PSSSF yatoa ufafanuzi madai kuwa kuna changamoto ya huduma katika Tawi la Arusha

PSSSF yatoa ufafanuzi madai kuwa kuna changamoto ya huduma katika Tawi la Arusha

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
Majibu malalamiko Arusha 1_page-0001.jpg
Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) umetoa ufafanuzi kuhusu hoja iliyotolewa na Mwanachama wa JamiiForums.com aliyedai kuwa Mamlaka husika zichukue hatua juu ya Tawi la Arusha anapodai kuna huduma zisizoridhisha na kwamba wamekuwa hawawajali Wateja.

Kusoma zaidi alichoandika Mdau bofya hapa ~ Serikali tunaomba muitazame upya PSSSF Branch ya Arusha, huduma ziboreshwe

UFAFANUZI KUHUSU MADAI YA TATIZO PSSSF ARUSHA
Kwenye ukurasa wa Jamii Forums, kuna taarifa yenye kichwa "Kuna Tatizo PSSSF Arusha." Taarifa hiyo inadai kuwa wanachama watatu wamefuatilia mafao yao kwa muda mrefu, na wawili kati yao wanasemekana kufariki dunia wakiwa bado wanashughulikia mafao yao kupitia Ofisi yetu ya Kanda ya Kaskazini, jijini Arusha.

Awali ya yote, tunapenda kutoa pole kwa familia, ndugu, jamaa, na marafiki wa wanachama wetu iwapo kweli wapo waliopoteza maisha wakiwa katika mchakato wa kufuatilia mafao yao.

Aidha, uchambuzi wa madai yaliyotolewa unaonyesha kuwa yamejikita zaidi kwenye dhana ya kufikirika ambayo haiwezi kusaidia mlalamikaji wala Mfuko katika kutatua tatizo lolote endapo lipo.

Hata hivyo, ipo sababu moja kuu inayoweza kusababisha ucheleweshaji wa malipo kwa mwanachama, ambayo ni ukosefu wa nyaraka au taarifa muhimu zinazohitajika kutoka kwa mwanachama husika.

Kwa lengo la kutatua changamoto yoyote inayoweza kuwepo, Mfuko unatoa rai kwa mlalamikaji kupiga simu bure kupitia namba 0800 110040 ili kutupatia taarifa kamili za wahusika. Hii itatuwezesha kuchunguza suala hili kwa kina na kuhakikisha linashughulikiwa ipasavyo.

Mfuko wa PSSSF unajitahidi kila siku kutoa huduma bora kwa wanachama wake, na dhamira yetu ni kuhakikisha malalamiko au changamoto yoyote inatatuliwa haraka na kwa ufanisi.

Imetolewa na:
Yessaya Mwakifulefule
Meneja Uhusiano na Elimu kwa Umma
 
Kama una mzazi anafuatilia mafao PSSSF tafadhali sana uwe unamsindikiza. Nilishuhudia wazee wakiwa treated vibaya sana kwa sababu tu hawana nguvu tena, hawezi kujipigania na hawajui haki zao. Wazee wanakalishwa kuanzia asubuhi mpaka jioni bila kujali hata afya zao hasa wale wanaoumwa, na lugha zinazotumika na wafanyakazi sio za upole bali wazee wanagombezwa kama watoto.
Hii niliona ktk tawi lao moja Kanda ya ziwa, nikawaza sana 😭😭
 
Kama una mzazi anafuatilia mafao PSSSF tafadhali sana uwe unamsindikiza. Nilishuhudia wazee wakiwa treated vibaya sana kwa sababu tu hawana nguvu tena, hawezi kujipigania na hawajui haki zao. Wazee wanakalishwa kuanzia asubuhi mpaka jioni bila kujali hata afya zao hasa wale wanaoumwa, na lugha zinazotumika na wafanyakazi sio za upole bali wazee wanagombezwa kama watoto.
Hii niliona ktk tawi lao moja Kanda ya ziwa, nikawaza sana 😭😭
Wanao fanya ivyo ni hawa hawa wanao lilia ajira waki pata wanasahau wanakua na dharau
 
Natamani kufahamu hizo nyaraka muhimu zinazohitajika ili mnyonge apewe shekeli zake.

