Rafiki ni adui aliye karibu, chunga sana

Rafiki ni adui aliye karibu, chunga sana

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Joined
Mar 24, 2018
Posts
28,297
Reaction score
68,017
RAFIKI NI ADUI ALIYE KARIBU

Na, Robert Heriel

Rafiki ni mtu ambaye unaukaribu naye wa kimahusiano, unayeshirikiana naye katika mambo mengi, unayemuamini, unayetunziana naye siri na kusaidiana katika shida na raha.

Moja ya kanuni kuu ya ulimwengu. (Universal law) ni ''kutomuamini mtu yeyote'' (Trust no one) Kama alivyosema mwanafalsafa Niccolò Machiavelli mwenye asili ya kiitaliano katika Principle of management and Adminstration.

Machiavelli (tamka Makyeveli) katika falsafa za kisiasa(political philosophies) alitoa kanuni nyingi sana ambazo viongozi wengi wakubwa na mashuhuri duniani wamekuwa wakizitumia katika shughuli zao za utawala.

Miongoni mwa falsafa zake ni pamoja na hizi;

1. "Kamwe usimzidi kiongozi/boss wako" (1. Never Outshine the Master)
Yaani unapokuwa na kiongozi wako hakikisha hata kama unauwezo, ujuzi au elimu zaidi yako usionyeshe mbele yake usije ukapata sifa zaidi yake. Hii itakuweka sehemu mbaya.

2."Uliza/Jifanye kama Rafiki, Fanya kama Jasusi/mpelelezi" (Pose as a Friend, Work as a Spy)
Tafuta taarifa kwa mazungumzo ya kirafiki ili kujua dhamira au mipango ya watu, kuwa mpelelezi au jasusi, kwa kupata taarifa kwa huo ndio ulinzi wako.

3. Muangamize kabisa adui yako (Crush your Enemy Totally)
Unapopigana na adui yako usimpige nusu nusu mpige mpaka umuangamize kabisa. Usipofanya hivyo utasababisha Revenge isiyo na ulazima.

4. Jua ni nani unayeshughulika/ pambana naye, Usifanye kwa mtu asiyehusika (Know Who You’re Dealing with – Do Not Offend the Wrong Person) Hakikisha unayepambana naye ndiye adui halisi, usijepambana na mtu asiyehusika, kumbe adui yupo pembeni.

5. Usijitolee kwa ajili ya mtu yeyote (Do Not Commit to Anyone)
Dumisha uhuru wako, usijitolee kupambania wengine, bali wafanye wapambane wenyewe, hii itawafanya wakuone wewe ndiye mkombozi.

6. Kamwe usiwaamini sana Marafiki, Jifunze jinsi ya kutumia Maadui ( Never put too Much Trust in Friends, Learn how to use Enemies)

Jamani naomba niishie hapa kwa habari za huyu Niccolo Machiavele na falsafa zake, ingawaje zipo nyingi sana lakini lengo langu sio kuzielezea bali kutoa mifano michache, kisha nieleleze suala la kutokumuamini Mtu yeyote yule.

Watu wote waliofanikiwa katika utawala na wenye mafanikio makubwa duniani walifuata au walitumia baadhi ya kanuni hizo hapo juu.

Rafiki ni watu wazuri sana ikiwa tuu hutavunja kanuni ya msingi ya Trust no one(usimwamini yeyote). Rafiki anakuwa mbaya pale unapoanza kumuamini. Unapomuamini rafiki yako ndio unaanza kumfanya adui yako wa karibu.

Watu wote wanaolia kwa uchungu katika matatizo yao chanzo huwa ni marafiki au watu wao wa karibu. Ni kosa la kiufundi kumuamini mtu, kumpa siri zako hasa zile siri ambazo ni nguzo za maisha yako.

Huweza mpa rafiki yako siri ya mafanikio yako, hii ni kwa sababu 99% ya roho ya binadamu imejawa na ubinafsi na wivu. Kitendo cha kumwambia siri ya mafanikio yako ni kuamsha hisia za wivu juu yako, na huo ndio mwanzo wa kuanguka kwako.

