Tetesi: Press Conference ya Chadema haitakuwa "LIVE"

Tetesi: Press Conference ya Chadema haitakuwa "LIVE"

Determinantor

Platinum Member
Joined
Mar 17, 2008
Posts
59,045
Reaction score
94,974
Kuna taarifa nimekutana nazo mahali kuwa ingawa ITV na AZAM wali-confirm jana kuwa watarusha LIVE (Mubashara) Press Conference ya Chadema leo hii wametoa sababu kuwa hawataweza kufanya hivyo kama walivyokuwa wameahidi, ITV kwa upande wao wamedai mitambo yao ina matatizo kidogo kwahio hawataweza wakati AZAM wamesema wamepeleka mitambo yao Zanzibar (huenda kuna shughuli nyingine).

Bas tunaendelea kushukuru kwa kila figisufigisu! Tunachukulia majibu hayo positively kama ni kweli au ni uongo! Huenda kesho na baadhi ya magazeti yasiripoti kabisa, tusishangae.

Au CCM wanaogopa ile taarifa ya siri kuwa Makada wao wengi watakikimbia Chuma Chakavu kwenye Press hii??
TAARIFA KUHUSU PRESS CONFERENCE YA CHADEMA KUWA LIVE..

Binafsi nimeongea na mkuu wa Idara ya ya Habari na Mawasiliano CHADEMA Kamanda Tumaini Makene.

Ameniambia kwamba mpaka jana Saa 5usiku walikubaliana na CHANNEL TATU ZA TALEVISHENI kuonesha Mkutano wa CHADEMA na waandishi wa habari moja kwa Moja (LIVE) ikiwa ni pamoja na ITV NA AZAM.

Leo asubuhi ameambiwa na ITV kwamba hawataweza kurusha live Mkutano huo kwa sababu za kiufundi ambazo ziko juu ya uwezo wao......

AZAM TV nao wametoa taarifa kwamba hawataweza kurusha Mkutano huo Live kwa sababu vyombo vyao vimepelekwa Zanzibar ingawa jana walikubaliana na CHADEMA kurusha Mkutano Huo LIVE....

"Kutokana na hayo, imeshindikana kurusha Mkutano huo Live na kwa hiyo Chadema tutarekodi Mkutano huo na kurusha kipindi usiku au Jioni......... "Amemalizia Makene.

Binafsi nimesikitika Sana........

Daniel Ezekiel Daniel
 
Kuna taarifa zinasema televisheni zilizokua zirushe live mazimiyo ya kamati kuu ya chadema yamezuiliwa japo kua hayajaweka wazi na nani lakini hayatakuwa live tena.. wadadisi wa wambo wanasema nimwendelezo wa fgisu figisu za Demokrasia Tanzania

Zapa Radio tutaendelea kufwatilia hili na tutakuja na jibu
 
Kutorusha Live hivyo vyombo vya habari viko sahihi.Kuna vitu ni hatari kwao vinavyoweza kuwagharimu ikiwa ni pamoja na kufungiwa na TCRA hasa ukizingatia tabia ya kuropoka vitu visivyo na ushahidi na hatarishi kwa usalama wa nchi waliyo nayo CHADEMA.Waweza ongea kitu hewani ambacho kinaweza kigharimu kituo cha television.Hiyo ya kurekodi kwanza imetulia.Wahariri wanapata muda wa kuangalia na kujiridhisha kuhusu hicho kilichomo humo kwenye tamko kabla ya kurusha hewani kwa usalama wa kituo chao,usalama wa nchi na ukweli na uhakika wa habari husika.

Kituo kabla ya kurusha LIVE lazima kiwe na uhakika wa tabia na aina ya huyo mrusha habari Live lazima wamfanyie uchambuzi wa vipengele vya kitaalamu vya KYC (know your customer) kabla ya kutoa go ahead ya kuwa ruksa rusha live.Wakimkatalia ni sawa.Kwani Hata CNN au BBC hata ilipwe shilingi ngapi haiwezi rusha Live mahojiano na viongozi wa magaidi wa kundi la ISS au ALKAEDA.
 
Kutorusha Live hivyo vyombo vya habari viko sahihi.Kuna vitu ni hatari kwao vinavyoweza kuwagharimu ikiwa ni pamoja na kufungiwa na TCRA hasa ukizingatia tabia ya kuropoka vitu visivyo na ushahidi na hatarishi kwa usalama wa nchi waliyo nayo CHADEMA.Waweza ongea kitu hewani ambacho kinaweza kigharimu kituo cha television.Hiyo ya kurekodi kwanza imetulia.Wahariri wanapata muda wa kuangalia na kujiridhisha kuhusu hicho kilichomo humo kwenye tamko kabla ya kurusha hewani kwa usalama wa kituo chao,usalama wa nchi na ukweli na uhakika wa habari husika.