Kuungwa hawakuombi chochote, tena wanaanza kukata automatic, ila kutoa hadi upeleke rundo la nyaraka
 
Sasa nyaraka muhimu zipi ninyi @psssf, kwani wakati mnakata hiyo michango mlikata Kwa nyaraka zipi!? Mimi nashauri psssf watungiwe sheria kuwa pale mtumishi anapostaafu on the spot mafao yake yawe yameshalipwa ,wakati mnakata makato hamkuniomba nyaraka ila nikianza kufuatilia mlichokuwa mnanikata mnadai nyaraka,huu sio uungwana hata kidogo.
 
Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) umetoa ufafanuzi kuhusu hoja iliyotolewa na Mwanachama wa JamiiForums.com aliyedai kuwa Mamlaka husika zichukue hatua juu ya Tawi la Arusha anapodai kuna huduma zisizoridhisha na kwamba wamekuwa hawawajali Wateja.

Kusoma zaidi alichoandika Mdau bofya hapa ~ Serikali tunaomba muitazame upya PSSSF Branch ya Arusha, huduma ziboreshwe

UFAFANUZI KUHUSU MADAI YA TATIZO PSSSF ARUSHA
Kwenye ukurasa wa Jamii Forums, kuna taarifa yenye kichwa "Kuna Tatizo PSSSF Arusha." Taarifa hiyo inadai kuwa wanachama watatu wamefuatilia mafao yao kwa muda mrefu, na wawili kati yao wanasemekana kufariki dunia wakiwa bado wanashughulikia mafao yao kupitia Ofisi yetu ya Kanda ya Kaskazini, jijini Arusha.

Awali ya yote, tunapenda kutoa pole kwa familia, ndugu, jamaa, na marafiki wa wanachama wetu iwapo kweli wapo waliopoteza maisha wakiwa katika mchakato wa kufuatilia mafao yao.

Aidha, uchambuzi wa madai yaliyotolewa unaonyesha kuwa yamejikita zaidi kwenye dhana ya kufikirika ambayo haiwezi kusaidia mlalamikaji wala Mfuko katika kutatua tatizo lolote endapo lipo.

Hata hivyo, ipo sababu moja kuu inayoweza kusababisha ucheleweshaji wa malipo kwa mwanachama, ambayo ni ukosefu wa nyaraka au taarifa muhimu zinazohitajika kutoka kwa mwanachama husika.

Kwa lengo la kutatua changamoto yoyote inayoweza kuwepo, Mfuko unatoa rai kwa mlalamikaji kupiga simu bure kupitia namba 0800 110040 ili kutupatia taarifa kamili za wahusika. Hii itatuwezesha kuchunguza suala hili kwa kina na kuhakikisha linashughulikiwa ipasavyo.

Mfuko wa PSSSF unajitahidi kila siku kutoa huduma bora kwa wanachama wake, na dhamira yetu ni kuhakikisha malalamiko au changamoto yoyote inatatuliwa haraka na kwa ufanisi.

Imetolewa na:
Yessaya Mwakifulefule
Meneja Uhusiano na Elimu kwa Umma
Hizi nyaraka lukuki mnazodai ni urasimu usio na maana wakati mtu akileta barua yake ya kuajiriwa na kukoma ajira na kitambulisho Cha taifa vinatosha kwani hamuweki record kwa njia ya electronic
 
Huwa siwaelewewi mnaposema walete nyaraka ili wapate sifa ya kupewa mafao yao ina maana ninyi mlikua mnawakata watu wasiokua na sifa. vitambulisho ni NIDA na barua ya mwajiri hao wastaafu wanafatilia kila kukicha hapo Arusha mnahitaji nini tena au vyeti halisi vya shule ndio inafanya wachelewe kupata stahiki zao?
 
Back
Top Bottom