona walipata faisa mwaka jana. Yawezekana waliongeza mishahara nk.
Nikija kwenye hoja ya kuongezeka kwa abiria na mauzo lakini bado ikapatikana hasara:
1) Kwamba ni ujanja wa kutaka kukwepa kodi nk inawezekana kabisa, lakini pia;
2) Inawezekana kuna routes mpya ambazo wameanzisha bila kutafakari juu ya gharama zake; yaani waliangalia prestige zaidi kuwa wameongeza routes kumbe ni hasara tupu. Nawapa ushauri wa bure: Kila route ifanyiwe uchanganuzi wa peke yake kuona kama inapata faida au la, au inachangia katika kupata faida ingawa yenyewe inapata hasara.
Kwa mfano unaweza kuwa na feeder route unayoingiza hasara lakini kwa kuwa ina-feed kwenye route kubwa inayoingiza faida basi unalazimika kuendelea nayo; kimantiki hapa una-consider apportionment ya faida kwa hiyo main route.
 

Amini kununua zana mpya huleta hasara na yameshawahi nikuta na ndio wanaposimamia makampuni mengi kukwepesha kodi kubwa inayotakiwa kulipa mwishini mwa mwaka tokana na faida. Kumbuka kama wameamua kuongeza idadi ya ndege inawezekana kabisa gharama ya ndege moja ni zaidi ya faida wanayotazama kuiata kampuni hiyo kwa miaka zaidi ya mitatu, hivyo basi kwa miaka mitatu tutazamie hilo kuendelea hadi ghrama zitakaporudi kwa utaratibu wa kuangazli mapato na matumizi katika mpangilio wa kulipa kodi.
 

anyway.................
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…