beth
JF-Expert Member
- Aug 19, 2012
- 3,880
- 6,368
Mgombea wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Queen Cuthbert Sendiga ameendelea leo na Kampeni zake baada ya siku tatu za mapumziko ambazo alizitumia kufanya media tour jijini Dar es Salaam.
Akiwa katika Mkoa wa Pwani wilaya ya Kisarawe, aliweza kukutana na makundi mbalimbali na kuweza kunadi sera zake huku akitilia mkazo sera ya kilimo.
"Mkulima wa sasa bado anatumia jembe la mkono na anategemea kubadilisha maisha yake hili ni jambo la kutia huruma sana. Mkulima wa sasa anahitaji uhakika wa nyenzo bora za kulima, pembejeo za kisasa, uhakika wa kuuuza mazao yake akishakua amevuna, hii yote naenda kuitilia mkazo katika muda wangu wa kuwa madarakani endapo mtanipatia kura ya ndio tarehe 28 mwezi huu"
Mgombea ataendelea na Kampeni zake kesho Jumamosi katika wilaya ya Bagamoyo na kuendelea na kampeni zake kusini mwa nchi.
Akiwa katika Mkoa wa Pwani wilaya ya Kisarawe, aliweza kukutana na makundi mbalimbali na kuweza kunadi sera zake huku akitilia mkazo sera ya kilimo.
"Mkulima wa sasa bado anatumia jembe la mkono na anategemea kubadilisha maisha yake hili ni jambo la kutia huruma sana. Mkulima wa sasa anahitaji uhakika wa nyenzo bora za kulima, pembejeo za kisasa, uhakika wa kuuuza mazao yake akishakua amevuna, hii yote naenda kuitilia mkazo katika muda wangu wa kuwa madarakani endapo mtanipatia kura ya ndio tarehe 28 mwezi huu"
Mgombea ataendelea na Kampeni zake kesho Jumamosi katika wilaya ya Bagamoyo na kuendelea na kampeni zake kusini mwa nchi.