Rais kusafiri nje ni Utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi 2020|25

Rais kusafiri nje ni Utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi 2020|25

Jabali la Siasa

JF-Expert Member
Joined
Jul 10, 2020
Posts
2,823
Reaction score
2,466

Shaka: Kibali Rais Samia kusafiri nje amepewa na CCM​

MONDAY DECEMBER 06 2021​


kibali pic

Summary

Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Shaka Hamdu Shaka amesema kibali cha kusafiri nje ya nchi, Rais Samia Suluhu Hassan amepewa na Ilani ya Uchaguzi ya chama hicho.

Dar es Salaam. Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Shaka Hamdu Shaka amesema kibali cha kusafiri nje ya nchi, Rais Samia Suluhu Hassan amepewa na Ilani ya Uchaguzi ya chama hicho.

Shaka ameeleza hayo leo Jumatatu Desemba 6, 2021 mbele ya Rais Samia, kwenye hafla ya kuzindua kiwanda cha Elsewedy Electronic East Africa Ltd cha kuzalisha vifaa vya umeme (Electronic Products ) kilichopo Kisarawe II, Wilaya ya Kigamboni Dar es Salaam.

Shaka amesema kumekuwa na maswali mengi kwa watu kuhoji kwanini Rais huyo amekuwa akisafiri nje ya nchi mara kwa mara na kwamba ilani ya chama hicho imempa njia na nguvu namna ya kusimamia diplomasia ya uchumi wa ndani ya nchi.

“Kumekuwa na maswali kwanini Rais anasafiri sana nchi za nje. Amepewa baraka na kibali cha kusafiri nje ya nchi na ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi ibara ya 132 kifungu kidogo cha 18, kifungu kidogo cha 22 kifungu kidogo cha 32 kifungu kidogo cha 46imemuonesha namna ya kusimamia diplomasia ya uchumi wan chi.,”amesema Shaka

Amesema Uongozi ni kitu cha ajabu sana na uhalisia wa uongozi utangulizwa na uzalendo na kwamba Rais huyo ameshaonesha asilimia 100 kutokana na ujasiri,utayari,karama ya udhubutu wa kutekeleza ilani kwa Weledi na kwa mafanikio makubwa.

Amesema hadi sasa Rais huyo muelekeo wake ni mzuri na alipeleka taifa kule ambako walio wengi wanatarajia kuwa na uchumi unaokuwa kila siku ndani ya Afrika na kuwafanya watanzania kujivunia nafasi yao ya kijiografia.
 
Mbona kuna mtu hakutoka nje ya nchi ila Uchumi uliporomoko hadi 4.1%?

Mimi Mama chapa kazi Watu tunaona,

Wawekezaji 111 tungewapa wapi?

Nchi imefunguka Mama Chapa Kazi,
 
Sawa, huo uzalendo uanze kwa kumalizia bwawa la nyerere na kupunguza gharama za umeme kama tulivyosikia Waziri Mkuu akieleza. Jamani mkumbuke hapa duniani tunapita tuu, tamaa zina mwisho, lets improve people's lives.

Hamna thawabu kubwa kama hiyo. Malizieni hilo bwawa tupate umeme wa bei ndogo. Michezo ya dana dana iachwe, wengine tutaupima uzalendo kuanzia hapo.
 
Sawa, huo uzalendo uanze kwa kumalizia bwawa la nyerere na kupunguza gharama za umeme kama tulivyosikia Waziri Mkuu akieleza. Jamani mkumbuke hapa duniani tunapita tuu, tamaa zina mwisho, lets improve people's lives. Hamna dhawabu kubwa kama hiyo. Malizieni hilo bwawa tupate umeme wa bei ndogo. Michezo ya dana dana iachwe, wengine tutaupima uzalendo kuanzia hapo.
Hujasikia leo Elsewedy leo walivyosema kuhusu bwawa hili mkuu,Tuombe uzima mwakani utaona matokeo
 
Mkuu JPM alinunua Njiwa cash acha rais ale mema ya nchi sisi wadanganyika ndani ya Tanzakiza acha tupambane na mfumuko wa bei
 
Haya wazee, acha king hangai amalizie sehemu ya utalii wake.

Hizi nafasi ni nadra sana ukizipata zitumie kikamilifu kama mkwere, livyo zitumia.

Anyway diplomasia inakuwa kwa kasi ya madeni.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kweli kabisa Sir

Hata aliepita alikuwa anatenbea na mabulungutu ya hela na kugawa anavyotaka

Na alinunua jogoo kwa Laki

Mahindi akaambiwa 5000 hiii bhagoshaa

Kila Rais na design yake tu sijui ajae atakuwaje maana kila mmoja na style yake
 
Back
Top Bottom