Project funding sources


Mkuu mimi nitakutafuta,sisi wapenda kilimo hapa ndo penyewe.
 

Mkuu jumanne nitakuwa dar,je tunaweza kupanga kuonana,mambo mengine yanahitaji action tu.
 
Mkuu jumanne nitakuwa dar,je tunaweza kupanga kuonana,mambo mengine yanahitaji action tu.


Mimi nipo safari kidogo lakini yupo member tunayefanya nae hii plan anaweza kuonana na wewe bila shaka mkuu!
 
Mzuzu,

Niko kwenye kesi kama yako. Nataka kufanya project ila sema ni tofauti kabisa. Umenipa nguvu ya kutokata tamaa. Hongera kwa kutupa wengine ari ya kuumiza kichwa na kusonga mbele.

Kumbuka ukifanikiwa basi itakuwa moja ya project itakayoonyesha kuwa JF ni kweli Jamii forum. Si kupita na kuongea blaa blaa siku zote. Baada ya kukatishwa na wanasiasa jana, leo nimeisoma hii habari na kunipa faraja. Kweli Watanzania tunaanza kuamka. Kwenye njia pana njia. Tatizo wengi hutaka kupita short cut kwa kutapeli au kuiba. Wengine wanaamua kuomba kazi ya kulala bungeni na kuchukua posho mbili mbili. Hizi siku zikiisha, watabaki watu kama wewe wenye kutaka kuiletea maendeleo ya kweli Tanzania.

Ngoja niitunze hii thread kwa future. Itakuja kuwa ni Bench Mark ya kuanzia kupata mawazo ya mwenzetu alianzia wapi na kafikia wapi. Na kama alikwama basi alikwama wapi. Documents zote mkuu uziweke na ikibidi huko mbeleni uje uwawekee wengine wapate shule ya BURE (kama utataka).

Again, all the best.
 
Mzuzu
naomba e_mail yako.
Nahitaji kuwasiliana na wewe.
 

Hapo kwenye blue colour. Mimi nilishathibitisha zamani kuwa jf ni kwa ajili ya jamii. Kupitia jf mimi nimepata members watano ktk project moja ninayofanya. Wengi wameibiwa mno kiasi kwamba kati ya watu kumi unaweza kupata waaminifu -ve kabisa. Ila wapo vijana wenye fedha na idea nzuri wamekosa partiners ktk biashara na miradi.

Avatar yako nimeipenda sana, naifanyia kazi sasa hivi.
 
kwa kweli na mimi nimefarijika sana na mawazo ya wana-JF. kama inavyojulikana kupata mkopo benki ni next to impossible hasa unapokuwa unaanza na huna track record ya bank.
so the only option ni kuunganisha nguvu.!!
kikubwa ni kuendelea kupeana taarifa na links!!
mbarikiwe
 
Ipime ardhi na uipatie hati miliki itakuwa ni security tosha na utapata mkopo
Asante sana kwa mawazo yenu, mie pia ninajaribu ingawa anavyosema Malila nimeanzia small scale, sasa nilinunua ardhi nijitanue kidogo lakini nimeingia mgogoro na mhindi mmoja mbaye ameibuka na kusema heka 400 nzima za kijiji ni zake, suala hili analishughulikia mbunge wetu mahakama ya ardhi, ila inaenda slow, nimekata tamaa nao, sasa ningependa kushika tena ardhi ili niweze kuendelea na mradi wangu ila nahofia hii kutokea tena.
Je nikitaka kusajili shamba ninaanzia wapi, nimeonyeshwa wilaya ya Kibaha ni ardhi nzuri, naomba mnisaidie hapa.
 

Kimsingi ukitaka kusajili ardhi ambayo unaimiliki kimila inabidi uanzie kijiji husika,unakwenda kwa bwana ardhi wa Wilaya(mijini hakuna mashamba) ambaye atakupa mipango iliyopo ya matumizi husika kwa ardhi unayotaka kuomba,kwa hiyo ukitoka pale yeye ndio atakwambia pa kwenda,kama ni wizarani au idara gani nyingine( kama ofisi za Kanda).

Kibaha si pazuri kwa mtu anayeanza,sehemu kubwa ya ardhi yake ni mali ya watu,unaweza kutapeliwa. Nenda nje ya mji kabisa kama Ngerengere,Kidugalo,Mkuranga etc.
 

Malila,

Hiyo ni kawaida kabisa duniani kote.

Kuna jamaa yangu aliniambia jinsi jamaa mmoja huko majuu alivyodanganywa na kuachwa hoi. Alikuwa ashirikiane na Wageruman katika ujenzi wa highyway. Akachukua Mkopo mkubwa sana na kununua vifaa vya hela nyingi sana. Pesa zilikuwa zizje kutoka kwa Wajeruman kwa ajili ya kugharamia gharama zote kwa siku za mwanzo. Jamaa wakajitoa na jamaa akabaki na vifaa bila kujua afanye nini. Nasikia alikuwa kasimama kwenye BMW lake kali sana na analia kuwa "nimefilisika".

Hivyo hilo la waaminifu na wasio waaminifu inabidi ujaribu kulipunguza maana hutakuja kufanya kitu wala kuowa.

Juu ya AVATAR, yaani hiyo picha, kama kweli umeipenda basi naweza kukutumia yenye HIGH QUALITY maana nilipiga mwenyewe na ninayo hiyo picha. NiPM na uweke email yako ntakutumia bila wasiwasi.

Vinginevyo niseme ni vizuri kufahamu watu unaoweza hata kuwaomba mawazo na ushauri. Tuko pamoja kwa hili na niwatakie tena mafanikio mema ili muwe moja ya Bench Mark (point of reference) ya JF.
 
Malila na wengine:

Yule Mhindi aitwaye Professor Muhammad Yunus kama sikosei (alishinda Noble price) alianzisha Bank ambayo anatoa mikopo / Misaa midogo midogo. Hivi badala ya watu kufikiri kuvuna na kupanda mbegu kama DECI? si ingelikuwa vema kuanzisha benki ya Watanzania (bila kuihusisha serikali) ambayo ingelikuwa ikitoa misaada kama hii wengi wanalilia hapa?

Masharti yangelikuwa kwamba, mtu anayetaka Mkopo inabidi aanze kidogo kidogo kukopa na kulipa na hadi kule mbele awe na uwezo wa kukopa na kulipa hela nyingi. Hakuna member mmoja kuwa na asilimia kubwa maana itakuwa ya mtu mmoja. Na kila mkopo ukitoka kwenye mradi, Bank inakuwa member wa huo mradi hadi pale jamaa atakapolipa deni na riba yake na ndipo anaachiwa na kujitegemea wenyewe.

Kuna haja ya kurudisha Bank ya Biashara ya (WA)Tanzania.
 

Mimi siogopi kihivyo,ila najaribu kuwatahadharisha watu juu ya tatizo hili la maadili. Nimepata uzoefu mkubwa kwa kukumbana na matatizo kama hayo,mnaanza mradi,patiner wako ni mlevi au mvivu,mzinzi nk. Asante mkuu.
 

Mkuu umepotea kabisa sikupati tena!
 
HTML:
MZUZU unaweza kunicheck kwa email:

baraka.baraka@yahoo.com

HTML:
Haina shaka mkuu wangu nakucheck sasa hivi


Mbona kimya mkuu?
 
HTML:
MZUZU unaweza kunicheck kwa email:
 
baraka.baraka@yahoo.com

HTML:
Haina shaka mkuu wangu nakucheck sasa hivi


Mbona kimya mkuu?


Mbona nilikucheck kwenye hiyo yahoo yako kitambo sana??
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…