Visa kama Samson na Deila hutufundisha hayo, kuwa Samson awali alikaza sana kutokumuamini Rafiki yake wa kimapenzi aitwaye Delilah. Lakini baada ya kushawishi sana yaani Delilah kutumia kanuni isemayo ""Uliza/Jifanye kama Rafiki, Fanya kama Jasusi/mpelelezi" ( Pose as a Friend, Work as a Spy)" Ambayo nimeitaja hapo juu, Samson akakubali kutoa siri akijua Delilah ni rafiki mwema kumbe ni adui aliyekaribu. Hakuna asiyejua kilichotokea.

Kisa cha Sadam Hussein hakuna asiyejua jinsi ilivyotokea mpaka akaja kukamatwa na kuuawa.
Kisa cha Yesu na Yuda Msaliti ambaye alikuwa rafiki yake.

Kwenye Ulimwengu huu, tahadhari ni muhimu sana kwa kila hatua unayopiga, kila hatua inaweza kuwa na mtego. Unapokanya ni lazima uhakikishe ni salama, wanaokuzunguka lazima uwatathimini, lazima uwajue kama kanuni isemayo "Jua ni nani unayeshughulika/ pambana naye, Usifanye kwa mtu asiyehusika ( Know Who You’re Dealing with – Do Not Offend the Wrong Person)"

Ukitaka kufanikiwa njia rahisi ni kujua kuwatumia maadui kuliko kuwatumia marafiki. Adui yupo real, Rafiki mara nyingi huwa wanafiki. Ni heri umuamini adui kwa maana unamjua.

Yesu wa Nazareth(Mwanafalsafa anayenikosa) aliwahi kusema adui wa mtu ni yule wa karibu. Na hata wahenga walisema kikulacho kinguoni mwako. Misemo hii ni king'ora kwetu kuwa lazima tuchukue tahadhari tuwapo na Rafiki zetu.

Rafiki wa kwanza ni Mke wako/ mume wako japo wengine wanaweza kukataa lakini huwezi kuwa na mwenzi ambaye sio rafiki yako hiyo ni ngumu. Usimuamini sana mke/mume wako mpaka utakapofikia kiwango cha juu na muda ukiwa umeyoyoma sana kiasi kwamba hata akifanya shambulizi lolote litakuwa halina madhara makubwa.

Marafiki wengine huweza kuwa wazazi, ndugu, jamaa na wengineo.

Muhimu kuzingatia. Usiwe na marafiki wengi kwani kwa kufanya hivyo hutaweza kuwa-manage hivyo unajitengenezea mazingira ya kuzungukwa na adui wengi.
Pili usimuamini yeyote yule.

Kama ukiambiwa utaje rafiki zako mpaka wafike kumi nakushauri fanya hivi
1. Mungu
2. wewe
3. wewe
4. wewe
5, 6, 7, 8, 9, 10 zote wewee.

Hiyo ni Universal Law kuivunja hiyo ni kujitafutia matatizo mwenyewe.

Mungu anasemaje kuhusiana na hili?
Mungu anasema; Usimwamini mtu yeyote zaidi yake. Imani huleta mategemeo. Na Mungu anasema; Ole wake amtegemeaye(amwaminiye) mwanadamu.

Kumuamini mtu ni kumtajarajia kwa mambo fulani. Matarajio ndio huumiza watu. Ulimuamini mtu hawezi kukusaliti sasa amaekusaliti, moyo unakuuma.

Hakuna amri inayotaka watu waaminiane hasa amri ya za Mungu. Bali ipo Amri moja tuu, Mpende jirani yako kama nafasi yako ilivyo.
Kosa kubwa linalofanywa na wengi ni kuchanganya Upendo na Imani ambapo kimsingi ni vitu viwili tofauti licha ya kuwa vinaweza kushirikiana.

Kutokumuamini mtu kutakufanya uishi kwa tahadhari, pia kutakufanya usiumie kipumbavu na kizembe.

