Profesa Ali Tabibu aeleza mabadiliko na mahusiano ya Kitaaluma na Tanzania katika mazungumzo na balozi Yakubu

Profesa Ali Tabibu aeleza mabadiliko na mahusiano ya Kitaaluma na Tanzania katika mazungumzo na balozi Yakubu

Ojuolegbha

JF-Expert Member
Joined
Sep 6, 2020
Posts
1,278
Reaction score
797
Balozi wa Tanzania nchini Comoro Mhe. Saidi Yakubu amefanya mazungumzo na Professa Ali Tabibu Ibouroi, Mkuu wa Chuo Kikuu cha Comoro alipomtembelea katika makao makuu ya Chuo hicho.

Prof. Ibouroi alimweleza Balozi Yakubu kuwa Chuo hicho kimeanzishwa miaka 20 iliyopita na ndio chuo kikuu pekee nchini Comoro kikiwa kina wanafunzi 12,000 na walimu 300 ambapo kina vituo vya ufundishaji 10 katika visiwa vitatu vya Ngazidja, Anjouan na Moheli.
IMG-20240913-WA0014.jpg
Mkuu huyo wa Chuo alieleza pia maeneo kadhaa ya ushirikiano na Tanzania ambapo wana ushirikiano na Chuo Kikuu cha Dar es salaam tangu mwaka 2008 na mwaka jana walisaini makubaliano ya ushirikiano na Chuo Kikiu cha Taifa cha Zanzibar ikiwemo kubadilishana walimu na wanafunzi.
IMG-20240913-WA0012.jpg
Kwa upande wake, Balozi Yakubu alipongeza ushirikiano uliopo na kuongeza kuwa fursa zaidi za ushirikiano bado zipo hususan katika shahada za uzamili na uzamivu ambazo hazijaanza kutolewa na chuo hicho.
IMG-20240913-WA0010.jpg
Aidha, Balozi Yakubu alipendekeza Chuo hicho kuangalia uwezekano wa kushirikiana na vyuo vya Tanzania ili kuanzisha taasisi zitakazotoa kozi za kitaaluma kama vile Uhasibu na Tehama badala ya utaratibu wa sasa ambapo wanafunzi wa Comoro lazima kuchukua kozi za kitaaluma toka nchi za jirani.

Viongozi hao walikubaliana pia kuratibu ziara za viongozi na wadau wa sekta ya Elimu.
 

Attachments

  • IMG-20240913-WA0011.jpg
    IMG-20240913-WA0011.jpg
    73.5 KB · Views: 4
  • IMG-20240913-WA0013.jpg
    IMG-20240913-WA0013.jpg
    80.2 KB · Views: 2
  • IMG-20240913-WA0009.jpg
    IMG-20240913-WA0009.jpg
    78.3 KB · Views: 2
Back
Top Bottom