Pre GE2025 Rais anafanya makosa makubwa sana kuwapigia debe baadhi ya viongozi wa CCM kwamba "nirudishieni huyu" mwaka 2025

Pre GE2025 Rais anafanya makosa makubwa sana kuwapigia debe baadhi ya viongozi wa CCM kwamba "nirudishieni huyu" mwaka 2025

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Synthesizer

Platinum Member
Joined
Feb 15, 2010
Posts
12,699
Reaction score
22,598
Hapa juzi nimeona taarifa Rais Samia akiwaambia wananchi wa Kilosa wamrudishie Prof. Kabudi katika uchaguzi wa 2025. Nimejiuliza sana bila kupata jibu, kama Rais Samia haoni ni kosa kubwa sana kwake, kuwaambia wananchi nirudishieni Prof Kabudi, au kiongozi yeyote wa CCM, mwaka 2025?

Rais Samia anaposema nirudishieni kiongozi fulani aliyepo madarakani mwaka 2025, haya yanajitokeza;
  • Haheshimu utashi wa wananchi kwamba wanaweza wakawa hawamtaki kiongozi aliyepo, hata kama ni waziri
  • Anawaambia watu wengine watakaotaka kutia nia kuwania nafasi hizo za CCM kwamba nafasi hizo tayari zina wenyewe
  • Haheshimu utaratibu CCM iliyojiwekea wa kuwapata viongozi kwa kuanza na kura za maoni na anaona yeye ndie anaepaswa kuwaambia nani anataka awe kiongozi au wamrudishe
  • Tayari amejihakikishia kwamba yeye ndio Rais ajae 2025 japo uchaguzi bado
Kama kuna mtu Rais Samia anampenda na angependa akiona akirudishwa kwenye nafasi yake 2025, basi asubiri huyo mtu apitishwe ngazi zote za kura za maoni na kuteuliwa kushindana na mtu wa chama cha upinzani ndio anaweza kuwaambia wananchi nirudishieni fulani mwaka 2025. Kauli kama hizo zinapotolewa mapema kiasi hiki zinakuwa hazina tofauti na kauli ya Nape ambayo huenda imemuondoa kwenye uwaziri.

Reherence: Samia ampigia chapuo Profesa Kabudi kiaina
 
Hapa juzi nimeona taarifa Raisi Samia akiwaambia wananchi wa Kilosa wamrudishie Prof. Kabudi katika uchaguzi wa 2025. Nimejiuiza sana bila kupata jibu, kama Raisi Samia haoni ni kosa kubwa sana kwake, kuwaambia wananchi nirudishieni Prof Kabudi, au kiongozi yeyote wa CCM, mwaka 2025...
Ambacho ungelalamikia chenye uzito ni kufanya campaign kabla ya muda wake, hayo mengine ni haki yake kusema.
 
Ambacho ungelalamikia chenye uzito ni kufanya campaign kabla ya muda wake, hayo mengine ni haki yake kusema.
Hilo ni jambo tofauti kabisa na hili. Sasa unafikiri mimi ninaetaka kugombea ubunge wa Kilosa kwa tiketi ya CCM najisikiaje Samia anapowaambia watu wa Kilosa "endeleeni kuniletea Kabudi"? Unaona Samia ananitendea haki, au ameona sisi wengine hutufai kwa sababu sio ma professor kama Kabudi? Kwa nini asisubiri wananchi waamue?
 
Kiongozi mpenda maendeleo anapenda kufanya kazi na wapenda maendeleo wenzake. Alichofanya Rais ni kuwakumbusha wananchi Fulani ni mchapakazi na mpenda maendeleo kama yeye hivyo mkimchagua mtakuwa mmemsaidia kuwaleteeni maendeleo kwa haraka
 
Hapa juzi nimeona taarifa Raisi Samia akiwaambia wananchi wa Kilosa wamrudishie Prof. Kabudi katika uchaguzi wa 2025. Nimejiuiza sana bila kupata jibu, kama Raisi Samia haoni ni kosa kubwa sana kwake, kuwaambia wananchi nirudishieni Prof Kabudi, au kiongozi yeyote wa CCM, mwaka 2025...
Kinachoni sikitisha ni kwamba system yetu haihitaji kura yako wew ili ishike dola rejea kaulihizi mara nyingi hutolewa na Rais aliyepo madarakani tunaposema katiba mpya ni muhimu nataka muelewe ili tuondokane na kumfanya mtu moja awe mwamuzi wa mambo yote
 
Kiongozi mpenda maendeleo anapenda kufanya kazi na wapenda maendeleo wenzake. Alichofanya Rais ni kuwakumbusha wananchi Fulani ni mchapakazi na mpenda maendeleo kama yeye hivyo mkimchagua mtakuwa mmemsaidia kuwaleteeni maendeleo kwa haraka
Tunachosema hapa ni kwamba Raisi anafanya makosa, bila kujali anamsema mtu mwingine mpenda maendeleo. Huwezi kukiuka taratibu zilizowekwa kwa sababu kama unazotaja hapa, hizi watu mmesoma shule gani? Kwamba hizo nafasi ziliumbwa kwa ajili ya watu fulani wengine wote hawafai?
 
Mgombea Jenga hoja wananchi wakuone wewe ndio msaada katika kuwakifisha kwenye maendeleo Sasa unataka upande wa pili wakupambe na kukusifia "UBAYA UBWELA".Mama mitano tena
 
nadhani ni muhimu kuelewa kwamba nchi hii inaongozwa na serilikali sikivu ya CCM ambacho ndiyo chama Tawala...

ni vema zaidi ikaeleweka bayana kwamba yanayotekelezwa hivi sasa ndani ya chama na serilikali sikivu ya CCM ni matakwa ya wanainchi na waTanzania kwa ujumla kupitia ilani ya uchaguzi ya CCM 🐒

wale wanaopaswa kusubiri kuhubiri sera na mipango yao ni vyama vya siasa visivyo na dollar, ila sio CCM.

CCM iko kazini kwa mujibu wa sheria za chama, katiba ya nchi na ridhaa ya wanainchi na,

kwahivyo,
hayupo Kiongozi wa chama au serikali anaekiuka taratibu za chama au katiba ya nchi, bali ni uwajibikaji wa wazi kwa maslahi mapana ya waTanzania wote 🐒

so,
upotoshaji sio jambo zuri hata kidogo katika mambo haya bayana 🐒
Sasa kula za maoni za kazi gani?
 
Back
Top Bottom