Sheria hii ni muhimu kwenye kila nyanja ya maisha. hasa kwenye Utawala na mamlaka, Biashara, makazini, na ndani ya ndoa.

Kumbuka; Penye chuki wema Ulitangulia.

Kwa leo niishie hapa, maana wadau wangu hawaishi kulia makala ndefu.

Barikiweni!!!!

Ulikuwa nami;

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
0693322300
Kwa sasa Dodoma
 
Good,ukipata wasaa mwingine tushushie tena mambo kama haya ili tujengane vizuri mana siasa imetupumbaza tu..kazi nzuri ndugu

Shukrani mkuu.

Kama hutojali tembelea ukurasa wangu wa FB huko nashusha kila siku.

Hapa kuna baadhi nikipost mods hawaziruhusu.

Page inaitwa; Robert Heriel Tz
 
sSukrani mkuu.

Kama hutojali tembelea ukurasa wangu wa FB huko nashusha kila siku.

Hapa kuna baadhi nikipost mods hawaziruhusu.

Page inaitwa; Robert Heriel Tz
Nimekupata apo nitaingia uko mkuu nipate madini aisee
 
Andiko zurii...[emoji120][emoji120]
 
Upendo hauna kuaminiana.
Tupendane tu masuala ya kuaminiana ni kitu tofauti.
Ukichanganya kupendana na kuaminiana ndiyo unajikuta umetumbukia kwenye uadui.

Everyday is Saturday............................... 😎
 
Umeelezea vizuri kabisa hvo ulizoandika zinatoka kwenye kitabu Cha 48 laws of power by Robert Greene I wonder why umemtaja nicolo makyevel.

Coz yeye ndiye founder wa hizo law. huyo Robert Greene amezifafanua tuu kama mimi nilivyozifafanua. Ila msingi mkuu umetoka kwa mwanafalsafa huyo ambaye kidunia anaitwa the Father of Political Philosophy
 
Coz yeye ndiye founder wa hizo law. huyo Robert Greene amezifafanua tuu kama mimi nilivyozifafanua. Ila msingi mkuu umetoka kwa mwanafalsafa huyo ambaye kidunia anaitwa the Father of Political Philosophy
Mimi nilikisoma kwa huyo Robert Greene I didn't know kuwa founder ni huyo Nicollo, I wish ningepata kitabu chake
 
Mimi nilikisoma kwa huyo Robert Greene I didn't know kuwa founder ni huyo Nicollo, I wish ningepata kitabu chake


Huyo mwamba ni nyoko, huyo Niccolo ni wamoto, waweza tafuta habari zake hata mtandaoni. Kuhusu Bwana Robert Green yeye ni Modern Macheaville yaani ameboresha baadhi ya kanuni Mkuu.

Pia nimekisoma hicho kitabu cha Robert Greene Mkuu
 
Huyo mwamba ni nyoko, huyo Niccolo ni wamoto, waweza tafuta habari zake hata mtandaoni. Kuhusu Bwana Robert Green yeye ni Modern Macheaville yaani ameboresha baadhi ya kanuni Mkuu.

Pia nimekisoma hicho kitabu cha Robert Greene Mkuu
Yani ukisoma kitabu chake ingawa mifano ni ya zamani Ila Ina reflect current situation ya maisha yetu, ama kweli humu duniani hamna jipya tena watu wa zamani walikuwa smart Sana kuliko hicho kizazi chetu Cha yahoo. Com.
Huyo Nicollo lazima nimsome
 
Haya ni zaidi ya madini aisee..mada zako haziboi na zinafikirisha sana! Ahsante kwa makala zako.
 
RAFIKI NI ADUI ALIYE KARIBU

Na, Robert Heriel

Rafiki ni mtu ambaye unaukaribu naye wa kimahusiano, unayeshirikiana naye katika mambo mengi, unayemuamini, unayetunziana naye siri na kusaidiana katika shida na raha.

Moja ya kanuni kuu ya ulimwengu. (Universal law) ni ''kutomuamini mtu yeyote'' (Trust no one) Kama alivyosema mwanafalsafa Niccolò Machiavelli mwenye asili ya kiitaliano katika Principle of management and Adminstration.

