Hehehe!!! Sijaelewa umenitag niseme nini, watashindana sana hawa na ndio utamu wa nchi inayoongozwaa kwa misingi ya kidemokrasia, wananchi wanakua huru kuchagua kiongozi wao. Sio kama kwenu huko kundi la watu hukutana Dodoma CCM na kuamua nani awe rais...hehehe
Anyway, huyu Raila apambane tu ila sikupendezwa na tamko lake juzi aliposema yeye ndiye alikua mshauri wa Magufuli, ina maana ujuha wote huo wa mwenda zake huko kwenu ulitokana na ushauri wa Raila. Akitumia kete ya Magufuli atapata uungwaaji mkono na Wakenya wengi maana wengi walizoea kusoma kumhusu Magufuli kwenye vyombo vya habari namna alikua anatajwa kama mtetezi wa wanyonge, ila kwa wachache tuliokua tunajua uhalsia wa hali ya Tanzania tunaona kama itakua msiba kwa taifa letu.
Pona yetu tuna katiba nzuri na bora kuzidi zote ukanda wote huu, maana isingekua kwa katiba hii, hata huyu rais wa sasa Uhuru Kenyatta nimemuona angekua dikteta balaa sana, sema amekua akitulizwa kila akiota mapembe, alijaribu teuzi za kimabavu mabavu zikabatilishwa zote, hivyo hata Raila au Ruto au yeyote atakayeukwaa, hatatuzingua maana tunalindwa na katiba, kwenu huko ndio hatari sana na Nyerere aliwahi kulisema hilo, kwamba siku mtapata rais wa hovyoo chini ya hiyo katiba mtamkoma.
Mgombea urais wa Kenya anayeungwa mkono na wananchi wengi nchini humo mh Raila Odinga amesema yeye alikuwa ni Mshauri wa aliyekuwa Rais wa Tanzania hayati Magufuli. Raila amesema Magufuli aliweza kumpigia simu hata saa 12 asubuhi ili apate ushauri wake na kwamba alimshauri hata namna ya kupata...
Raila anasema hayo kwa sababu ametathmini nafasi ya Tz kimataifa na kikanda na kugundua kwamba Magufuli ameiweka kwenye nafasi adhimu na nadra kwa nchi nyingi za Afrika kwa muda mfupi kiasi hicho (mnyonge mnyongeni haki yake mpeni na hakuna aliye mbaya kwa 100%).
Wakenya wengi wanachagiza serikali yao kujilinganisha na Tz ya Magufuli. Kwakuwa hiyo ndiyo mindset ya Wakenya walio wengi (ukiachilia Wakalenjini ambao ni Kipsigis, Nandi, Keiyo, Marakwet, Sabaot, Pokots, Tugen, Terik, Sengwer, Lembus, na Ogiek ambao wote ni 6,358,113 katika idadi ya watu wote wa Kenya wapatao 47,564,296 (2019)). Hivyo alichosema Raila kinathibitisha tu kwamba maji hufuata mkondo (anasema wanachotaka watu kusikia siyo anachotaka yeye watu wasikie). Raila ni strategist ambaye alianza siasa Magufuli akiwa hajazaliwa (Mzee Oginga Odinga alijenga mazoea ya kusafiri na Raila na Oburu kwenye ziara za kitaifa na kimataifa wakingali wako darasa la tatu, Magufuli alikuwa hajazaliwa).
Kama Raila ndiyo alimshauri Magufuli namna ya kupaisha nchi kwa muda mfupi kama walivyofanya Joseph Stalin, Abeid Karume na William Tubman basi ni wazi kwamba maendeleo ya Tz ya Magufuli yameatamiwa na Raila na kwamba alifanya hivyo kama sample population/case study ya kuwaonyesha Wakenya na dunia kwamba anatosha kuwa Rais wa Kenya 2022 (baada ya kukosa fursa ya kufanya hivyo ndani ya Kenya). Ni kama Tz ili-import mawazo ya Raila na kufanikiwa kufanya mambo mengi kwa muda mfupi yaliyoifanya Tz kuwa/kuendeleza mambo mengi yakiwemo:
1. Viwanja vya ndege vya kimataifa 5 (JNIA, Songwe, Znz, Mwz, KIA (ameviboresha JPM))
2. Viwanja vya ndege vya kikanda (Mtw, Chato, Arusha, Bkb, Kgm, Tbr, Msm, Pmb, Ddm (ameviboresha JPM))
3. Kukarabati na kupanua na kunuia kupandisha hadhi toka kuwa viwanja vya ndege vya kikanda hadi vya kimataifa (Mtw, Ddm, Chato,).
4. Ununuzi wa ndege mpya 12.
5. Ununuzi wa rada mpya 3 za kuona anga ya nchi kwa asilimia 98%, zamani zilizokuwepo (za Mramba) ziliona anga kwa chini ya 50%. Hivi sasa Rwanda na Burundi zinategemea rada za Tz kwa ndege za kiraia zinazotua na kuruka Bujumbura na Kigali.
6. Upanuzi wa bandari zote kuu.
7. Ujenzi wa SGR na ukarabati na upanuzi wa MGR.
8. Nchi yote inafikika kwa reli, meli, barabara na ndege.
9. Ujenzi wa Meli katika maziwa yote makuu.
10. Tz ndiyo kinara katika EAC na GLR kwa miundombinu ya usafirishaji ambayo ndiyo kiungo kikubwa cha uchumi wowote duniani.
11. Ukarabati na upanuzi wa hospitali kufikia hadhi ya kimataifa; za MNH, MOI, JKCI, BMC, Benjamin Mkapa, KCMC. Ocean Road (ambayo inapokea kesi za saratani Afrika ya Mashariki, Kati na SADC).
