R.I.P SAID MRISHO ZICCO WA KILOSA

Konaball

JF-Expert Member
Joined
Mar 11, 2009
Posts
2,949
Reaction score
1,940
Habari nilizopata kuwa mchezaji wa zamani wa Yanga na Timu ya Taifa Said Mrisho (ZICCO WA KILOSA) Amefariki leo wakati akiletwa toka Morogoro kuja Muhimbili Hospital kwa ajiliya matibabu
 
Aaaaah! Mimi sijapata kumshuhudia katika kipindi cha uchezaji wake, ila nafahamu kidogo historia yake kacheza Tumbaku huyu, pamoja na magunia ya kilosa.
Atakumbukwa sana kwa mashuti yake makali.

Kacheza pia plsner ya ilala akiwa na kina Julio.

Poleni sana wazee wangu Charles Boniphace mkwasa pamoja na Jamhuri kiwelu julio.
 
Wewe ni MTU wa Mpira!
 
Daah nimekaa nae nyumba moja pale Shubira Morogoro, Asante kwa taarifa.
 
Miongoni mwa wachezaji walio pewa nickname na kuendana nazo kibongobongo ni huyu na juma amri maftah (pele wa mwanza )pleaner ya akina sisso hiyo
 
Wakati akimalizia soka lake alisaidia kuipandisha daraja Mtibwa sugar! Aliishi pale Manungu kwa muda mrefu na wenzie kina Alphonce Modest, Juma Buruhani, Reuben Mgaza......R.I.p Ziko wa Kilosa
 
R.I.P Zico wakilosa,poleni sana wafiwa wote,Hamidu mrisho,Mrisho jr na wengineo wote wapenda mpira
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…