Machiavelli (tamka Makyeveli) katika falsafa za kisiasa(political philosophies) alitoa kanuni nyingi sana ambazo viongozi wengi wakubwa na mashuhuri duniani wamekuwa wakizitumia katika shughuli zao za utawala.

Miongoni mwa falsafa zake ni pamoja na hizi;

1. "Kamwe usimzidi kiongozi/boss wako" (1. Never Outshine the Master)
Yaani unapokuwa na kiongozi wako hakikisha hata kama unauwezo, ujuzi au elimu zaidi yako usionyeshe mbele yake usije ukapata sifa zaidi yake. Hii itakuweka sehemu mbaya.

2."Uliza/Jifanye kama Rafiki, Fanya kama Jasusi/mpelelezi" (Pose as a Friend, Work as a Spy)
Tafuta taarifa kwa mazungumzo ya kirafiki ili kujua dhamira au mipango ya watu, kuwa mpelelezi au jasusi, kwa kupata taarifa kwa huo ndio ulinzi wako.

3. Muangamize kabisa adui yako (Crush your Enemy Totally)
Unapopigana na adui yako usimpige nusu nusu mpige mpaka umuangamize kabisa. Usipofanya hivyo utasababisha Revenge isiyo na ulazima.

4. Jua ni nani unayeshughulika/ pambana naye, Usifanye kwa mtu asiyehusika (Know Who You’re Dealing with – Do Not Offend the Wrong Person) Hakikisha unayepambana naye ndiye adui halisi, usijepambana na mtu asiyehusika, kumbe adui yupo pembeni.

5. Usijitolee kwa ajili ya mtu yeyote (Do Not Commit to Anyone)
Dumisha uhuru wako, usijitolee kupambania wengine, bali wafanye wapambane wenyewe, hii itawafanya wakuone wewe ndiye mkombozi.

6. Kamwe usiwaamini sana Marafiki, Jifunze jinsi ya kutumia Maadui ( Never put too Much Trust in Friends, Learn how to use Enemies)

Jamani naomba niishie hapa kwa habari za huyu Niccolo Machiavele na falsafa zake, ingawaje zipo nyingi sana lakini lengo langu sio kuzielezea bali kutoa mifano michache, kisha nieleleze suala la kutokumuamini Mtu yeyote yule.

Watu wote waliofanikiwa katika utawala na wenye mafanikio makubwa duniani walifuata au walitumia baadhi ya kanuni hizo hapo juu.

Rafiki ni watu wazuri sana ikiwa tuu hutavunja kanuni ya msingi ya Trust no one(usimwamini yeyote). Rafiki anakuwa mbaya pale unapoanza kumuamini. Unapomuamini rafiki yako ndio unaanza kumfanya adui yako wa karibu.

Watu wote wanaolia kwa uchungu katika matatizo yao chanzo huwa ni marafiki au watu wao wa karibu. Ni kosa la kiufundi kumuamini mtu, kumpa siri zako hasa zile siri ambazo ni nguzo za maisha yako.

Huweza mpa rafiki yako siri ya mafanikio yako, hii ni kwa sababu 99% ya roho ya binadamu imejawa na ubinafsi na wivu. Kitendo cha kumwambia siri ya mafanikio yako ni kuamsha hisia za wivu juu yako, na huo ndio mwanzo wa kuanguka kwako.

Visa kama Samson na Deila hutufundisha hayo, kuwa Samson awali alikaza sana kutokumuamini Rafiki yake wa kimapenzi aitwaye Delilah. Lakini baada ya kushawishi sana yaani Delilah kutumia kanuni isemayo ""Uliza/Jifanye kama Rafiki, Fanya kama Jasusi/mpelelezi" ( Pose as a Friend, Work as a Spy)" Ambayo nimeitaja hapo juu, Samson akakubali kutoa siri akijua Delilah ni rafiki mwema kumbe ni adui aliyekaribu. Hakuna asiyejua kilichotokea.

