Programme zinazoanzishwa vyuoni, ni wajibu wa nani kuzipeleka kwenye soko la ajira?

Programme zinazoanzishwa vyuoni, ni wajibu wa nani kuzipeleka kwenye soko la ajira?

A

Anonymous

Guest
Kuna programme mpya zinaanzishwa vyuoni hasa vyuo vikuu lakini hazijulikani kwa waajiri. Programme hizi zinaweza kuwa zinampa vigezo mtu aliyechukua hizo programme lakini anashindwa kupata kazi kwa sababu waajiri hawazitambui na akienda kuomba kazi wanamwambia wanahitaji mtu aliyesoma programme fulani.

Kwa mfano: Mtu aliyesoma Bachelor of Arts in Literature anaweza kufanya kazi kama tutor (tutorial assistant) wa masomo ya communication skills lakini soko halimtambui mtu huyu.

Binafsi nimesoma hiyo course na kwasasa nafanya kazi kama part-time wa hilo somo kwenye moja ya chuo cha kati hapa nchini. Changamoto ninayoipata pamoja na wengine waliosoma hii course ni kutotambulika kwenye soko la ajira linapokuja suala la kufundisha communication skills.

Niliwahi kwenda kwenye ofisi za ajira kuwauliza kwanini mfumo wa ajira unatutema wakati tuna vigezo? Niliambiwa kuwa wao wanaweka vigezo walivyopewa na taasis inayotaka kuajiri na sio wao wanaotengeneza vigezo. Je! Ni nani ana jukumu la kuwataarifu waajiri kuwa waliosoma programme fulani wana sifa za kufanya kazi fulani?

Baada ya kutoka utumishi na kupewa hayo majibu nilimtafuta mkufunzi kutoka kwenye department ya Literature (UDSM) na kumueleza hii changamoto akasema sisi (wahitimu wa hii programme) tukaongee na utumishi. Nikamwambia utumishi nimeishaenda na majibu niliyopewa nikampa. Niliona kabisa anapata kigugumizi juu ya hii changamoto japo alisema watalijadiri idarani.

Nimetolea mfano programme niliyosoma lakini zipo programme nyingi sana vyuoni hasa programme mpya ambazo hazitambuliki kwa waajiri hivyo kuwafanya waliosoma hizo programme kuwa na machaguo machache sana kwenye soko la ajira.

Kuna kila haja ya vyuo kuiangalia hii changamoto na kuitafutia ufumbuzi hasa kuzifanya hizi programme zijulikane kwa waajili. Hii inawezekana maana karibia vyuo vyote vina kitengo cha masoko (marketing) ambacho kinabidi kiende mbali zaidi na kuzitangaza programme zinatolewa na chuo kwa waajiri.
 
Zipo programs nyingi ambazo kimsingi graduates wake wananyimwa fursa kwasababu ya kutotambulika lakini pia ukweli ni kwamba BA Literature huwezi kuwa TA wa Communication Skills kwasababu huwezi kuwa na content kubwa kwenye Communication skills kama aliyesoma BA Linguistics/English japo kuna courses mnashare. Wewe subiri zitangazwe za TA Literature ndo uombe.
 
Sio kweli, kama mtu amesoma literature na ameopt course za linguistic ana vigezo vya kufundisha cTA ya communication skills.
Nasema hivi kwasababu nafundisha communication skills kama TA. Mitaala mingi iayotumiwa vyuo vya kati haipo nje ya knowledge aliyonayo mtu wa literature. Baadhi ya module ni grammar (parts of speech, phrases, clauses and sentence) hivi vitu vyote kwa mtu aliyesoma literature na akaopt course za linguistics amevisoma.
pia module nyingine ni communication skills (verbal com, non-verbal com, written com, reading, etc) hizi pia mtu aliyesoma literature amesoma so kwenye qulifications anabidi azingatiwe akapambane kama wengine.
 
Kuna programme mpya zinaanzishwa vyuoni hasa vyuo vikuu lakini hazijulikani kwa waajiri. Programme hizi zinaweza kuwa zinampa vigezo mtu aliyechukua hizo programme lakini anashindwa kupata kazi kwa sababu waajiri hawazitambui na akienda kuomba kazi wanamwambia wanahitaji mtu aliyesoma programme fulani.

Kwa mfano: Mtu aliyesoma Bachelor of Arts in Literature anaweza kufanya kazi kama tutor (tutorial assistant) wa masomo ya communication skills lakini soko halimtambui mtu huyu.

Binafsi nimesoma hiyo course na kwasasa nafanya kazi kama part-time wa hilo somo kwenye moja ya chuo cha kati hapa nchini. Changamoto ninayoipata pamoja na wengine waliosoma hii course ni kutotambulika kwenye soko la ajira linapokuja suala la kufundisha communication skills.

Niliwahi kwenda kwenye ofisi za ajira kuwauliza kwanini mfumo wa ajira unatutema wakati tuna vigezo? Niliambiwa kuwa wao wanaweka vigezo walivyopewa na taasis inayotaka kuajiri na sio wao wanaotengeneza vigezo. Je! Ni nani ana jukumu la kuwataarifu waajiri kuwa waliosoma programme fulani wana sifa za kufanya kazi fulani?

Baada ya kutoka utumishi na kupewa hayo majibu nilimtafuta mkufunzi kutoka kwenye department ya Literature (UDSM) na kumueleza hii changamoto akasema sisi (wahitimu wa hii programme) tukaongee na utumishi. Nikamwambia utumishi nimeishaenda na majibu niliyopewa nikampa. Niliona kabisa anapata kigugumizi juu ya hii changamoto japo alisema watalijadiri idarani.

