Kamgomoli
JF-Expert Member
- May 3, 2018
- 1,896
- 4,058
Hatimaye tarehe 23/10/2022 ikafika baada ya siku kadhaa za tambo, ngebe na kelele nyingi kutoka kila upande. Kwangu Derby ya safari hii ilitawaliwa na saikolojia ya nje ya uwanja kati ya wale wa sizitaki mbichi hizi na wale wa kuendeleza rekodi kwanza ya kumfunga mtani na pili kuendelea kuwa 'Unbeaten'.
NDANI YA UWANJA
1. Wachezaji wa kila upande waliingia na hofu na tahadhari kubwa hasa upande wa Simba. Ile Simba tuliyoizoea ikicheza kwa ku flow kupitia beki za pembeni ikawa tofauti kidogo. Zimbwe na Mwenda walichukua tahadhari kwani Nabi aliwawekea Tuisila na Moloko, hii ikawafanya wasipande juu ovyo. Simba walikuwa hatari sana kwenye counter attacks na km Okra angeacha ubinafsi na uchoyo kuna nafasi km mbili hivi huenda zingebadilika kuwa magoli.
2. Tuisila na Moloko wajitathimini kama kweli wametoka nje kuja kuongeza thamani kwenye ligi yetu. Wanacheza staili ya mawinga wa kizamani. Kwenye soka la kisasa winga huwezi tegemea mbio tu. Wao kila mpira ni kukimbia halafu si wazuri kwenye kukaba pindi timu ikiwa haina mpira. Angalau Moloko anauafadhari tatizo ni kubwa mno kwa Tuisila. Tuisila hana uwezo mzuri wa kumiliki mpira,kupiga chenga na hata krosi zake nyingi hazina macho.
3. Mayele anachakujifunza kutoka kwa Phiri. Siyo kila mechi lazima afunge yeye ana ubinafsi sana ndiyo maana ana takwimu chache za usaidizi. Jana licha ya kukabwa sana na Onyango na Inonga bado alipata nafasi kadhaa ambazo kama angeweza kutoa pasi kwa wenzake angeweza kuisadia timu zaidi.
4. Okra jana angeweza kuwa shujaa ila uchoyo umeikosesha timu yake magoli zaidi. Kwa zile nafasi alizozipata kama angetoa pasi kama Chama alivyofanya kwake basi kuna magoli yangeongezeka. Alizingua sana licha ya kufungia timu yake goli pekee.
5. Yanga inabidi watafute kiungo mkabaji mwenye kasi zaidi ya Aucho. Faulo nyingi alizocheza Aucho ni matokeo ya kuzidiwa mbio na kupelekea kuchelewa kuufikia mpira kwa wakati.
6. Ki Aziz, Licha ya kufunga goli bora la viwango vya duniani bado namuona hajafikia kiwango km alipokuwa Mimosa. Nilimuona akipoteza mipira kadhaa, papatu papatu nyingi na ni mzito kidogo. Kocha wa mazoezi amfuatilie zaidi. Pia Mipira ya kona inamsumbua kupiga, kona zake nyingi hazifiki zinakuwa fupi zinaishia kwa mabeki. Pamoja na mapungufu yake bado ni mchezaji muhimu.
7. Hali ya joto iliathiri mchezo. Kuna muda hasa kipindi cha kwanza niliona wachezaji wakijimwagia maji mara kwa mara kutokana na joto kali.
8. Refa alijitahidi kwa kiasi chake japo sikuona sababu ya kubwatukiana na wachezaji mara kwa mara huku akitoa mimacho kama nini sijui!
Yote kwa yote mchezo ulikuwa 50 x 50, na kila timu imepata ilichostahili.
Nawasilisha.
NDANI YA UWANJA
1. Wachezaji wa kila upande waliingia na hofu na tahadhari kubwa hasa upande wa Simba. Ile Simba tuliyoizoea ikicheza kwa ku flow kupitia beki za pembeni ikawa tofauti kidogo. Zimbwe na Mwenda walichukua tahadhari kwani Nabi aliwawekea Tuisila na Moloko, hii ikawafanya wasipande juu ovyo. Simba walikuwa hatari sana kwenye counter attacks na km Okra angeacha ubinafsi na uchoyo kuna nafasi km mbili hivi huenda zingebadilika kuwa magoli.
2. Tuisila na Moloko wajitathimini kama kweli wametoka nje kuja kuongeza thamani kwenye ligi yetu. Wanacheza staili ya mawinga wa kizamani. Kwenye soka la kisasa winga huwezi tegemea mbio tu. Wao kila mpira ni kukimbia halafu si wazuri kwenye kukaba pindi timu ikiwa haina mpira. Angalau Moloko anauafadhari tatizo ni kubwa mno kwa Tuisila. Tuisila hana uwezo mzuri wa kumiliki mpira,kupiga chenga na hata krosi zake nyingi hazina macho.
3. Mayele anachakujifunza kutoka kwa Phiri. Siyo kila mechi lazima afunge yeye ana ubinafsi sana ndiyo maana ana takwimu chache za usaidizi. Jana licha ya kukabwa sana na Onyango na Inonga bado alipata nafasi kadhaa ambazo kama angeweza kutoa pasi kwa wenzake angeweza kuisadia timu zaidi.
4. Okra jana angeweza kuwa shujaa ila uchoyo umeikosesha timu yake magoli zaidi. Kwa zile nafasi alizozipata kama angetoa pasi kama Chama alivyofanya kwake basi kuna magoli yangeongezeka. Alizingua sana licha ya kufungia timu yake goli pekee.
5. Yanga inabidi watafute kiungo mkabaji mwenye kasi zaidi ya Aucho. Faulo nyingi alizocheza Aucho ni matokeo ya kuzidiwa mbio na kupelekea kuchelewa kuufikia mpira kwa wakati.
6. Ki Aziz, Licha ya kufunga goli bora la viwango vya duniani bado namuona hajafikia kiwango km alipokuwa Mimosa. Nilimuona akipoteza mipira kadhaa, papatu papatu nyingi na ni mzito kidogo. Kocha wa mazoezi amfuatilie zaidi. Pia Mipira ya kona inamsumbua kupiga, kona zake nyingi hazifiki zinakuwa fupi zinaishia kwa mabeki. Pamoja na mapungufu yake bado ni mchezaji muhimu.
7. Hali ya joto iliathiri mchezo. Kuna muda hasa kipindi cha kwanza niliona wachezaji wakijimwagia maji mara kwa mara kutokana na joto kali.
8. Refa alijitahidi kwa kiasi chake japo sikuona sababu ya kubwatukiana na wachezaji mara kwa mara huku akitoa mimacho kama nini sijui!
Yote kwa yote mchezo ulikuwa 50 x 50, na kila timu imepata ilichostahili.
Nawasilisha.