Kisa cha Sadam Hussein hakuna asiyejua jinsi ilivyotokea mpaka akaja kukamatwa na kuuawa.
Kisa cha Yesu na Yuda Msaliti ambaye alikuwa rafiki yake.

Kwenye Ulimwengu huu, tahadhari ni muhimu sana kwa kila hatua unayopiga, kila hatua inaweza kuwa na mtego. Unapokanya ni lazima uhakikishe ni salama, wanaokuzunguka lazima uwatathimini, lazima uwajue kama kanuni isemayo "Jua ni nani unayeshughulika/ pambana naye, Usifanye kwa mtu asiyehusika ( Know Who You’re Dealing with – Do Not Offend the Wrong Person)"

Ukitaka kufanikiwa njia rahisi ni kujua kuwatumia maadui kuliko kuwatumia marafiki. Adui yupo real, Rafiki mara nyingi huwa wanafiki. Ni heri umuamini adui kwa maana unamjua.

Yesu wa Nazareth(Mwanafalsafa anayenikosa) aliwahi kusema adui wa mtu ni yule wa karibu. Na hata wahenga walisema kikulacho kinguoni mwako. Misemo hii ni king'ora kwetu kuwa lazima tuchukue tahadhari tuwapo na Rafiki zetu.

Rafiki wa kwanza ni Mke wako/ mume wako japo wengine wanaweza kukataa lakini huwezi kuwa na mwenzi ambaye sio rafiki yako hiyo ni ngumu. Usimuamini sana mke/mume wako mpaka utakapofikia kiwango cha juu na muda ukiwa umeyoyoma sana kiasi kwamba hata akifanya shambulizi lolote litakuwa halina madhara makubwa.

Marafiki wengine huweza kuwa wazazi, ndugu, jamaa na wengineo.

Muhimu kuzingatia. Usiwe na marafiki wengi kwani kwa kufanya hivyo hutaweza kuwa-manage hivyo unajitengenezea mazingira ya kuzungukwa na adui wengi.
Pili usimuamini yeyote yule.

Kama ukiambiwa utaje rafiki zako mpaka wafike kumi nakushauri fanya hivi
1. Mungu
2. wewe
3. wewe
4. wewe
5, 6, 7, 8, 9, 10 zote wewee.

Hiyo ni Universal Law kuivunja hiyo ni kujitafutia matatizo mwenyewe.

Mungu anasemaje kuhusiana na hili?
Mungu anasema; Usimwamini mtu yeyote zaidi yake. Imani huleta mategemeo. Na Mungu anasema; Ole wake amtegemeaye(amwaminiye) mwanadamu.

Kumuamini mtu ni kumtajarajia kwa mambo fulani. Matarajio ndio huumiza watu. Ulimuamini mtu hawezi kukusaliti sasa amaekusaliti, moyo unakuuma.

Hakuna amri inayotaka watu waaminiane hasa amri ya za Mungu. Bali ipo Amri moja tuu, Mpende jirani yako kama nafasi yako ilivyo.
Kosa kubwa linalofanywa na wengi ni kuchanganya Upendo na Imani ambapo kimsingi ni vitu viwili tofauti licha ya kuwa vinaweza kushirikiana.

Kutokumuamini mtu kutakufanya uishi kwa tahadhari, pia kutakufanya usiumie kipumbavu na kizembe.

Sheria hii ni muhimu kwenye kila nyanja ya maisha. hasa kwenye Utawala na mamlaka, Biashara, makazini, na ndani ya ndoa.

Kumbuka; Penye chuki wema Ulitangulia.

Kwa leo niishie hapa, maana wadau wangu hawaishi kulia makala ndefu.

Barikiweni!!!!

Ulikuwa nami;

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
0693322300
Kwa sasa Dodoma
picha
 
RAFIKI NI ADUI ALIYE KARIBU

Na, Robert Heriel

Rafiki ni mtu ambaye unaukaribu naye wa kimahusiano, unayeshirikiana naye katika mambo mengi, unayemuamini, unayetunziana naye siri na kusaidiana katika shida na raha.

