Sabi Sanda
JF-Expert Member
- Mar 7, 2006
- 409
- 31
Natumaini wote tumesikia kazi ambayo Profesa Maboko wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam amepewa na timu yake ya kufanya uchuguzi wa kina kuhusu mfumo mzima wa utoaji mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu na kisha kutoa mapendekezo kuhusu namna bora ya kumaliza tatizo la utoaji mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu na kuhakikisha kuwa bodi ya mikopo inakuwa na ufanisi uliotukuka.
Matumaini yangu ni kuwa wataanza kwanza kwa kupata taarifa kamili kuhusu utumwaji wa fedha toka Hazina kwenda bodi ya mikopo na kuona kama kuna udhaifu wowote hapo. Kwa upande mwingine, wataangalia kwa kina na kuona kwa kiwango gani vyuo vinatimiza wajibu wao kwa wakati kuhusu suala hili la mikopo kwa wanafunzi wao.
Mbali na ucheleweshaji wa mara kwa mara wa mikopo kwenda kwa wanafunzi, moja ya eneo ambalo wanafunzi wamekuwa wakililalamikia sana ni suala la MEANS TEST.
Badala ya kutumia MEANS TEST ili kujua mwanafunzi husika anastahili asilimia kiasi gani, napendekeza kiwango cha ufaulu wa mwanafunzi husika katika somo la Hisabati ngazi ya kidato cha nne ndiyo kiwe kigezo kikuu. Iwapo wazo hili litakubalika mapendekezo ni kuwa:-
1. Mwanafunzi atakayepata A apate mkopo kwa asilimia 105--Asilimia tano ya ziada hapa itolewe kama Motisha.
2. Mwanafunzi atakayepata B apewe asilimia 85. Pia hapa asilimia 5 itolewe kama motisha.
3. Mwanafunzi atakayepata alama ya C apate mkopo kwa asilimia 65. Pia hapa asilimia 5 iwe kama motisha.
4. Mwanafunzi atakayepata alama ya D apate asilimia 20 tu ya mkopo.
5. Na mwisho, mwanafunzi atakayepata F apate asilimia 000 ya mkopo.
Matumaini yangu ni kuwa wataanza kwanza kwa kupata taarifa kamili kuhusu utumwaji wa fedha toka Hazina kwenda bodi ya mikopo na kuona kama kuna udhaifu wowote hapo. Kwa upande mwingine, wataangalia kwa kina na kuona kwa kiwango gani vyuo vinatimiza wajibu wao kwa wakati kuhusu suala hili la mikopo kwa wanafunzi wao.
Mbali na ucheleweshaji wa mara kwa mara wa mikopo kwenda kwa wanafunzi, moja ya eneo ambalo wanafunzi wamekuwa wakililalamikia sana ni suala la MEANS TEST.
Badala ya kutumia MEANS TEST ili kujua mwanafunzi husika anastahili asilimia kiasi gani, napendekeza kiwango cha ufaulu wa mwanafunzi husika katika somo la Hisabati ngazi ya kidato cha nne ndiyo kiwe kigezo kikuu. Iwapo wazo hili litakubalika mapendekezo ni kuwa:-
1. Mwanafunzi atakayepata A apate mkopo kwa asilimia 105--Asilimia tano ya ziada hapa itolewe kama Motisha.
2. Mwanafunzi atakayepata B apewe asilimia 85. Pia hapa asilimia 5 itolewe kama motisha.
3. Mwanafunzi atakayepata alama ya C apate mkopo kwa asilimia 65. Pia hapa asilimia 5 iwe kama motisha.
4. Mwanafunzi atakayepata alama ya D apate asilimia 20 tu ya mkopo.
5. Na mwisho, mwanafunzi atakayepata F apate asilimia 000 ya mkopo.