Rais Kikwete awasili Dodoma katika maandalizi ya kulifungua Bunge la Katiba.

Rais Kikwete awasili Dodoma katika maandalizi ya kulifungua Bunge la Katiba.

MwanaDiwani

JF-Expert Member
Joined
Mar 22, 2013
Posts
5,536
Reaction score
2,266
PG4A1229.jpg

Rais Jakaya Kikwete akizungumza na Makamu wa Rais, Dr. Mohamed Bilal, Waziri Mkuu, Mizengo Pinda na Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana baada ya kuwasili kwenye uwanja wa Ndege wa Dodoma
PG4A1249.jpg

Rais Kikwete akiongea na baadhi ya viongozi wa CCM na serikali ya CCM baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa Dodoma.
 
Pamoja na kelele nyingi, lakini ikumbukwe kuwa, ni hisani ya CCM kwa kupitia matakwa ya wananchi katika kuendana na muda unaokuja mbeleni ndiyo iliona haja ya kuridhia mchakato wa kuwepo katiba nyingine ambayo itakidhi matakwa ya kitaifa kwa kipindi kingine kama cha maisha ya katiba hii ya mwaka 1977 tunayoitumia kwa sasa.

Kuna watu wanakuja na hoja za kusema Ilani ya uchaguzi ya CCM ya mwaka 2010 haikuainisha umuhimu wa kuwepo kwa katiba mpya lakini hao hao wanasahau kuwa ndiyo wananchi hao hao walioipatia CCM ridhaa za kuongoza nchi kwa mamilioni ya kura pamoja na kutokuwepo kwa kipengele cha mchakato wa kupata katiba mpya. Wananchi waliona ni CCM pekee itakayoweza kuwatengenezea mazingira mazuri katika upatikanaji wa katiba mpya ndiyo maana wakaamua kwanza kuipa kura za ushindi 2010 ili baada kwa kupitia CCM waweze kufikia malengo yao ya upatikanaji wa katiba mpya.

CCM haipo madarakani by default, la hasha bali imeendelea kuwepo kwa sababu kuu moja ambayo ni kuwaelewa wananchi walio wengi na kukubaliana na matakwa yao katika njia ya kuyafikia malengo yao bila kuwabagua hata wale wachache wenye malengo tofauti katika sera na Ilani za uchaguzi.

CCM ni amani, CCM ni upendo, CCM ni Mshikamano na CCM ni furaha.

CCM ni Itikadi, CCM ni sera, CCM ni Ilani ya uchaguzi na CCM ni ushindi.

Baada ya uchaguzi mkuu 2010, wananchi waliona kuna umuhimu wa kuandika katiba mpya na kwa sababu CCM ni chama kinachosikiliza mawazo ya wananchi wote (chama sikivu), basi kikaona kuna umuhimu wa kukubaliana na matakwa ya wananchi.

Wananchi wanafahamu kuwa, haiwezekani mwizi akaanza kukueleza njia ya kulinda nyumba yako wakati maisha yake yanategemea wizi, hii ina maana kuwa, haiwezekani wananchi wakakupa kura kwa kujipambanua tu wewe ni mwanademokrasia na kioo katika maendeleo ya taifa wakati ndani ya chama chako hakuna hata uhuru wa kutofautiana kimtazamo achilia mbali kifikra. Lakini kikubwa zaid, ubaguzi ndiyo kigezo cha utendaji ndani ya chama. Kama wewe hukubahatika kuzaliwa eneo lileee au hutoki kuleeee basi uwepo wako ndani ya chama unakuwa una mashaka makubwa labda uwe ni kondoo katika maamuzi yao ndani ya chama.
 
Kikwete asimamie anayohubiri na si mbele ya umma anasema hivi alafu baadae kwenye vikao vya chama anabadilika!! Tutajua alafu haitamjenga!
 
Kikwete asimamie anayohubiri na si mbele ya umma anasema hivi alafu baadae kwenye vikao vya chama anabadilika!! Tutajua alafu haitamjenga!
Kwanza nianze kwa kukusahihisha. Rais huwa hahubiri. Wahubiri wako kwenye nyumba za ibada ambako mzizi wake ni imani kwa maana kuwa, serikali kazi yake ni kutekeleza yale yaliyoainishwa na chama tawala kupitia sera na ilani yake ya uchaguzi na siyo kuwaaminisha watu jambo lolote.

