Rais Kenyatta aruhusu Watanzania kuanza kufanya kazi na biashara Kenya bila kuwa na Work Permit wala Business visa

Kigelegele kwa Kenyatta aruhusu watanzania kuanzia sasa ruksa kufanya kazi na biashara kenya bila kuwa na work permit wala Business visa.

Kasema mida hii mkutano wa wafanya biashara.
Anajua hatuwezi ku compete na wakenya. Ukitaka kuhakikisha nasisi turuhusu hivyo hivyo uone wakenya watakavyochukua ajira zote hapa tz hasa mashirika na sekta binafsi.

Sent from my TECNO RA7 using JamiiForums mobile app
 
Kigelegele kwa Kenyatta aruhusu watanzania kuanzia sasa ruksa kufanya kazi na biashara kenya bila kuwa na work permit wala Business visa.

Kasema mida hii mkutano wa wafanya biashara.
Nilijua tu serikali ya CCM itanasa kwa ulaini kabisa! Hivi kweli kwa akili yako Mtanzania anaweza akapewa fursa ya kufanya kazi Kenya? Labda kuwa scavenger (mzoa taka) pale Nairobi na miji mingine!
 
sasa hapo mbona ni kosa letu kama nchi, mkenya ameona fursa tumezubaa , bado unamlaumu kwa lipi ?
viwanda tulikuwa navyo tukauwa kwa sera zetu mbovu ,wenzetu wamejitahidi kuvitunza na ndo vinatoa ajira na kulipa kodi vizuri
leo hii siagi tunategemea blueband , wakati tulikuwa na Tanbond yetu tukauwa , halafu tunataja tulaumu kwa nini mkenya analeta proceesd goods kwetu.
 
Kigelegele kwa Kenyatta aruhusu watanzania kuanzia sasa ruksa kufanya kazi na biashara Kenya bila kuwa na work permit wala Business visa.

Kasema mida hii mkutano wa wafanya biashara.
Je umejiridhisha hilo jambo(hiyo ruhusa) haliko kwenye protocol za East Africa Community?
 
Zanzibar tu mbara hana uhuru wa kufungua biashara wala kuajiriwa akitaka awaruhusu kenya kufanya hivyo Zanzibar
 
Mama angalie mtego huu ili kulinda raia wake maana Kenya hawana cha kupoteza kwenye fursa ya kila kitu hadi omba omba barabarani.
Omba omba kutoka 🇰🇪 Waje 🇹🇿 Wafanye nini? Na hizo pesa zenu zisizo na thamani?

Make it make sense
 
Sasa kama inamilikiwa na Kenya Airways na bado inafanyiwa figisu. Nini kinakuaminisha kuwa ATCL kwenye route hiyo itapata huruma kibiashara?.
Kwanini tuandikie mate na wino upo? ATCL waombe kibali cha kuanzisha safari za nairobi...kama wakifanyiwa figisu then tutakua na evidence kwamba kenya wanatuhujumu na tunaweza kuchukua hatua.
 
Hotuba yake nzima kenyatta hii hapa

 
Nasoma comments za kwene huu uzi, nyie Watanzania hata mubebwe mgongoni kabisa hambebeki, mumekua mnalalamika kwa sisi Wakenya tuna makampuni 500 Tanzania, ilhali nyie mumewekeza 30 pekee hapa Kenya, sasa sijui mfanyiwe nini, haya vikwazo vyote vimeondolewa bado mnalialia......
 
Hivi kenya kuna ajira gani kwa watanzania,hili chaka la working permit tusijaribu kuliingua kwenye biashara hapo sawa,kwenye ajira watuache kwanza kidogo
Kasema mkafanye biashara siyo kutafuta ajira.

Sisi wauza mahindi mama katufungulia milango soon na sisi tutaanza kujenga magorofa na kusomesha watoto wetu IST.

[emoji122][emoji122][emoji122][emoji2223][emoji2223][emoji2223][emoji2223][emoji2223][emoji2223][emoji2223][emoji2223][emoji2223][emoji2223][emoji2223][emoji2223][emoji2223][emoji2223][emoji2223][emoji2223][emoji2223][emoji2223][emoji2223][emoji2223][emoji2223][emoji2223][emoji2223][emoji2223][emoji2223][emoji2223][emoji2223][emoji2087][emoji2087][emoji2087][emoji2087][emoji2087][emoji2087][emoji2087][emoji2223][emoji2223][emoji2223][emoji2135][emoji2101][emoji2101][emoji2101][emoji2101][emoji2101]
 
Mtego huu, anataka na Samia aseme hivyohivyo kwa wakenya
Twafa!! Ametegeshea na mama aseme hivyo hivyo!! Twafa!!
Mazingira ya watanzania kufanya biashara na kazi Kenya si rafiki! Kwa hiyo pamkja na kuruhusiwa bado ni watanzania wachache sana watakaothubutu kwenda Kenya kufanya biashara au kufanya kazi. Lakini ukifungulia mlango huo kwa wakenya kuja Tanzania, ndani ya miezi 6 kila sehemu ya Tanzania watajaa wakenya na tutajikuta watanzania tunakuwa watumwa ndani ya nchi yetu wenyewe!! Ni kama wachaga walivyotapakaa kkla kona. Wao ni sawa maana ni watanzania. Yeye ameruhusu sisi tusiruhusu!
 
Huo ni mtego, Watanzania tujihadhari kesho tutageuziwa kibao, ndio maana nchi kama Marekani, inajaribu kupunguza biashara na China ila kulinda soko la ajira na biashara kwa Wamarekani.
 
Mkuu kula 100, huo ni mtego, sijui tunaenda wapi, Wakenya watafurika hapa nchini hadi wapika chai watakuwa wao, hiyo karibu ya Kenyata ni sumu kwenye kikombe cha dhahabu.
 
Siyo suala la unyonge! Kwao hakuna nafasi lakini anasema njoo! Ukienda hutapata nafasi ya ardhi ili ujenge kiwanda chako kwa mfano. Kwetu kuna nafasi kwa hiyo wakija wanapata nafasi.
Ni sawa na familia mbili zikubaliane kuoleana! Vijana wako wakija kuoa kwangu sitawatoza mahari! huku nikijua kabisa sina mabinti wa kuozesha maana tayari walishaolewa!
Lakini nimeona wewe bado una mabinti wengi tu hawajaolewa! Ukikubali nitakuwa nimekuingiza mkenge!
 
Wacheni uoga na kutojiamini nyinyi mliobatizwa jina la wanyonge nanyi mkakubali tena kwa kushangilia.
 
Mkuu kula 100, huo ni mtego, sijui tunaenda wapi, Wakenya watafurika hapa nchini hadi wapika chai watakuwa wao, hiyo karibu ya Kenyata ni sumu kwenye kikombe cha dhahabu.
Mbona wachina wapo hadi wauza karanga mitaani lkn hamfungui midomo yenu kuwasemea?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…