Moja ya kanuni kuu ya ulimwengu. (Universal law) ni ''kutomuamini mtu yeyote'' (Trust no one) Kama alivyosema mwanafalsafa Niccolò Machiavelli mwenye asili ya kiitaliano katika Principle of management and Adminstration.

Machiavelli (tamka Makyeveli) katika falsafa za kisiasa(political philosophies) alitoa kanuni nyingi sana ambazo viongozi wengi wakubwa na mashuhuri duniani wamekuwa wakizitumia katika shughuli zao za utawala.

Miongoni mwa falsafa zake ni pamoja na hizi;

1. "Kamwe usimzidi kiongozi/boss wako" (1. Never Outshine the Master)
Yaani unapokuwa na kiongozi wako hakikisha hata kama unauwezo, ujuzi au elimu zaidi yako usionyeshe mbele yake usije ukapata sifa zaidi yake. Hii itakuweka sehemu mbaya.

2."Uliza/Jifanye kama Rafiki, Fanya kama Jasusi/mpelelezi" (Pose as a Friend, Work as a Spy)
Tafuta taarifa kwa mazungumzo ya kirafiki ili kujua dhamira au mipango ya watu, kuwa mpelelezi au jasusi, kwa kupata taarifa kwa huo ndio ulinzi wako.

3. Muangamize kabisa adui yako (Crush your Enemy Totally)
Unapopigana na adui yako usimpige nusu nusu mpige mpaka umuangamize kabisa. Usipofanya hivyo utasababisha Revenge isiyo na ulazima.

4. Jua ni nani unayeshughulika/ pambana naye, Usifanye kwa mtu asiyehusika (Know Who You’re Dealing with – Do Not Offend the Wrong Person) Hakikisha unayepambana naye ndiye adui halisi, usijepambana na mtu asiyehusika, kumbe adui yupo pembeni.

5. Usijitolee kwa ajili ya mtu yeyote (Do Not Commit to Anyone)
Dumisha uhuru wako, usijitolee kupambania wengine, bali wafanye wapambane wenyewe, hii itawafanya wakuone wewe ndiye mkombozi.

6. Kamwe usiwaamini sana Marafiki, Jifunze jinsi ya kutumia Maadui ( Never put too Much Trust in Friends, Learn how to use Enemies)

Jamani naomba niishie hapa kwa habari za huyu Niccolo Machiavele na falsafa zake, ingawaje zipo nyingi sana lakini lengo langu sio kuzielezea bali kutoa mifano michache, kisha nieleleze suala la kutokumuamini Mtu yeyote yule.

Watu wote waliofanikiwa katika utawala na wenye mafanikio makubwa duniani walifuata au walitumia baadhi ya kanuni hizo hapo juu.

Rafiki ni watu wazuri sana ikiwa tuu hutavunja kanuni ya msingi ya Trust no one(usimwamini yeyote). Rafiki anakuwa mbaya pale unapoanza kumuamini. Unapomuamini rafiki yako ndio unaanza kumfanya adui yako wa karibu.

Watu wote wanaolia kwa uchungu katika matatizo yao chanzo huwa ni marafiki au watu wao wa karibu. Ni kosa la kiufundi kumuamini mtu, kumpa siri zako hasa zile siri ambazo ni nguzo za maisha yako.

Huweza mpa rafiki yako siri ya mafanikio yako, hii ni kwa sababu 99% ya roho ya binadamu imejawa na ubinafsi na wivu. Kitendo cha kumwambia siri ya mafanikio yako ni kuamsha hisia za wivu juu yako, na huo ndio mwanzo wa kuanguka kwako.

Visa kama Samson na Deila hutufundisha hayo, kuwa Samson awali alikaza sana kutokumuamini Rafiki yake wa kimapenzi aitwaye Delilah. Lakini baada ya kushawishi sana yaani Delilah kutumia kanuni isemayo ""Uliza/Jifanye kama Rafiki, Fanya kama Jasusi/mpelelezi" ( Pose as a Friend, Work as a Spy)" Ambayo nimeitaja hapo juu, Samson akakubali kutoa siri akijua Delilah ni rafiki mwema kumbe ni adui aliyekaribu. Hakuna asiyejua kilichotokea.