Nimetolea mfano programme niliyosoma lakini zipo programme nyingi sana vyuoni hasa programme mpya ambazo hazitambuliki kwa waajiri hivyo kuwafanya waliosoma hizo programme kuwa na machaguo machache sana kwenye soko la ajira.

Kuna kila haja ya vyuo kuiangalia hii changamoto na kuitafutia ufumbuzi hasa kuzifanya hizi programme zijulikane kwa waajili. Hii inawezekana maana karibia vyuo vyote vina kitengo cha masoko (marketing) ambacho kinabidi kiende mbali zaidi na kuzitangaza programme zinatolewa na chuo kwa waajiri.

Ninadhani kwenye bold ulimaanisha Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma. Kwa uelewa wangu, key player kwenye suala hilo ni Wizara yenyewe yani Ofisi ya Rais - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora. Jaribu kuwaandikia wao kuaddress hilo suala maana kwenye scheme of work ndio huwa inaelezwa taasisi inahitaji mtaalam gani na awe ana sifa zipi za kielimu ili awe kukidhi matakwa ya kufanya kazi katika position hiyi.

Aidha, kama OR-UTUMISHI wamo humu, wajaribu kufanya kazi kwa karibu na Wizara za Elimu na Wizara nyingine zinazohusiana na mambo ya elimu ili ikiwezekana ile framework kubwa kabisa ya workforce ya nchi iwe inahuishwa mara kwa mara kuaccomodate taaluma mpya zinazokuja ili tusijekulimit watu wenye uwezo kisa tu hawajsoma course fulani wakati ukiangalia contents knowledge ambayo mwisho wa siku mtu ataipata ni ile ile kwa wastani.


Kama wameruhusu mtu aliesoma Political Science and Public Adminsitration aajiriwe kama HR, nadhani inawezekana kabisa kwa mtu aliesoma Bachelor of Arts in Literature akafanya kazi kama mkufunzi wa Communication Skills.
 
Ukija kwa upande wa Zanzibar course ya Agricultural Economics ambayo inafundishwa SUA na UDSM hazijulikani katika portal ya ajira yni ni mtihani tuu wakati kwa upande wa bara zinajulikana dah inauma
 
Hapo kwenye kuiandikia barua Sekretarieti ya Ajira naona inaweza kuwa initiative nzuri. Asante kwa hoja.
 
Duh yan AEA ya SUA znz aijulikani ni aibu.
Ukija kwa upande wa Zanzibar course ya Agricultural Economics ambayo inafundishwa SUA na UDSM hazijulikani katika portal ya ajira yni ni mtihani tuu wakati kwa upande wa bara zinajulikana dah inauma
u
 
Kuna programme mpya zinaanzishwa vyuoni hasa vyuo vikuu lakini hazijulikani kwa waajiri. Programme hizi zinaweza kuwa zinampa vigezo mtu aliyechukua hizo programme lakini anashindwa kupata kazi kwa sababu waajiri hawazitambui na akienda kuomba kazi wanamwambia wanahitaji mtu aliyesoma programme fulani.

Kwa mfano: Mtu aliyesoma Bachelor of Arts in Literature anaweza kufanya kazi kama tutor (tutorial assistant) wa masomo ya communication skills lakini soko halimtambui mtu huyu.

Binafsi nimesoma hiyo course na kwasasa nafanya kazi kama part-time wa hilo somo kwenye moja ya chuo cha kati hapa nchini. Changamoto ninayoipata pamoja na wengine waliosoma hii course ni kutotambulika kwenye soko la ajira linapokuja suala la kufundisha communication skills.

Niliwahi kwenda kwenye ofisi za ajira kuwauliza kwanini mfumo wa ajira unatutema wakati tuna vigezo? Niliambiwa kuwa wao wanaweka vigezo walivyopewa na taasis inayotaka kuajiri na sio wao wanaotengeneza vigezo. Je! Ni nani ana jukumu la kuwataarifu waajiri kuwa waliosoma programme fulani wana sifa za kufanya kazi fulani?

Baada ya kutoka utumishi na kupewa hayo majibu nilimtafuta mkufunzi kutoka kwenye department ya Literature (UDSM) na kumueleza hii changamoto akasema sisi (wahitimu wa hii programme) tukaongee na utumishi. Nikamwambia utumishi nimeishaenda na majibu niliyopewa nikampa. Niliona kabisa anapata kigugumizi juu ya hii changamoto japo alisema watalijadiri idarani.

Nimetolea mfano programme niliyosoma lakini zipo programme nyingi sana vyuoni hasa programme mpya ambazo hazitambuliki kwa waajiri hivyo kuwafanya waliosoma hizo programme kuwa na machaguo machache sana kwenye soko la ajira.

Kuna kila haja ya vyuo kuiangalia hii changamoto na kuitafutia ufumbuzi hasa kuzifanya hizi programme zijulikane kwa waajili. Hii inawezekana maana karibia vyuo vyote vina kitengo cha masoko (marketing) ambacho kinabidi kiende mbali zaidi na kuzitangaza programme zinatolewa na chuo kwa waajiri.
Hii ni changamoto kubwa sana kwenye ajira portal, unakuta imetangazwa nafasi especially hizi za kufundisha unakuta field husika unaomba inakukatalia wakati anayekubaliwa mumesoma kitu kimoja tu. Inashangaza sana, na unakuta unakuta mtu ana vigezo, na ujuzi katika somo au position husika lakin kwa sababu title ya program yake haipoidentified kwenye post husika anatemwa nje
 
Mfano inawezatangazwa post anahitajika Tutorial assistant in "ethics" af ikawa limited program moja tu, wakati zipo program nyingi zimesoma tu hiyo Ethics, na mathalani hakuna program ya ethics level ya bachelor kwanini wasiruhusu wenye qualification wote wakaomba tu watachuja huko!
 
Back
Top Bottom