hekimatele
JF-Expert Member
- May 31, 2011
- 9,890
- 2,795
Hapo tunafungwa na goal la Tik Tak,,,bonge la dili linachezwa.
Mwaka umefika sasa toka Sauda aje na bado mnasema ''JUZI"
Kweli kabisa mkuu unaamini kuwa kampuni imeongeza mauzo na idadi ya abiria bado ikapata hasara kubwa zaidi katika historia ya kampuni hiyo, kiasi cha kutishia uhai. Na bado mwaka mmoja uliopita kampuni hiyo hiyo ilikuwa inafanya kazi kwa faida!? Sisi wengine ni kama Tommaso, huwa hatuamini vitu kirahisi. Katika layman language, Ni sawa na mwenye duka bidhaa na wateja wameongezeka, mauzo yameongezeka lakini bado anapata hasara wakati mwaka jana alipata faida kwa wateja wachache na kuuza bidhaa kidogo ukilinganisha na mwaka huu.
1. 'pleased to announce..' hii ni lugha ya protokali tu kama vile unapoandika 'dear..' hata kama barua inaenda kwa adui yako.
2. sauda kaja juzi tu, matatizo haya yalianza zamani na hayana uhusiano kabisa na uwezo wa kiutendaji wa sauda, hata KQ inapitia magumu.
3. statements ziko audited hauamini nini?
Cha kushangaza,,,
- Idadi ya abiria imeongezeka kwa asilimia 9.5
- Total revenue nayo imeongezeka kwa asilimia 8.2
- Mwaka 2011 kampuni hii ilitangaza faida
My Take:
Ukiangalia tangazo lao kuwa kampuni is PLEASED to announce full year results na ukweli kuwa hayo mambo matatu makuu hapo juu ni kiashiria cha faida kwa kampuni lakini wao wamepata loss, tena kubwa mno katika historia ya aviation industry na kwa kampuni ndogo kama yao. Napata shida sana kuwaamini hawa jamaa,,, hii inamaanisha kuwa either wao wenyewe wana tatizo la management,,,
Au ndio mpango mzima kwa kulazimisha bail out kwa pesa zetu walipa kodi. Dr Mgimwa mzee wangu, open your eyes. How come someone is pleased to announce loss,,,, they dont regret to announce loss. Sauda Rajabu ni janga la kitaifa.
View attachment 110621
Wakati Precision wanatangaza kuuza hisa zao mwaka juzinilijua tu shirima biashara imemshinda na anataka kurudisha mtaji wake asepezake awekeze kwenye biashara nyingine. Kwa tunaomjua shirima tunajua analink nawatu wenye mitaji mikubwa ambao kama kweli biashara ya Aviation inalipa walawasingeshindwa kuwekeza mihela yao. Kuna wakubwa wengi serikalini nawafanyabiashara wakubwa ambao wamezificha hela zao nje ya nchi na wanatafutabiashara halali za kuwekeza hawazipati.
Kwa kitendo cha shirima kutangaza kuuza hisa, nilijuasomething fishy is coming and poor people and naive low income earners willcarry this burden. Watanzania wengi either wamesoma kwenye masomo ya biasharaau wamesikia au kuona jinsi watu huko ulaya na marekani wanavyoendesha maishayao kwa kutegemea kuuza na kununua hisa kwenye masoko ya mitaji. Wasichojua kuwahiyo theory hapa kwetu haiwezekaniki ni kuwa makampuni na biashara zote zenyerekodi ya faida kubwa (super profit) hisa zake zinashikiliwa na wajanjawachache (wengi wao wahindi) na hazijasajiliwa kwenye soko la mitaji la dsm (DSE).Ukiona kampuni inasajiliwa DSE ujue either inaelekea kufa kwa hiyo wenyekampuni wanasambaza risk kwa watu wengu au hiyo kampuni faida yake ni ndogo mnokiasi kwamba kwa gawio la kawaida ambalo mtu atalipata kwa mwaka linawezaku-break even na rate of inflation.
Ukitaka kuthibitisha haya angalia bishara zenye faida10 (10 most profitable businesses) halafu uliza shareholders ni kina nani? Kwakuanzia anza na makampuni ya simu.
Nashukuru rafiki zangu niliowaonya kuhusu kununua hisa za precision walinisikia.
Mwaka haujafika wewe. Sauda ameingia PW mwaka huu mwanzoni.
Sasa mwaka upo wapi hapo?
kuinvest ama kui-bailout Precision kutategemea mambo mengi, sio kweli kwamba kwa vile wamechemka leo basi hawawezi kuinuka tena. Ukiangalia vizuri ni kuwa challenges inayopitia precision inahusu industry nzima ya aviation, ndio maana kuna hivo vipengele ambavyo unaona ni positive lakini wamepata hasara, hata hao FastJet juzi tu wametangaza kupunguza wafanyakazi, na vile vile utakumbuka hata baadhi ya route walizifuta. Sasa kwa PA ambayo inaendeshwa na mikopo mikubwa lazima itikisike.Kikubwa ni kwamba Serikali isiingize mkono wake hapa, na isinunue share hata kidogo kama kufa acha wafe hawakujipanga washenzi hawa, Fast Jet kawagusa kidogo tu wamefika kileleni.
kama kuna expenses zimeongezeka leo bei za mafuta n.k?Mwaka umefika sasa toka Sauda aje na bado mnasema ''JUZI"
Kweli kabisa mkuu unaamini kuwa kampuni imeongeza mauzo na idadi ya abiria bado ikapata hasara kubwa zaidi katika historia ya kampuni hiyo, kiasi cha kutishia uhai. Na bado mwaka mmoja uliopita kampuni hiyo hiyo ilikuwa inafanya kazi kwa faida!? Sisi wengine ni kama Tommaso, huwa hatuamini vitu kirahisi. Katika layman language, Ni sawa na mwenye duka bidhaa na wateja wameongezeka, mauzo yameongezeka lakini bado anapata hasara wakati mwaka jana alipata faida kwa wateja wachache na kuuza bidhaa kidogo ukilinganisha na mwaka huu.
