Elections 2010 Prof Safari for President 2015

Elections 2010 Prof Safari for President 2015

Ntemi Kazwile

JF-Expert Member
Joined
May 14, 2010
Posts
2,182
Reaction score
308
Inaonekana CHADEMA wamejipanga vema kukabiliana na mbinu chafu za CCM, ile turufu yao ya kusema CHADEMA ni chama kinachoongozwa na kanisa itakufa pale watakaposimamisha mgombea mwisilamu na kwa maoni yangu Prof Safari anaweza kuwa anaandaliwa kuchukua nafasi ya Dr Slaa kama mgombea wa uraisi wa Chadema 2015.

Hongera sana CHADEMA kwa kuwanyamazisha hawa matapeli wanaowapaka matope
 
Na hilo ndilo lengo la Prof. Safari kuhamia Chadema. (watu wana malengo bwana!)

Na ikiwa ndivyo hivyo a hoja ndio hiyo kwanini wasemuweke ZK kugombea?

Je kwa kufanya hivyo watajenga au ndio watakichimbia kaburi chama chao?
 
Kwani Prof Safari ni Muislam peke yake CDM na je tunachagua kiongozi kwasababu ya dini yake........Dini, ukabila/ukanda isiwe kigezo
 
Na haya ni matope pia, unajua kuwa udini CDM ni mbinu ya CCM bado unaleta hoja kusapoti hayo matope. Anayeulizia ZK, by 2015 he 'll be 39. Katiba itaka kuanzia 40
 
Mie naona kama anavizia post ya ugombea mwenya wakishinda apate umakamu wa raisi. Si mlikuwa mnawebeza eti mgombea mwenza wa CDM darasa la 7? Sasa wanaye professor!
 
Inaonekana CHADEMA wamejipanga vema kukabiliana na mbinu chafu za CCM, ile turufu yao ya kusema CHADEMA ni chama kinachoongozwa na kanisa itakufa pale watakaposimamisha mgombea mwisilamu na kwa maoni yangu Prof Safari anaweza kuwa anaandaliwa kuchukua nafasi ya Dr Slaa kama mgombea wa uraisi wa Chadema 2015.

Hongera sana CHADEMA kwa kuwanyamazisha hawa matapeli wanaowapaka matope

wapiga kura bado hawajashawishika kwa hili labda kwa uchache mawazo ya mwanakijiji yafanyiwe kazi na chadema. Halafu Zitto naye watakuwa wamemtendea haki kweli? maana mbowe alisha test akachemka, Slaa karusha rusha miguu kaishia kwenye maandamano sasa ni zamu ya Zitto ajaribu.CDM ikitaka ijinyonge yenyewe ni kumsimamisha huyo Pro safar, kwani hatotangazika kama akisimama Zitto.
 
Prof. Saffari hana sifa ya kuwa mgombea Urais wa chama kikuu cha upinzani Tanzania, CHADEMA. Kwanza nani amekwambia kuwa DK. WILLIBROD SLAA hagombei 2015? Hata kama Slaa akiamua hagombei, Prof. Saffari si chaguo bora la kuchukua nafasi hiyo.

Ukiacha kuwa ana elimu ya kutosha, hana uzoefu wa kuchaguliwa kwenye nafasi yoyote ya kitaifa ya uongozi, eg udiwani, ubunge, etc, hivyo chama makini kama CHADEMA hakiwezi kukurupuka tu out of nowhere na kumchagua kuwa mgombea wake urais.
 
mmeanza tena ...ni nani kasema Prf. amekuja CDM kuwa rais,hivi nyinyi mnadhani mwisho wa siku kila mwanasiasa atakuwa raisi? ..Urais kama taasisi sivyo mnavyotaka iwe..,wenzetu CCM ndo wanaleta mtu on the basis of Patronage & facial beauty ..
 
watu wengine bwana, wako kuleta chokochoko na fitna tu, hii thread ni application ya udini!
 
wapiga kura bado hawajashawishika kwa hili labda kwa uchache mawazo ya mwanakijiji yafanyiwe kazi na chadema. Halafu Zitto naye watakuwa wamemtendea haki kweli? maana mbowe alisha test akachemka, Slaa karusha rusha miguu kaishia kwenye maandamano sasa ni zamu ya Zitto ajaribu.CDM ikitaka ijinyonge yenyewe ni kumsimamisha huyo Pro safar, kwani hatotangazika kama akisimama Zitto.
Lini umefanya utafiti wa wapiga kura kugundua kuwa bado hawashawishiki? Afadhali ungesema tu kuwa ni maoni yako au ni wewe ambaye bado hushawishiki ungeeleweka vizuri tu.
 
