Wauaji waliopatikana na hatia na wauzaji dawa za kulevya ambao wametoka gerezani hivi majuzi nchini Urusi wanakabiliwa na kuandikishwa kupigana nchini Ukraine chini ya mabadiliko ya sheria.
Rais Vladimir Putin aliifanyia marekebisho sheria ya kuwaita askari wa akiba na kuwajumuisha wanaume waliopatikana na hatia ya uhalifu mkubwa ambao walitoka gerezani hivi majuzi.
Wafungwa wa zamani waliopatikana na hatia ya uhalifu wa ngono dhidi ya watoto au ugaidi bado hawajajumuishwa katika mpango huo.