Prof. Kabudi katufundisha jambo juu ya utanzania na umuhimu wa kuilinda Tanzania ili tuendelee kuitwa watanzania. Ni mzalendo wa kweli

Prof. Kabudi katufundisha jambo juu ya utanzania na umuhimu wa kuilinda Tanzania ili tuendelee kuitwa watanzania. Ni mzalendo wa kweli

KARLO MWILAPWA

JF-Expert Member
Joined
Apr 10, 2019
Posts
2,789
Reaction score
4,951
Kila mara Prof. Kabudi anapoongea uwa nakuwa makini kutega sikio kuchota busara na hekima, hakika kwangu ni moja ya watu ambao sichoki kuwasikiliza. Kwa wengine inawezekana anaongea vitu vikubwa kuliko uelewa wao na wanashindwa kumuelewa lakini tunaomuelewa Prof. Kabudi hatuna mashaka na uchungu alionao juu ya kupotea kwa rasilimali za nchi hii. Ni mzalendo kwelikweli anayemsaidia kwa nguvu zote Rais wetu kulinda na kutunza rasilimali zetu dhidi ya mabeberu.

Siku ya jumamosi 23/11/2019, Prof.Kabudi katufundsha umuhimu wa utanzania wetu na hasa kuilinda Tanzania ili tuendelee kuitwa watanzania. Ni wachache sana wangemuelewa Mhe. Prof. Kabudi lakini ni ukweli pasina na shaka mtu huyu hachoki kukikumbusha kizazi hiki umuhimu wa Tanzania na jitihada zote zinazohitajika kuulinda utanzania. Prof. Kabudi anatukumbusha kuwa hakuna nchi utakayovinunia utanzania wako kama si Tanzania, leo kizazi za vijana wadogo kinashangilia utanzania wao unapoyumbishwa. Aibu kubwa sana hii.

Prof. Kabudi ni baba, mlezi na mwalimu; anatuelekeza, anatuasa na anatuonya popote pale anapopata fursa na muda wa kufanya hivyo. Kama mzazi, mlezi na mwalimu Prof. kabudi anatumia maneno ya Biblia kutoka kitabu cha Mithali 22:6 yanayosema “ mlee mtoto katika njia impasayo, naye hataiacha hata atakapokuwa mzee”. Prof. Kabudi ana jukumu la kutulea na kutukumbusha njia sahihi za kuulinda utanzania wetu ili nasi tuje kuwakumbusha vijana wetu. Vijana wanabeza njia hiyo wanataka kwenda njia wanayoiona wao, Prof. Kabudi hataki kuona hilo likitokea na matokeo ya hilo ni kuangamia kwa taifa.

Ukiachana na mapungufu ya kibinadamu aliyonayo Prof.Kabudi, hakika ni mzalendo wa kwelikweli na ana ujasiri mkubwa wa kusimamia rasilimali zetu bila kujali uhai wake, hakika vijana wa taifa hili wana mengi ya kujifunza kwa mtu huyu. Prof. Kabudi anahakikisha kila senti ya nchi hii inatumika kwa matumizi yaliyokusudiwa na anajivunia utanzania wake kuliko chochote alichonacho, huu ni uzalendo wa kiwango cha juu sana.

Kardinali Pendo aliwahi kusema, namnukuu ‘ tunajiuliza baada ya Magufuli atakuwa nani ila mkiwepo wengi wa aina yako nisingekuwa na shaka ya kuwaza nani atafuata baada yake’, ni maneno aliyosema dhidi ya Makonda. Kwakuwa urais hautoki kwa mwanadamu, unatoka kwa Mungu nami naamini katika hao wengi waliosemwa na Kardinali Pengo wewe Prof. Kabudi ni mmojawapo. Nakutakia usaidizi mwema ya majukumu yako kwa Mkuu wa nchi.
 
Profesa kabudi ni Mzalendo haswa

Wasaliti wa Nchi wajiandae kisaikolojia
 
Mipovu anayomwaga Kabudi haisaidii nchi ndiyo maana tunasena hapa dawa ya deni ni kulipa full stop.
 
Siasa za siasa.
tapatalk_1573980728131.jpeg
 
Ile hotuba ilijaa tamathali za semi na maneno meengi alitakiwa kusema ukweli kuwa ndenge imekamatwa na yule mkulima wa afrika kusini anadai hela zake, Sio kumdanganya mkuu kuwa eti ni njama za mabeberu wakishikiriana na viongozi wa nchi hii,kama vipi alipwe.
Unashabikia beberu kulipwa kutoka nchi masikini...!!?
 
Issue ya ndege,tulitakiwa kumfukuza huyo balozi wa Canada,hii mara ya pili tunachezewa akili na serikali ya Canada,mbona hayatokei zinapochukuliwa dreamliner USA
 
Issue ya ndege,tulitakiwa kumfukuza huyo balozi wa Canada,hii mara ya pili tunachezewa akili na serikali ya Canada,mbona hayatokei zinapochukuliwa dreamliner USA
Natamani itokee muda huu
 
Duuuh sawa twende huyo ndio msomi unahutubia umoja wa mataifa kwa kuishia kumsifia Rais tu
 
Ndugu yangu Mwilapwa Mungu hapendi dhuluma anataka uaminfu na ukweli.Huyo Kabudi unaemsema kuwa ni mlezi mwema na bora anatetea dhuluma na hana ukweli wowote.Mkulima wa watu anadai haki yake tumeshindwa kumlipa tunakuja kuongopeana kwa luleta maneno yaliyojaa methali ,naha na vitendawili kana kwamba vitatusaidia.
Kwann Kabudi asishauri mkulima kulipwa ili tuachanee na haya majanga? Kwami tukimlipa kidogo kidogo hatuwezi maliza deni?.Tutumie logic kuliko emotions
 
Kabudi hana hata chembe ya uzalendo zaid ya njaa na tamaa ya madaraka. Mtu huyu ukimuangalia kwa makini utatambua yakua hana lolote zaid ya siasa uchwara,. Sasa kilichopo nn huyu anadai kisheria alafu unajitutumua et nimemuita balozi na kumuambia bila tashititi sjui, dah maigizo haya kamwe hayatuachi salama
 
Unashabikia beberu kulipwa kutoka nchi masikini...!!?sijashabikia kulipwa jaribu kuelewa ni kwamba Kabudi alitakuwa kuongea ukweli sio kutoa hotuba ya uongo uongo tu ye alitaka tuamini suala kuzuiliwa kwa ndege ni suala la Tanzania na Canada?hao mabeberu si angewataja viongozi wa awamu hii wanafanya kazi kwa style ya NITOKE VIPI.
 
Katufundisha nini? Sioni katika bandiko lako?
 
Back
Top Bottom