Inawezekana wewe humuelewi Rais wetu ndiyo maana unaona kama anachokifanya siyo kile anachokisema. Huwezi kupewa kura na chama chako na pia wananchi kwa kutokusimamia kile unachokisema.

CCM iliamua kumpitisha awe mgombea wake vipindi viwili katika kuongoza taifa kwa sababu iliona kauli zake zinaendana na matendo yake kiutekelezaji.

Inabidi uzijongee fikra zako tena.
 
Pamoja na kelele nyingi, lakini ikumbukwe kuwa, ni hisani ya CCM kwa kupitia matakwa ya wananchi katika kuendana na muda unaokuja mbeleni ndiyo iliona haja ya kuridhia mchakato wa kuwepo katiba nyingine ambayo itakidhi matakwa ya kitaifa kwa kipindi kingine kama cha maisha ya katiba hii ya mwaka 1977 tunayoitumia kwa sasa.

Kuna watu wanakuja na hoja za kusema Ilani ya uchaguzi ya CCM ya mwaka 2010 haikuainisha umuhimu wa kuwepo kwa katiba mpya lakini hao hao wanasahau kuwa ndiyo wananchi hao hao walioipatia CCM ridhaa za kuongoza nchi kwa mamilioni ya kura pamoja na kutokuwepo kwa kipengele cha mchakato wa kupata katiba mpya. Wananchi waliona ni CCM pekee itakayoweza kuwatengenezea mazingira mazuri katika upatikanaji wa katiba mpya ndiyo maana wakaamua kwanza kuipa kura za ushindi 2010 ili baada kwa kupitia CCM waweze kufikia malengo yao ya upatikanaji wa katiba mpya.

CCM haipo madarakani by default, la hasha bali imeendelea kuwepo kwa sababu kuu moja ambayo ni kuwaelewa wananchi walio wengi na kukubaliana na matakwa yao katika njia ya kuyafikia malengo yao bila kuwabagua hata wale wachache wenye malengo tofauti katika sera na Ilani za uchaguzi.

CCM ni amani, CCM ni upendo, CCM ni Mshikamano na CCM ni furaha.

CCM ni Itikadi, CCM ni sera, CCM ni Ilani ya uchaguzi na CCM ni ushindi.

Baada ya uchaguzi mkuu 2010, wananchi waliona kuna umuhimu wa kuandika katiba mpya na kwa sababu CCM ni chama kinachosikiliza mawazo ya wananchi wote (chama sikivu), basi kikaona kuna umuhimu wa kukubaliana na matakwa ya wananchi.

Wananchi wanafahamu kuwa, haiwezekani mwizi akaanza kukueleza njia ya kulinda nyumba yako wakati maisha yake yanategemea wizi, hii ina maana kuwa, haiwezekani wananchi wakakupa kura kwa kujipambanua tu wewe ni mwanademokrasia na kioo katika maendeleo ya taifa wakati ndani ya chama chako hakuna hata uhuru wa kutofautiana kimtazamo achilia mbali kifikra. Lakini kikubwa zaid, ubaguzi ndiyo kigezo cha utendaji ndani ya chama. Kama wewe hukubahatika kuzaliwa eneo lileee au hutoki kuleeee basi uwepo wako ndani ya chama unakuwa una mashaka makubwa labda uwe ni kondoo katika maamuzi yao ndani ya chama.


Unapojidanganya kuhusu ridhaa ya watanzania usisahau kupata hesabu ya watanzania waliowapigia kura.... Kwamba ni chini ya asilimia 20 ya watanzania wote waliotakiwa kupiga kura 2010. Yaani ukipanua wigo ni chini ya asilimia 5 ya watanzania wote. Tena usisahau ni uchaguzi ambao idadi ya waliopiga kura ilikuwa chini kuliko nyakati zote tangu Tanganyika na Zanzibar zijipatie uhuru.

Huo ukweli ukiweza kuutafakari then ni vizuri ukajikumbusha nini maana ya ridhaa ya wananchi. Kama busara ingekuwepo hii ni aibu tosha kufungua mdomo na kusema CCM ilipewa ridhaa ya kuongoza nchi hii. Kwasababu mmejikinai na kuiua dhamira zenu basi hata soni na busara zimewakimbia.
 
Back
Top Bottom