Rais akidanganya naye awajiwajibishwe na bunge

Rais akidanganya naye awajiwajibishwe na bunge

mwananthropolojia

JF-Expert Member
Joined
Oct 6, 2012
Posts
956
Reaction score
657
tumekuwa tukiona jinsi ,wabunge wetu wanavyojaribu kuwawajibisha mawaziri wetu wanaosema uongo katika bunge,na hii imesaidia sana kuleta uwajibikaji kwa kiasi fulani ingawa tumekuwa tukiona wakikingiwa vifua na maspika wetu wababe,ila sijawahi kusikia raisi akidanganya kama naye bunge letu linaweza kumwajibisha, kwani katika katika mfumo wetu wa check and balance ,bunge linakua linaitazama serikali isfanye uozo na kuwajibika kweli kwa wananchi waliowachagua kuwatawala.

swali nililonalo ni je raisi ambaye ndiye mkuu wa serikali akidanganya umma anaweza kuwajibishwa?ingawa mkuu wa shughuli za serikali bungeni ni waziri mkuu, raisi anawajibika kwa nani? na kama hawajibiki kokote napendekeza kwenye katiba ijayo naye ajumuishwe akisema uongo kwa wananchi hata kama ni majukwaani ili mradi alikuwa kwenye shughuli za uraisi basi kupitia kwa wawakilishi waliochaguliwa na wananchi ambalo ni bunge nao wamwajibishe.
na maspika kazi zao ziwe kusimamia bunge na sio nao kushiriki katika majadiliano na ubishani ndani ya bunge
 
... Mkuu kama ikipita hii ya kuwawajibisha marais, itasaidia sana, kwani Marais wetu ndiyo wanaongoza kwa kusema uongo. "kwenye vitabu vitakatifu wanajulika kwa jina la WAKRETE"
 
Katiba inaruhusu RAIS kuwajibishwa na bunge...sema mfumo wa serikali ya chama cha JEMBE na NYUNDO hauruhusu hiyo kitu.......
 
tatizo raisi anakuwa anafanyia shughuli zake zote za serikalini nje ya bunge na anakuwa na nafasi kubwa ya kudanganya wananchi,hii katiba mpya inatakiwa iangalie matamko yote yanayotolewa na raisi akiwa kwenye shughuli zake za uraisi,zipimwe na kama amesema uongo suala lipelekwe bungeni na ajieleze,ila kwa sasa ni ngumu kwani inaonekana kama hawajibiki kwa bunge bali bunge ndio linawajibika kwake ,this is too much power
 
Back
Top Bottom