12. Ujenzi wa hospitali 7 za kikanda zikiwemo za Mtwara na Musoma. Hivi sasa hospitali ya Musoma Kwanga, inatoa huduma za mifupa kwa kiwango cha kupokea rufaa toka hospitali ya kimataifa ya Bugando.
13. Hospitali mpya za Wilaya zaidi ya 67, vituo vya afya vipya vya kufanya upasuaji pia 44.
14. Miradi ya maji safi na salama zaidi ya 1200.
15. Barabara mpya za lami za 3500 km sawa na umbali wa toka Dsm hadi Misri Aswan Airport (ukichanganya na za awamu zilizopita za Nyerere na Mwinyi zinafika 11,000 km sawa na umbali wa kutoka Dsm hadi Washington DC ambayo ni 12,780 km kama tutakamilisha miradi michache inayoendelea)
16. Bwawa la umeme, Raila labda aliona ni salama na nafuu kununua umeme toka Tz.
17. Elimu bure, hivi leo wanaoingia kidato cha kwanza ambao ndiyo product ya kwanza ya elimu bure kwa shule za msingi ni double 1ml ndiyo maana madarasa yanajengwa kwa kasi kubwa kabla ya 15 Januari, tumeweza kuwafikia Kenya ambao wamedahili 1,088,456 kuingia kidato cha kwanza.
18. Uuuzaji wa bidhaa-lugha ya Kiswahili. Kuna order kubwa duniani ya Walimu wa Kiswahili ambao Tz pekee haiwezi kukidhi kiu hiyo ya dunia, itabidi Kenya na DR Congo watusaidie, bado kuna changamoto za kiuhamiaji zilizotokana na Uviko 19.
19. Utokomezaji njaa, Kenya njaa ni tatizo kubwa la kisera (hasa sera ya kilimo cha umwagiliaji kwa sababu nusu ya Kenya ni semi-arid), Kusini Kenya inategemea mlima Kilimanjaro iyeyushe barafu ndipo maji yatiririke kwenda kwenye vijito vyao Kajiado County hadi Ngong.
20. Vita ya wakulima na wafugaji vya miaka 25 vimetokomezwa na Magufuli, Kenya hadi leo jamii za wafugaji Samburu (The Butterfly People), Somalis, Pokot, Turkana, Maasai, Wakurya, Meru, bado wanauana hadi leo tangu enzi za Jomo Kenyatta.
21. Vyuo Vikuu 26 (10 umma na 16 binafsi) siyo haba maana tunaikaba koo Kenya ambayo ina vyuo vikuu 30 umma, 30 chartered private universities.
22. Hifadhi za wanyama 22.
23. Shule mpya za sekondari 228 (za Jafo), SSH anajenga shule mpya za sekondari 1000.
24. Kuingia Uchumi wa Pato la Kati la Chini.
Whatnot?
NB. Kama Raila ndiyo alikuwa Mshauri wa Magufuli hadi kujenga, kuboresha na kuendeleza haya basi nafikiri SSH akae miguuni pake Raila.
Rutto alikua anafikiria Kama wewe kuhusu Magufuli ndio sababu inaonekana atapoteza katika uchaguzi ujao, yeye alijenga chuki na wivu kwa Tanzania na Magufuli bila kujua kwamba Tanzania na Magufuli ndio kiongozi na mfano wa kuigwa hapa Africa tangu enzi za Nyerere.
Ukitaka kufanikiwa kuchaguliwa kuwa kiongozi wa nchi za SADC na EA lazima utaje kwamba utafuata nyayo za viongozi wa Tanzania, ndicho alichokifanya Raila Jambo ambalo limegeuza mwenendo na muelekeo wa kampeni za Kenya na kuonekana wazi kwamba Raila atashinda licha ya kwamba miezi michache nyuma Rutto alionekana "unstoppable".
Ukweli ndio huo kwamba Tanzania ni mfano Bora na no chuo cha uongozi toka enzi za Nyerere, atakayejaribu kushindana au kuichukia Tanzania basi ajiandae kushindwa katika uchaguzi, ninamsikitikia Sana Rutto kwa kushindwa kulijua hilo mapema, nilipenda awe rais wa Kenya, lakini kiburi chake cha kutotaka kutambua nguvu ya Tanzania/Magufuli kutasababisha kushindwa uchaguzi.
Siasa na sera za kimataifa za Nyerere zilijengwa kwenye msingi na imani moja isiyobatilika kwamba ili Tz iwe salama lazima ihakikishe majirani zake wote 8 wanaoizunguka wanaongozwa na viongozi ambao pia Tz imewaithibati (accreditation), ndiyo maana Uganda na Shelisheli Tz iliwapiga Idi Amin na Kaburu kwa mfuatano/respectively na kupandikiza viongozi na hakuna Jumuiya ya Kimataifa ilithubutu kukohoa.
Safu ya viongozi wote wa Tz wamelinda tunu hiyo adhimu duniani ambayo US imeiiiga toka Tz. US nayo inapiga huko duniani na kupandikiza inayemtaka. Mgombea yeyote wa nchi jirani yoyote asiyetaka kuambatana na Tz atabaki kuwa mshindi/rais wa magazetini tu milele.
Joshua Nkomo akihutubia kikao cha Kamati ya Ulinzi na Usalama cha ZAPU (siyo ZANU PF) alisema "kama angealikwa kwenye mkutano wa Berlin wa kuligawa bara la Afrika basi angemwomba Otto von Bismarck kuwa Southern Rhodesia (baadaye Zimbabwe) ipakane na Tanganyika"