SoC04 Punguzo la tozo namba za usajili maalum za magari katika kuongeza pato la Serikali Tanzania

SoC04 Punguzo la tozo namba za usajili maalum za magari katika kuongeza pato la Serikali Tanzania

Tanzania Tuitakayo competition threads

Malick M. Malick

JF-Expert Member
Joined
Apr 2, 2013
Posts
658
Reaction score
312
Katika Nchi tuna utaratibu wa kila chombo cha Moto kupata usajili kupata namba maalumu [maalufu kama Plata Namba]

Kwa magali tunaanza na T AAA na Sasa Tupo T EAA ,na Pikipiki zinaanza MC [Vyombo vya miguu miwili au mitatu ] MC ambayo zina gharama za kawaida

Ila serikaĺi imeweka utaratibu kwa namba maalumu za kulipia kwa vyombo vya moto vya miguu minne [Magari ] ambayo ni Tsh 5000,000 [Milioni 5 ) Kwa miaka 3

Maana serikali inapata watumiaji wachache hivyo kukusanya mapato machache

Ushauri wangu kwa serikali ingeweka kiwango cha Tsh 100,000 kwa mwezi ingepata watumiaji wengi kwa mwezi pato la makusanyo yangekua makubwa sana kwa mwezi na kwa mwaka pato lingekua kubwa zaidi

Maana wateja wangekua wengi sana na pato la serikali lingekua kubwa sana kupitia tozo hiyo ya pleti namba, Taifa lingekusanya mapato mengi na kupunguza tozo kwenye maeneo mengine

Maana swala la pleti namba maalumu ni hiyari sio la lazima hivyo kuwafanya watu kuchagia pato la serikali kwa hiyari

Ukichua idadi ya magari yaliyopo Tanzania na idadi ya magari yanayo ingia maana yake watumiaji wa huduma hiyo wataongezeka sana kwa nchi yetu na kuongeza pato kubwa kwa Taifa letu

Pia serikali ipunguze kodi ya uingizaji wa magari chakavu [Used] yanayonunuliwa kutoka nje ili magari mengi yaingie nchini ,magari yanapokua mengi nchini matumizi ya mafuta yanaongezeka maana yake serikali itakusanya kodi nyingi kwenye lita za mafuta yanayotumika katika nchi na kuongeza mapato ya serikali kwa sababu matumizi ya mafuta [ni chanzo cha uhakika cha mapato ya serikali]

Pia serikali ifute kodi zote kwenye mashine mbalimbali zinazotumika katika uzalishaji ili kuwafanya watanzania wengi kuanzisha viwanda vingi vidogo vidogo ambayo vinatoa ajira kubwa kwa watanzania wengi na kuongeza pato la Taifa

Mwisho Kama Nchi inatakiwa kupitia kodi zetu zote katika bidhaa na kuzirekebisha kwa sababu bidhaa nyingi nchini zinakua bei kubwa kwa sababu kodi zetu na mfumo wa kodi wetu haujawa mzuri lazima tuwe na sera ya Kodi kama Taifa ili kuzuia Kodi zetu kuondoa kuwa sio rafiki kwa wote watoa huduma wote na mwisho kuzifanya bidhaa au huduma kuwa juu mlaji wa mwisho
Jina :Malick Maliki
 
Upvote 2
Naunga mkono wazo hili ,serikali ikilichukua itasaidia kupunguza kuwakamua wananchi kwenye tozo za mafuta ,na miamala ya simu

Kwasababu namba maalumu ni hiyari hivyo itaongeza watumiaji kuna mtu ananua gari namba A ,kukiwa na usajili bei nafuu ,atalipia usajili huo kuficha namba A ,mtu ataamua kuweka jina lake kwenye plate namba
 
Back
Top Bottom