Rais kuteua ma-Vice chancellor vyuoni; Katiba mpya itamke vipi?

Rais kuteua ma-Vice chancellor vyuoni; Katiba mpya itamke vipi?

MNYISANZU

JF-Expert Member
Joined
Oct 21, 2011
Posts
7,046
Reaction score
1,102
Huu ni mjadala, tujadili katiba mpya itamke vipi kuhusu hili?
 
Ni suala la madaraka makubwa ya Rais haipaswi kuwa hivyo.
 
Siasa ziwekwe mbali na maeneo ya kitaaluma. Kwa VC kuteuliwa na Rais, huko ni kuleta siasa vyuoni-kitu ambacho wote (bila kujali itikadi zetu) tutakuja kukijutia. Siku hizi hawa ma-VC hawafanyi tena kazi za taaluma, wao ni siasa mwanzo mwisho. Mfumo wa sasa haufai ktk mazingira haya ya siasa za vyama vingi na ushindani mkali wa sasa.

Kila wanachokiamua, kwanza wanakuwa wamekiangalia kwa lenzi ya siasa. Mfano mzuri ni kufukuzwa wanafunzi UDSM hivi karibuni. Hawakuishia kuwafukuza tu, wameamua wasisome chuo chochote cha Umma na hata kupata mkopo wa bodi. Sasa hapa tujiulize UDSM wamepata wapi mamlaka ya kuzuia wanafunzi waliowafukuza wasidahiliwe vyuo vingine vya umma? Toka lini UDSM ikawa na mamlaka ya kuviamulia vyuo vingine vya umma kama sio siasa hizi?

Mwisho nipendekeze mchakato wa kumpata VC uanzie ngazi za chini kabisa ktk chuo husika. Wahadhiri wapendekeze majina ambayo TCU watachagua mmojawapo. Hii itawafanya ma-VC kuwajibika kwa wanataaluma wenzao, badala ya kuwajibika kwa wanasiasa na chama tawala na kuwadharau wanataaluma wenzao kana kwamba hawajawahi kuwa wanataaluma.
 
Unatakaje? wapigiwe kura?
Uchaguzi wa serikali ya wanafunzi uambatane na uchaguzi wa VC
OTIS
 
Kila chuo Kuna seneti(kikao cha directors and deans of faculties) hiki kikao ndio kichague kwa kupiga VC based on stated qualifications. Kwahiyo ni lazima mtu atimize vigezo Kabla ya kupigiwa kura.
 
Back
Top Bottom