Lakini mwaka huu ndio cancellation of flight imekuwa kubwa kuliko miaka yote na pia shirika linafanya kazi kishkaji kuliko wakati mwingine. Yule mkenya hata kama alikuwa na mapungufu au fisadi anaonekana alikuwa na akili sana kiasi cha kuacha BUBBLE ambayo hawakuiona na sasa imempasukia Saida. Uzuri naye ni mtanzania halisi, kila kitu analalamika kuwa kimesababishwa na mtangulizi wake...
Mfano wiki iliyopita mimi Ulukolokwitanga nilikuwa naenda Mwanza kwa ticketi ya kuondoka saa 12 jioni lakini kufika tu airport saa tisa na nusu wakanidaka na kunipandisha ndege tukaondoka saa 10 kamili. Kwa akili ya kawaida nikajua hawa jamaa wanaiga mashirika ya ki-Nigeria kwa usanii
Utakuta akina Sauda wanamsingizia Kioko hata kuhusu kuwa na deni kubwa. Bodi ya wakurugenzi ni ile ile, Mwenyekiti ndio mwenye biashara yake kwa asilimia kubwa sitegemei kuwa alikuwa mbumbumbu kiasi cha kuburuzwa na yule mkenya.Kaka habari ya pale kubwa ni madeni. Madeni makubwa sana. Unaposhindwa kumanage vizuri direct operating supplies kama mafuta lazima ikusumbue. Deni la wese liko juu na supplier amekomaa hamna kujaza wese mpaka wameshika hela mkononi. Hiyo ndo inasababisha uchelewaji wa ndege kwa sasa ukilinganisha na zamani ambapo walikua wananunua wese on credit basis.
Eeleweke kwamba kwa tangazo hilo haina maana kodi haijalipwa. Kuna mambo kadhaa kwa wafanya biashara wanajua nini kinaweza kusababisha kampuni kupata hasara katika mahesabu ya mwaka kwa kupanga au kwa kutopanga kwa sababu zifuatazo:
- Kukiwa na faida kubwa kampuni hufanya purchase kubwa ili kupunguza pesa nyingi ambazo serikali inachukua, hili ni jambo la kawaida kwa wafanyabiashara na makampuni makubwa wanajua. Halifanyiki kwa Tanzania tu hata nchi zilizoendelea. Nilishawahi kuwa na kajibiashara fulani nchini Marekani, maofisa wa revenue walinipa mbinu za kupunguza gharama za kodi. Vinginevyo revenue inapofanya marejesho ya mapato yako ya mwaka unapo-renue business yako ujue faida utaawana na serikali.
- Kampuni kununua vitendea kazi vipya ikiwa ikiwa ni pamoja na office expences, mitambo mipya nk
- Na mengineyo mengi yanaweza kusababisha kampuni kupata hasara.
Kwa waliowahi kufanya kazi kwenye makampuni makubwa katika idara ya uongozi, wataalamu wa mahesabu nk wanajua ninachoongelea hapa
Kuongeza mitambo mipya si rahisi kuongeza hasara kwani mara nyingi hiyo ni capital expenditure, labda kufanya ujanja wa hizo capital expenditure kuzi-expense as revenue expenditure. Hii in the short run unakwepa kodi lakini in future kodi itarudi palepale.
Nakubalina nawe juu ya kuongezeka kwa gharama hasa baada ya kuona walipata faisa mwaka jana. Yawezekana waliongeza mishahara nk.
Nikija kwenye hoja ya kuongezeka kwa abiria na mauzo lakini bado ikapatikana hasara:
1) Kwamba ni ujanja wa kutaka kukwepa kodi nk inawezekana kabisa, lakini pia;
2) Inawezekana kuna routes mpya ambazo wameanzisha bila kutafakari juu ya gharama zake; yaani waliangalia prestige zaidi kuwa wameongeza routes kumbe ni hasara tupu. Nawapa ushauri wa bure: Kila route ifanyiwe uchanganuzi wa peke yake kuona kama inapata faida au la, au inachangia katika kupata faida ingawa yenyewe inapata hasara.
Kwa mfano unaweza kuwa na feeder route unayoingiza hasara lakini kwa kuwa ina-feed kwenye route kubwa inayoingiza faida basi unalazimika kuendelea nayo; kimantiki hapa una-consider apportionment ya faida kwa hiyo main route.
Utakuta akina Sauda wanamsingizia Kioko hata kuhusu kuwa na deni kubwa. Bodi ya wakurugenzi ni ile ile, Mwenyekiti ndio mwenye biashara yake kwa asilimia kubwa sitegemei kuwa alikuwa mbumbumbu kiasi cha kuburuzwa na yule mkenya.
Naunga mkono ombi lao hawa PW kusaidiwa na serikali, lakini kwa operational costs peke yake lakini sio ku-service madeni yao, wakati wanafanya maamuzi ya kijinga kukopa au kukodi yale ma Boeing mawili walijisifia kuwa watakuwa very competent kwenye soko.
All in All PW ndio shirika letu kwa sasa, hatuna National Airline ila PW inatutoa kimasomaso kuwa Tanzania kuna shirika la ndege.