Replica
JF-Expert Member
- Aug 28, 2017
- 1,681
- 8,887
Rais Magufuli leo akiwa njiani kutoka msibani, amesimama mara kadhaa kuwasalimu wananchi na kuwasikiliza. Ameshangazwa na watu walio chini yake kushindwa kujenga choo cha soko ilihali mapato ya halmashauri yao ni zaidi ya bilioni 1.8
Rais Magufuli ametoa agizo la choo husika kukamilika ndani ya siku saba la sivyo mkurugenzi aandike barua ya kuacha kazi. Pia ameagiza siku saba wakati choo kinajengwa wananchi waende kujisaidia nyumbani kwa DC pamoja na mkurugenzi ambae nyumba yake iko mtaa wa pili kutoka soko lilipo kwani nchi haiwezi kukosa choo wakati wanakusanya bilioni 1.8.
Amesema yuko 'very serious' na suala hilo hivyo mwananchi akibanwa afunguliwe. Amewaamirisha wawatayarishie maji ya kutosha lakini kama wana akili watajenga usiku na mchana.
Rais Magufuli amesema haiwezekani wakusanye bilioni moja kutoka kwa wananchi alafu washindwe kuwajengea choo hivyo amewataka wafanyibiashara sokoni hapo kutolipa ushuru kuanzia leo mpaka siku kitapojengwa choo.