Rais Biden akutana na mawaziri waandamizi wa Ukraine

Rais Biden akutana na mawaziri waandamizi wa Ukraine

BigTall

JF-Expert Member
Joined
Mar 9, 2022
Posts
525
Reaction score
1,257
61268234_303.jpg

Rais Joe Biden wa Marekani amekutana na mawaziri wawili wa Ukraine nchini Poland kuonyesha uungaji mkono wa Washington kwa serikali mjini Kyiv wakati Urusi ikiashiria kwamba inaweza kupunguza malengo yake ya kivita nchini Ukraine.

Biden aliketi kwenye meza ndefu nyeupe pamoja na mawaziri wake wa mambo ya nje Antony Blinken na yule wa ulinzi Lloyd Austin na upande wa pili alikuwepo waziri wa mambo ya kigeni wa Ukraine Dmytro Kuleba na waziri wa ulinzi wa nchi hiyo Oleksii Reznikov.

Kulingana na Wizara ya Mambo ya Kigeni ya Marekani, mkutano huo kati ya Biden na mawaziri wa mambo ya nchi za nje na ulinzi wa Ukraine ulijikita kwenye kusisitiza dhamira ya Marekani katika kutetea uhuru na hadhi ya mipaka ya Ukraine.

Mazungumzo hayo yamefanyika wakati Urusi imeendelea kufanya mashambulizi kwenye mji wa bandari wa Mariupol kwa kuyalenga makazi ya watu na vituo vya kijeshi kutokea angani na ardhini.

Katika hatua nyingine iliarifiwa jana kuwa vikosi vya Urusi vimechukua udhibiti wa Mji wa Slavutych ambao ni makazi ya wafanyakazi wa kinu cha nyuklia cha Chernobyl.

Putin alituma vikosi vyake nchini Ukraine tangu Februari 24, akiahidi kulisambaratisha jeshi la nchi hiyo na kuuangusha utawala unaoegemea upande wa magharibi wa rais Volodymyr Zelensky.

Source: DW
 
... loud and clear! Kuna uzi humu fashisti ameanza kuondoa vikosi wakiwa wamekufa wa kutosha.
 
Jamaa wapo kama makolo, raia wenu wanakufa, nyie mnafurahia kupiga picha na rais wa US. Sikuwahi kufikiri kuna wazungu 'vilaza '. US angekua ana nia angeingia mzigoni kuzichapa, anaogopa eti vita ya nyukilia.. ina maana raia wa Ukraine ndio wa kufa?
 
View attachment 2165550
Rais Joe Biden wa Marekani amekutana na mawaziri wawili wa Ukraine nchini Poland kuonyesha uungaji mkono wa Washington kwa serikali mjini Kyiv wakati Urusi ikiashiria kwamba inaweza kupunguza malengo yake ya kivita nchini Ukraine.

Biden aliketi kwenye meza ndefu nyeupe pamoja na mawaziri wake wa mambo ya nje Antony Blinken na yule wa ulinzi Lloyd Austin na upande wa pili alikuwepo waziri wa mambo ya kigeni wa Ukraine Dmytro Kuleba na waziri wa ulinzi wa nchi hiyo Oleksii Reznikov.

Kulingana na Wizara ya Mambo ya Kigeni ya Marekani, mkutano huo kati ya Biden na mawaziri wa mambo ya nchi za nje na ulinzi wa Ukraine ulijikita kwenye kusisitiza dhamira ya Marekani katika kutetea uhuru na hadhi ya mipaka ya Ukraine.

Mazungumzo hayo yamefanyika wakati Urusi imeendelea kufanya mashambulizi kwenye mji wa bandari wa Mariupol kwa kuyalenga makazi ya watu na vituo vya kijeshi kutokea angani na ardhini.

Katika hatua nyingine iliarifiwa jana kuwa vikosi vya Urusi vimechukua udhibiti wa Mji wa Slavutych ambao ni makazi ya wafanyakazi wa kinu cha nyuklia cha Chernobyl.

Putin alituma vikosi vyake nchini Ukraine tangu Februari 24, akiahidi kulisambaratisha jeshi la nchi hiyo na kuuangusha utawala unaoegemea upande wa magharibi wa rais Volodymyr Zelensky.

Source: DW

Raia wao wanakufa wenyewe wako bize kupiga picha [emoji16]
 
Ukraine wakitumia hiyo nafasi vizuri na kushirikiana na watu wenye nguvu zaidi wanaweza kujiongezea eneo na kuwakomboa hata raia wa urusi wanaoteseka kwaajili ya mjinga putin.
 
Mwanaume kaanzia Lyiv halafu wanakutana katikati hapo kati inapachikwa bendera ya Russia hapo Ukraine itatambulika kama Republic of Russia in Ukraine(RRU)
 
Ukraine wanabeba garama kubwa Ila US na washirika wametumia njia ya busara, kuonyesha maonyesho makubwa utayari Vita, pia uugwaji Mkono Ukraine japo kwa silaha ndogo indirectly. Putin limekuwa zio lake binafsi Hana uungwaji Mkono wa majority nyumbani na duniani.
Mwisho Putin umefika, dunia ya maamuzi ya MTU mmbabe anamiliki nuklia Ni hatari.
Nguvu za kijasusi zinaelekezwa pia Korea Kaskazini kulikomboa taifa lile mapema.
 
Ukraine wanabeba garama kubwa Ila US na washirika wametumia njia ya busara, kuonyesha maonyesho makubwa utayari Vita, pia uugwaji Mkono Ukraine japo kwa silaha ndogo indirectly. Putin limekuwa zio lake binafsi Hana uungwaji Mkono wa majority nyumbani na duniani.
Mwisho Putin umefika, dunia ya maamuzi ya MTU mmbabe anamiliki nuklia Ni hatari.
Nguvu za kijasusi zinaelekezwa pia Korea Kaskazini kulikomboa taifa lile mapema.
Aiseee.
Safi sana.
Kuna nchi ndogo TU kama Iran wameishindwa,wataiweza Urusi.
Nchi yenye jeshi kubwa kabisa duniani,
Majasusi Bora kabisa duniani,
Silaha imara kabisa duniani,
Raisi makini kabisa duniani.
 
Back
Top Bottom