Kisa cha Sadam Hussein hakuna asiyejua jinsi ilivyotokea mpaka akaja kukamatwa na kuuawa.
Kisa cha Yesu na Yuda Msaliti ambaye alikuwa rafiki yake.

Kwenye Ulimwengu huu, tahadhari ni muhimu sana kwa kila hatua unayopiga, kila hatua inaweza kuwa na mtego. Unapokanya ni lazima uhakikishe ni salama, wanaokuzunguka lazima uwatathimini, lazima uwajue kama kanuni isemayo "Jua ni nani unayeshughulika/ pambana naye, Usifanye kwa mtu asiyehusika ( Know Who You’re Dealing with – Do Not Offend the Wrong Person)"

Ukitaka kufanikiwa njia rahisi ni kujua kuwatumia maadui kuliko kuwatumia marafiki. Adui yupo real, Rafiki mara nyingi huwa wanafiki. Ni heri umuamini adui kwa maana unamjua.

Yesu wa Nazareth(Mwanafalsafa anayenikosa) aliwahi kusema adui wa mtu ni yule wa karibu. Na hata wahenga walisema kikulacho kinguoni mwako. Misemo hii ni king'ora kwetu kuwa lazima tuchukue tahadhari tuwapo na Rafiki zetu.

Rafiki wa kwanza ni Mke wako/ mume wako japo wengine wanaweza kukataa lakini huwezi kuwa na mwenzi ambaye sio rafiki yako hiyo ni ngumu. Usimuamini sana mke/mume wako mpaka utakapofikia kiwango cha juu na muda ukiwa umeyoyoma sana kiasi kwamba hata akifanya shambulizi lolote litakuwa halina madhara makubwa.

Marafiki wengine huweza kuwa wazazi, ndugu, jamaa na wengineo.

Muhimu kuzingatia. Usiwe na marafiki wengi kwani kwa kufanya hivyo hutaweza kuwa-manage hivyo unajitengenezea mazingira ya kuzungukwa na adui wengi.
Pili usimuamini yeyote yule.

Kama ukiambiwa utaje rafiki zako mpaka wafike kumi nakushauri fanya hivi
1. Mungu
2. wewe
3. wewe
4. wewe
5, 6, 7, 8, 9, 10 zote wewee.

Hiyo ni Universal Law kuivunja hiyo ni kujitafutia matatizo mwenyewe.

Mungu anasemaje kuhusiana na hili?
Mungu anasema; Usimwamini mtu yeyote zaidi yake. Imani huleta mategemeo. Na Mungu anasema; Ole wake amtegemeaye(amwaminiye) mwanadamu.

Kumuamini mtu ni kumtajarajia kwa mambo fulani. Matarajio ndio huumiza watu. Ulimuamini mtu hawezi kukusaliti sasa amaekusaliti, moyo unakuuma.

Hakuna amri inayotaka watu waaminiane hasa amri ya za Mungu. Bali ipo Amri moja tuu, Mpende jirani yako kama nafasi yako ilivyo.
Kosa kubwa linalofanywa na wengi ni kuchanganya Upendo na Imani ambapo kimsingi ni vitu viwili tofauti licha ya kuwa vinaweza kushirikiana.

Kutokumuamini mtu kutakufanya uishi kwa tahadhari, pia kutakufanya usiumie kipumbavu na kizembe.

Sheria hii ni muhimu kwenye kila nyanja ya maisha. hasa kwenye Utawala na mamlaka, Biashara, makazini, na ndani ya ndoa.

Kumbuka; Penye chuki wema Ulitangulia.

Kwa leo niishie hapa, maana wadau wangu hawaishi kulia makala ndefu.

Barikiweni!!!!

Ulikuwa nami;

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
0693322300
Kwa sasa Dodoma
Namba tatu inanifundisha kwanini lisu alipigwa 16 bullets na bwana yule mtu yule.
 
Back
Top Bottom