Professor J na Sugu ndani ya Mpambano mkali wa nani zaidi ya Radio one.

Freed Freed

JF-Expert Member
Joined
Jun 27, 2017
Posts
6,547
Reaction score
7,167
Habari wanajukwaa. Wasanii nguli walio pia wanasiasa, Joseph Haule na Joseph Mbilinyi wanapambanishwa ndani ya radio one nani zaidi jumapili hii. Muda huu watu wanapiga simu kutoa maoni nani zaidi. Nyimbo zao za enzi hizo zimepigwa na kubamba ile mbaya. Sugu kapata kura 2 na Professor J amepata kura 16.Hii ni kwa mujibu wa watu waliopiga simu.
 
Hawa jamaa walifanya kazi kubwa sana ya muziki hapa tz. walichangia sana kuiondoa ile dhana ya wazazi kwamba kujiingiza ktk muziki ni sawa na kujiunga kwenye vikundi vya kihuni.
 
Hicho kipindi kilibamba sana enzi zileee. Akati kofi olomide alivyokua anapambanishwa na wenge musica.
 
Jay anatisha aisee na ile ngoma yake ya machozi jasho na damu
 
Jay kwangu mm ni zaidi japo wote walipambana ili bongo fleva ikubalike na kweli kazi zao ni nzuri na walifanikiwa
 
Nakuchapa kiuchumi nakuchapa kisiasa , show za kibabe show za kibabeee...Prof jizeeee
 
Sugu hakuna kitu labda wawashindanishe kisiasa ndio Sugu atampita Profesa ila kimziki huko ni kumtukana Jay.

Sugu hajawahi kutoa Nyimbo ikawa wimbo wa Taifa ila Jay utakuta ngoma kama "Zali la Mentali,Ndio mzee,Nikusaidieje,Bongo Dar es salaam zote zilikwenda kuwa Hit Song ila Sugu alikuwa anaimba kihuni sana.
 
Hivi mzee Mengi ni kwamba amejizira hivi? Yaani redio zake hazifuatiliwi kabisa na vijana wala hazina mvuto , kwanini lakini mzee? Yaani mzee we wakuzidiwa na efm iliyokuja juzi tu?

Mzee ajiri timu mpya za vizazi vipya waje wafufue redio one ,mwaga mpunga unamng'oa hata Kipanya clouds au Kibonde hata kama hawana elimu ili wana ujuzi wa figisu za mjini na wana damu changa za kiburudani
 

Za Sugu naona zilikuwa kigumu zaidi wakati za Jay Nilikuwa bongo flava zaidi za kuimbika.

Hit song za Sugu Deiwaka, wanamuita Sugu, anamiaka chini ya18 , niko mikononi mwa polisi ,etc
Hivi nani ana album nyingi kati yao? Mzitaje mnaojua
 

Za Sugu naona zilikuwa kigumu zaidi wakati za Jay Nilikuwa bongo flava zaidi za kuimbika.

Hit song za Sugu Deiwaka, wanamuita Sugu, anamiaka chini ya18 , niko mikononi mwa polisi ,etc
Hivi nani ana album nyingi kati yao? Mzitaje mnaojua
 
Sugu mashairi yake yanauhalisia sana. Hayapambipambi hadi yapoteze uhalisia. Akichana unajua kabisa anamaanisha.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…