Mtazikwa na udini wenu!, nyie kalia majungu na udini hamfiki popote!, chadema hamna udini na sio chama cha watu 2 kama kile cha prof wa uchumi anaegombea yeye na maalim tu tangu 1995, angekua raisi hiyo 95 si angegoma kuondoka kama bgabgo?
 
Mbona maraisi wako wengi tu Tanzania! Raisi wa TFF, Raisi wa wasanii, raisi wa bendi gani tena vile etc etc! You can name them all.
What we are looking for ni kiongozi mwenye uwezo, nia ya dhati na maisha ya watanzia, mwadilifu, mwenye uwezo wa kusema hili hapana na hili liwe hivi! Mtu ambaye ni clean! mwenye vision ya kutaka kuona maendeleo ya dhat ya Tanzania hii yenye utajiri wa kila aina. Hatutaki kabila, dini wala rangi ya mtu!
 
Kwa mawazo haya wana JF bado tuna safari ndefu!
Kwa mtu mwenye nia ya dhati ya kuikomboa nchi yetu dhidi ya utawala huu haramu wa RA ni jambo la aibu kubwa kukuta watu wanamjadili Prof. na dini yake wakati huko serikalini Zitto na wenzake wanajadili nani amlipe RA na kampuni yake ya DOWANS badala ya kuangalia uwezekano wa kuepuka kuwalipa deni hilo la kugushi.
 
Na hilo ndilo lengo la Prof. Safari kuhamia Chadema. (watu wana malengo bwana!)

Na ikiwa ndivyo hivyo a hoja ndio hiyo kwanini wasemuweke ZK kugombea?

Je kwa kufanya hivyo watajenga au ndio watakichimbia kaburi chama chao?

Zitto 2015 atakuwa na miaka 39 kwa hiyo hatakuwa na sifa ya kugombea urais!
 
Prof. Saffari hana sifa ya kuwa mgombea Urais wa chama kikuu cha upinzani Tanzania, CHADEMA. Kwanza nani amekwambia kuwa DK. WILLIBROD SLAA hagombei 2015? Hata kama Slaa akiamua hagombei, Prof. Saffari si chaguo bora la kuchukua nafasi hiyo.

Ukiacha kuwa ana elimu ya kutosha, hana uzoefu wa kuchaguliwa kwenye nafasi yoyote ya kitaifa ya uongozi, eg udiwani, ubunge, etc, hivyo chama makini kama CHADEMA hakiwezi kukurupuka tu out of nowhere na kumchagua kuwa mgombea wake urais.
Hapo kwenye blue utakua ujamtendea haki Prof Safari, kama mwanachama anayo haki ya kugombea urais
 
Hapo kwenye blue utakua ujamtendea haki Prof Safari, kama mwanachama anayo haki ya kugombea urais

Chatu tofautisha na sifa/uwezo/qualification/electability na haki. Sijasema hana haki, ila kwa mawazo yangu hana sifa kwa kuwa hajawahi hata kuchaguliwa kuwa Mbunge, ni ngumu sana mtu huyo akawa na name recognition ya kutosha na kugombea Urais 2015. Pia atakuwa na weakness ya uzoefu ya uongozi wa umma kwa kuwa hajawahi kuchaguliwa kwenye nafasi yoyote ya uongozi.

Ni upumbavu kwa watu kuanza kuleta udini na kusema eti Prof. Saffari anafaa kuwa mgombea Urais wa CHADEMA 2015 kwa kuwa tu ni Muislamu. Hizi ni fikra za kipumbavu. Religion has nothing to do with it. Pia its too early kuanza kuzungumzia mgombea Urais wa CHADEMA wa 2015 mwaka huu wa 2011. Tuvute subira mpaka 2014 hivi ndiyo tuanze mjadala huu.
 
Ccm si mkae muandae mgombea wenu kuliko kuanza kuipangia cdm nani agombee? Mbona wanacdm waliokwenda nccr hawakugombea urais. Acheni udini wenu,cdm itapiga kura kumchagua nani atagombea wala si kwa nyie ccm kuleta hojaless zenu! Kaeni muishone ccm iliyotatuka tatuka!
 
Back
Top Bottom