Wo shi niubi
JF-Expert Member
- Aug 14, 2015
- 1,353
- 1,784
...🤔🤔🤔...Lakini kwa kauli hizi za paniki tutakaoumia ni sisi Watanzania wa kawaida.
Halafu sioni Kabudi akimaliza miaka mitano ya Uwaziri, mbinyo ukizidi yeye ndio atakaetolewa kafara.
Safi sana japo Lissu na Zitto watakuwa na hasira za sisi kukataa ushoga ila habari ndiyo hiyo. Tuwaachie wao wenyewe huo ushoga.WAZIRI wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Profesa Palamagamba Kabudi amesema Tanzania haitakubali kudhalilishwa utu na heshima yake kama nchi huru, kupigishwa magoti kupata misaada na mikopo kutoka katika nchi yoyote duniani.
Kipi bora kulinda taaluma au kulinda tumboHuyu jamaa alinifanya nihairishe kusomea PHD pamoja na kuchaguliwa kusomea kozi hiyo Mlimani.
Yaani ukimuangalia unaona kabisa anaongea aliyotumwa akaseme Prof mzima unalazimishwa kuongea pumba kwa ajili ya kulinda nafasi yako
Wao mawazo binafsi sio mawazo ya wote sisi mawazo binafsi ya mtawala ndiyo sheria.Wao uongozwa kwa katiba na sheria sisi uongozwa na maagizoHii dunia ni ngumu sana kuielewa, kina Pompeo wanahubiri katika mataifa mengine free and fair election, viongozi wakubali matokeo ya uchaguzi wakati huo Pompeo hamtambui na kumkubali Biden kama mshindi halali wa USA, hii inatuambia nini ndugu zangu?
Hii wizara naona Prof Kabudi imeshampwaya kabisa, pengine wamjaribu sasa January Makamba ama Emmanuel Nchimbi ambaye pia anaweza kuteuliwa kuwa mbungeWAZIRI wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Profesa Palamagamba Kabudi amesema Tanzania haitakubali kudhalilishwa utu na heshima yake kama nchi huru, kupigishwa magoti kupata misaada na mikopo kutoka katika nchi yoyote duniani...
Hakuna mantiki. Ameongea pumba na mashuduSiyo pumba. Sikiliza vizuri utaona mantiki
Hawa watu ni wachumia tumbo hatari, hawana utu kabisaa. Labda hata siyo Watanzania.......Ningependa kujua hao wapiga makofi ni akina nani. Bila shaka watakuwa ni akina Bia yetu, Johnthebaptist, magu2016, Jane Lowassa, mama D.... Nchi yaani ina watu wengi sana wasiojitambua. Wako kama mbwa. Wakipata chakula tu basi kazi yao ni kutikisa mkia tu kila wanapomwona anayewapa chakula!
Waziri kabudi hafai kabisa.21 November 2020
WAZIRI WA MAMBO YA NJE TANZANIA PROFESA PALAMAGAMBA KABUDI AWAJIBU MABEBERU, HATUJAWAHI KUPIGISHWA MAGOTI, UCHAGUZI ULIKUWA HURU NA HAKI
Waziri wa Mambo ya Nje Prof. Palamagamba Kabudi aijibu EU - Umoja wa Ulaya kufuatia kikao cha bunge hilo la ulaya huko makao makuu ya EU kutishia uwezekano wa vikwazo kupitia Kamati yake Mambo ya Nje ya Bunge la Umoja wa Ulaya kujadili uwezekano wa kuibana Tanzania kwa vikwazo vya aina mbalimbali ikiwemo kusitisha msaada wa kuifadhili bajeti ya Maendeleo ya Tanzania.
Prof. Palamagamba Kabudi ameomba msaada wa vyombo vya habari nchini kuisaidia serikali ya Tanzania kwa kujitokeza na kuieleza Jumuiya ya Kimataifa ukweli wa mambo. Na kueleza Nyerere aliwahi kuwadindia Germany na United Kingdom na kukataa misaada na fedha zao. Prof. Palamagamba Kabudi anashangaa waTanzania kuanza kutetemeka ktk mitandao ya kijamaii kuhusu nchi yetu kuwekewa vikwazo.
Prof. Palamagamba Kabudi amesema Tanzania haifuati sera za kidiplomasia za kujitenga kufanya kazi na Jumuiya za Kimataifa. Hivyo waziri Prof. Kabudi amesema Tanzania ipo tayari kukaa ktk meza moja na wadau wa kimataifa kuzungumzia mapungufu yaliyopo lakini si kwa kuburuzwa na mabeberu bila kuwa na facts mezani.
Prof. Palamagamba Kabudi amesema kuwa watu wahuni wachache wa Kamati ya Mambo ya Nje ya Bunge la Ulaya EU hawawezi kuitisha na kuidhalilisha Tanzania na watambue Tanzania ni nchi huru.
Prof. Palamagamba Kabudi amesema maneno hayo mazito akiongea na Wafanyakazi wa Wizara hiyo muhimu ya Mambo ya Nje akatumia fursa hiyo kujibu uvumi kuwa Tanzania itanyimwa misaada na kuwakumbusha wafanyakazi hao kutembea vifua mbele kwani Tanzania siyo nchi ndogo kidiplomasia, kimsimamo, kiji-Geopolitiki na kiushawishi kimataifa.
.....................................................
EU Parliament Committee on Foreign Affairs discussion on Tanzania
Tujikumbushe walioitwa "wahuni wachache" na Prof. Kabudi, tarehe 19 November 2020 jijini Brussels kwa dakika 45 mfululizo walisema nini kuhusu Tanzania ktk kikao cha Kamati ya Mambo ya Nje cha Bunge la Jumuiya ya EU
Tazama / sikiliza dakika 45 za mjadala ktk kamati hiyo:
Kaaa kijana Una maneno mazito sanaUtu upi anao uongelea Kabudi? Endelea kutoa historical speeches za darasani ukijisahau kwamba upo field.