Kituo kabla ya kurusha LIVE lazima kiwe na uhakika wa tabia na aina ya huyo mrusha habari Live lazima wamfanyie uchambuzi wa vipengele vya kitaalamu vya KYC (know your customer) kabla ya kutoa go ahead ya kuwa ruksa rusha live.Wakimkatalia ni sawa.Kwani Hata CNN au BBC hata ilipwe shilingi ngapi haiwezi rusha Live mahojiano na viongozi wa ISIS au ALKAEDA.
Uko sahihi.
 
ccm na serikali yake wanazidi kujimaliza, kumbe hata kuzuia bunge live hofu ni chadema? Wanaogopa wananchi kuambiwa madhaifu ya ccm? Kama wana ubavu na wako makini kwa nini wasiache chadema waongee nao waje waongee yao pia? Haa kweli serikali haikai makini kuleta maendeleo zaidi ya kujaza msuli kupigana na chadema.
 
Kutorusha Live hivyo vyombo vya habari viko sahihi.Kuna vitu ni hatari kwao vinavyoweza kuwagharimu ikiwa ni pamoja na kufungiwa na TCRA hasa ukizingatia tabia ya kuropoka vitu visivyo na ushahidi na hatarishi kwa usalama wa nchi waliyo nayo CHADEMA.Waweza ongea kitu hewani ambacho kinaweza kigharimu kituo cha television.Hiyo ya kurekodi kwanza imetulia.Wahariri wanapata muda wa kuangalia na kujiridhisha kuhusu hicho kilichomo humo kwenye tamko kabla ya kurusha hewani kwa usalama wa kituo chao,usalama wa nchi na ukweli na uhakika wa habari husika.

Kituo kabla ya kurusha LIVE lazima kiwe na uhakika wa tabia na aina ya huyo mrusha habari Live lazima wamfanyie uchambuzi wa vipengele vya kitaalamu vya KYC (know your customer) kabla ya kutoa go ahead ya kuwa ruksa rusha live.Wakimkatalia ni sawa.Kwani Hata CNN au BBC hata ilipwe shilingi ngapi haiwezi rusha Live mahojiano na viongozi wa magaidi wa kundi la ISS au ALKAEDA.
Mpuuzi mwingine huyu hapa, nyie akili zenu ziko wapi hata sijui, ngoja ni sign out nisiharibu siku yangu bure
 
CHADEMA wakosa fedha za kurusha Live Mkutano wao na Waandishi wa Habari.



CHADEMA walitoa taarifa kuwa wangerusha moja kwa moja mkutano wao na waandishi wa Habari ambao ulipangwa kufanyika leo kuanzia saa tano Asubuhi. Taarifa zinasema kuwa chama hicho kilialika vyombo vya Habari vya Azam, ITV, Channel Ten na Radio kadhaa kurusha hewani mkutano huo.

Hata hivyo, mpaka leo saa mbili Asubuhi, CHADEMA wamekosa fedha za kurusha hewani Mkutano huo. Inaelezwa kuwa Freeman Mbowe amesema kuwa chama hakina fedha kwa vile walitumia fedha nyingi kugharamia Mkutano wa Kamati kuu kutokana na kuongezeka kwa siku za mkutano huo kutoka siku mbili zilizopangwa awali hadi siku nne. Naye kiongozi wa heshima wa CHADEMA, Edward Lowasa alipofuatwa kuokoa jahazi alijinu kuwa imekuwa ninghafla mno na kwamba wangemwambia mapema, angewasiliana na maswahiba wake wangemsaidia.

Ka hali hiyo, Mkutano huo umeshindikana kuwa Live na sasa rusubiri recorded au clips zilizoeditiwa.
 
ccm na serikali yake wanazidi kujimaliza, kumbe hata kuzuia bunge live hofu ni chadema? Wanaogopa wananchi kuambiwa madhaifu ya ccm? Kama wana ubavu na wako makini kwa nini wasiache chadema waongee nao waje waongee yao pia? Haa kweli serikali haikai makini kuleta maendeleo zaidi ya kujaza msuli kupigana na chadema.
Huu ni utawala wa JPM , mlimfanya JK kama babu yenu. Utawala huu mtaishia kujamba tu.
 
Back
Top Bottom