Punda hataki aitwe punda

Mabel

JF-Expert Member
Joined
Sep 1, 2010
Posts
1,276
Reaction score
684
Siku moja PUNDA alikutana na Simba faragha kutoa malalamiko yake kuhusiana na wanyama wengine juu yake, mazungumzo yalikuwa hivi:

Punda: Wenzangu wanadai eti mimi sio MWEREVU ndio maana wananiita PUNDA!
Simba: Sasa wewe hutaki jina hilo na unataka nini?

Punda: Nataka uwakataze wasiniite tena jina hilo kwani mimi ni MWEREVU sana!
Simba: Sawa mimi nitawakataza ila kabla nataka nikupe kamtihani kadogo ili nihakikishe kweli wewe ni MWEREVU au la, uko tayari?

Punda: Ndiyo!
Simba: Sasa nenda nyumbani kwangu ukaniangalie kama nipo halafu urudi kunipa jibu

Basi PUNDA akatimua mbio kuelekea nyumbani kwa mfalume wa pori kumangalia kama yupo nyumbani kwake na punde akarudi

Simba: Umenikuta nipo nyumbani kwangu?
Punda: Aisee bwana sijakukuta, haupo!

Simba: Wewe ni punda na utaendelea kuitwa PUNDA daima, potea hapa!

Basi PUNDA akaondoka kwa unyonge
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…