Rais anapozungumza na kundi fulani la jamii, ndio anafikisha ujumbe kwa Taifa zima. Mara nyingi maRais wa Tanzania wamekuwa wakizungumza na Wazee wa Dar es Salaam manake Serikali iko Dar, japo wanadai Makao Makuu yako Dom. Hivyo kwa kuwa Makao Makuu ya Serikali yako Dom, na Rais alitaka kulihutubia Taifa kuhusu mtikisiko wa Uchumi, alichagua Wazee wa Dom na Wabunge kulifikishia ujumbe Taifa. Anaweza pia kuamua kuhutubia Wazee wa Singida, Ruvuma ama Mjini Magharibi. Kama alivyolihutubia Taifa Mwanza alipozungumzia pamoja na mambo mengine Sangara (mapanki). Hivyo aweza kuhutubia mkoa wowote na kuwaita Wazee. Wazee ni hazina.