Uchaguzi 2020 Prof. Lipumba akiwa Muleba: Mkinichagua kuwa Rais nitaunda Serikali ya umoja wa Kitaifa

Uchaguzi 2020 Prof. Lipumba akiwa Muleba: Mkinichagua kuwa Rais nitaunda Serikali ya umoja wa Kitaifa

CUF Habari

JF-Expert Member
Joined
Dec 12, 2019
Posts
239
Reaction score
234
IMG_20200923_143237_548.jpg
IMG_20200923_160607_557.jpg
MKINICHAGUA KUWA RAIS NTAUNDA SERIKALI YA UMOJA WA KITAIFA"PROF.LIPUMBA"

MULEBA KAGERA

Nchi yetu imejaa ufisadi, ubinafsi, migawanyiko, kuumizana, ubaguzi, kutokuaminiana, chuki, kukata tamaa na huzuni.

Haya ni majera hayanayohitaji kutibiwa na kuwarejeshea wananchi matumaini.

Tumefikia hapa tulipo kutokana na Tanzania kukosa taasisi imara za kusimamia uendeshaji wake.

Taasisi zilizoko uimara wake ni wa kinadharia kuliko wa uhalisia. Katika mazimgira haya mustakabali wa nchi umekuwa ukitegemea zaidi haiiba na matakwa ya rais aliyeko madarakani kuliko taratibu za kitaasisi.

CUF inataka nchi iwe na taasisi imara zinazounda mfumo madhubuti ambao utahakikisha kuwa nchi iko salama bila kujali ni chama gani kiko kwenye nadaraka.

Kuunda mfumo huu kunahitaji nguvu ya pamoja na ushirikishwaji wa kila Mtanzania.

Kwa sababu hii CUF inapendekeza serikali ya umoja wa kitaifa. Serikali hii jumuishi itakuwa na jukumu la kujenga mfumo unaohitajika.

Serikali ya Umoja wa Kitaifa chini ya CUF itaweka misingi ya kuhakikisha kuwa taifa linakuwa na Demokrasia ya kweli.

Serikali ya umoja wa kitaifa itakamilisha mchakato wa kupata katiba mpya yenye misingi imara ya demokrasia na utawala bora.

Katiba ambayo pamoja na mambo mengine itatenganisha kikamilifu mamlaka na nguvu za mihimili mbalimbali, italinda misingi ya ushindani wa kisiasa, itapanua na kukuza haki za kiraia, na itahakikisha uwepo wa uhuru wa kutosha wa vyombo vya habari na fursa ya
kujieleza.

Tunahitaji kuwa na katiba nzuri inayompa kila Mtanzania uhuru wa kweli wa kuchagua na au kuchaguliwa.

Tunahitaji kuwa na Muungano wa Watanganyika na Wazanzibari usio na mashaka ndani yake kwa pande zote mbili.
 
Huyu babu hata akigombea uenyekiti wa mtaa hapati, ruzuku ndiyo anaiaga hivyo baada ya kukubali kununuliwa na CCM
 
View attachment 1578501View attachment 1578502MKINICHAGUA KUWA RAIS NTAUNDA SERIKALI YA UMOJA WA KITAIFA"PROF.LIPUMBA"

MULEBA KAGERA


Nchi yetu imejaa ufisadi, ubinafsi, migawanyiko, kuumizana, ubaguzi, kutokuaminiana, chuki, kukata tamaa na huzuni.

Haya ni majera hayanayohitaji kutibiwa na kuwarejeshea wananchi matumaini.

Tumefikia hapa tulipo kutokana na Tanzania kukosa taasisi imara za kusimamia uendeshaji wake.

Taasisi zilizoko uimara wake ni wa kinadharia kuliko wa uhalisia. Katika mazimgira haya mustakabali wa nchi umekuwa ukitegemea zaidi haiiba na matakwa ya rais aliyeko madarakani kuliko taratibu za kitaasisi.


CUF inataka nchi iwe na taasisi imara zinazounda mfumo madhubuti ambao utahakikisha kuwa nchi iko salama bila kujali ni chama gani kiko kwenye nadaraka.

Kuunda mfumo huu kunahitaji nguvu ya pamoja na ushirikishwaji wa kila Mtanzania.

Kwa sababu hii CUF inapendekeza serikali ya umoja wa kitaifa. Serikali hii jumuishi itakuwa na jukumu la kujenga mfumo unaohitajika.


Serikali ya Umoja wa Kitaifa chini ya CUF itaweka misingi ya kuhakikisha kuwa taifa linakuwa na Demokrasia ya kweli.

Serikali ya umoja wa kitaifa itakamilisha mchakato wa kupata katiba mpya yenye misingi imara ya demokrasia na utawala bora.

Katiba ambayo pamoja na mambo mengine itatenganisha kikamilifu mamlaka na nguvu za mihimili mbalimbali, italinda misingi ya ushindani wa kisiasa, itapanua na kukuza haki za kiraia, na itahakikisha uwepo wa uhuru wa kutosha wa vyombo vya habari na fursa ya
kujieleza.

Tunahitaji kuwa na katiba nzuri inayompa kila Mtanzania uhuru wa kweli wa kuchagua na au kuchaguliwa.

Tunahitaji kuwa na Muungano wa Watanganyika na Wazanzibari usio na mashaka ndani yake kwa pande zote mbili.
Kwenye hiyo Serikali Bashite atakuwepo?
 
Serikali ya kitaifa huwa haiji hivihivi bali inaundwa kutokana na mazingira kama Zanzibar chama chochote kikishinda ni muhimu kuweka serikali ya kitaifa
 
Huyu Mzee bana, Kipi kinatakiwa tutangulie?
 
Back
Top Bottom