Prof Shivji atunukiwa Kiti Cha Usomi cha Mwalimu Nyerere

omarilyas

JF-Expert Member
Joined
Jan 24, 2007
Posts
2,130
Reaction score
150
Wazee najitahidi kuwatupia mambo ya leo MLIMANI wakati wa kumsimika msomi wetu Prof Issa Shivji Kiti Maalumu cha Usomi Cha Mwalimu Julius kambarage Nyerere. yeye anakuwa msomi wa kwanza kutunukiwa kiti hicho ambacho ni cha kwanza cha mfanowe kuanzashwa katika vyuo vyetu hapa nyumbani. kiti hiki kinamtambulisha Prof Shivji kama Msomi mahiri wa falsafa za mwalimu nyerere na mapmbano ya mwafrika. Kazi yeke itakuwa ni kufanya tafiti, mijadala na shughuli zingine zenye kulenga kutunza na kuchanganua mafundisho ya mwalimu nyerere haswa katika masuala ya vuguvugu la uafrika yaani PANAFRICANISM.

Natumai nitafanikiwa kuupload baadhi ya mapicha na ikishindikana naomba mwanakijiji na invisible wanijulishe jinsi ya kuwatumia wao.

Tanzanianjema
 
issa shivji ni mzalendo kweli kweli, ingekua kila msomi au maprofessor wa tanzania wanatetea wanyonge kama anavyofanya IS ingekua safi sana,kwa kifupi ni kwamba issa shivji ni mtanzania mwenye asili ya kiasia lakini ni mzalendo halisi kupita ben mkapa,edward lowassa,karamavi,msabaha,chenge,balali, jakaya na mafisadi wengine wote wasiopenda nchi yao bali matumbo na ufahari wakuwa na mali za wizi wanazoziiba kutoka kwa watu mufukara/maskini kabisa duniani yaani watanzania wakawaida.GOD BLESS YOU PROF ISSA SHIVJI KWA KUCHAGUA KUWA MZALENDO UNAYOIPENDA NCHI YAKO NA MTETEZI WAWANYONGE.
 
TanzaniaNjema:

Hebu tufahamishe kwa kina zaidi kuhusu tuzo hiyo. Ilianzishwa lini na ni nani anaiisimamia? Kwa kiingereza wanaiitaje?

Shivji anastahili sana kuipata hiyo tuzo. Ningetarajia itangazwe kwa uwazi zaidi na sifa zinazotakiwa ili mtu awe mtunukiwa ziwekwe wazi zaidi. Je, ni kamati inayohusika na uteuzi huo?

Mbona hii tuzo mhimu haifahamiki vizuri?

Mwenye taarifa zaidi tafadhari tuwekeeni hapa tupate kuzisoma.

TanzaniaNjema, natumai utarudi kama ulivyoahidi.
 
Hongera sana Prof Shivji You deserve it, please lead a fight for ufisadi in our country. Najua u mwanasheria, je ni sheria ipi inayowafanya mafisadi kama Chenge et al wasiwe rumande kwa kutuhumiwa kwa ufisadi wakati upelelezi ukiendelea?
 
Issa shivji anastahili kwa asilimia 100, kama marehem Chachage asingetangulia mbele ya haki nadhani ndie alikua anafuatia maana nae aliamini katika falsafa za Mwl nyerere...all the best Prof
 
Yes, without a doubt Prof Shivji deserve the honour to be the first research chair of Mwalimu JKN. He has long been one of the most articulate critics of the destructive effects of neoliberal policies in Africa, and in particular of the ways in which they have eroded the gains of independence.... He is a regular contributor to PAMBAZUKA FORUM at http://pambazuka.org/en/, just search for his name …… enjoy
 

This is the description of the award

 
ebu pateni information kibao kwa ku-google CORRUPTION INVOLVED JERSEY ISLAND ENGLAND halafu mtashangaa jinsi kisiwa hiki kilivyokubuhu kwa kuweka vijisenti.
 
Mtu kama Prof Issa Shivji na mfano wake ndio wanafaa kupewa nafasi za ubunge wa kuteuliwa na hata kupewa uwaziri.............JK umesikia!!!

Hongera sana Prof Issa......haki yako kabisa kukusanya hizo heshima
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…