Rais Magufuli aiagiza Wizara ya Nishati kumrejesha kazini mara moja aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa TPDC, Dkt. James Mataragio

Nadhani JK hivi sasa atapumua! Manake kaenda SA kumchukua yule mama aliyekuwa TIC, kaja bwana Mkubwa kamtema! Huyu nae alimtoa kwenye kazi yake mzuri tu US, miaka miwili baadae, akakutana na fitina za wabongo!

Kwanza hapa JPM asijikoshe, na nimeona misukule yake hapa ikijifanya kusifia! Ni taasisi nyingi tu zilitajwa kufanya wrong doing na CAG, ni kwanini mkono wa sheria uliwakumba TPDC peke yake?! Tusisahau kwamba, ni huyu huyu JPM ndie alitangaza hadharani kwamba gas yote tumeibiwa, na kwahiyo kuna uwezekano mkubwa kufikishwa mahakamani kwa Matagilo kuna mkono wake! Yaani ni yale yale unasimama hadharani na kusema ana ushahidi kwamba polisi wale walikula rushwa na kusindikiza wezi wa dhahabu, 6 months later, yule yule aliyesema ana ushahidi, hatimae anatangaza polisi wale wale aliosema wamekula rushwa, hivi sasa waachiwe huru na kurudishwa kazini mara moja!
 
Mizuka, mihemuko na majungu yametawala awamu hii, ni ngumu sana kufanya kazi / biashara n.k kwa kutumia utaalamu / uzoefu wako lazima wanaojiita 'wazalendo' wakuangushe.

Rais ameanza kufanyia kazi ndio sababu ameanza kuwarejesha

Kuna Mmoja wa ATC aliambiwa eti anatengeneza tiketi zake binafsi za ndege
 
Enzi hizo Magugupori anafukuza tu kila Mkurugenzi asiyempenda, kila Mkurugenzi asiyetoka Kanda ya Ziwa au asiye Msukuma, kila Mteule wa Kikwete... now the wranglings within his corrupt political party have brought him to his knees and he is made to swallow his own bitter pills!
 
I am so happy. Tulikua tunapoteza hii brain kwa sababu za kijinga kabisa.

Bodi ya mhongo ilikua ya kipumbavu kabisa.

Hivi unamuachaje Dr. Mataragio nje ya mambo ya gesi na mafuta?

Dokta kapige kazi. Uadilifu wako umeonekana baada ya yote.
Mnachonifurahishaga ni kupongeza kila uamuzi wa Magugupori...wakati ule Dr. Mataragio amesimamishwa kazi mlishangilia, na leo anarudi kazini mnashangilia pia😅😅
 
Si yule alikuwa kajikadiria mshahara,posho etc?
 
Sawa kabisa Mkuu na kampuni aliyoipa tenda ni ya Houston, Texas ambayo kabla ya kuja Tanzania alikuwa muajiriwa kwenye kampuni hiyo. Tetesi zinadai alitakiwa kukabidhi passport yake ili “asitoroke” nchini ila sijui kama bado yupo nchini au alishaondoka.

 
Hii taarifa sijui imetoka wapi. Haionekani kwenye vyanzo halisi vya Ikulu. Kwenye Website na Twitter ya Ikulu Mawasiliano, haipo hii taarifa.
 
Alifukuzwa na bodi ya wakurugenzi ilikuwa chini ya mwenyekiti profesa Sufian
 

Moja ya silaha kubwa ya JPM inayo mfanikisha uongozi wake ni kutokuendesha uongozi wake kwa mazoea.
 
Alikabidhi passport kweli....takukuru walimkalia vibaya sana! Yani nilikuwa namuona mpaka nahuzunika!

Pale TPDC, gesi inayotoka mtwara na inatumika pale kinyerezi kwa tanesco, kinyerezi 1&2, its only 7%!

Niliposikia hii nilichoka, hivi stiglers bwana mkubwa aling' ang'ania ya nini?
 
Reactions: BAK
Msechu hapana sikuona umuhimu wake kwa watz wa kawaida.
Mambo ya watzn wa kawaida na biashara ni vitu viwili tofauti,kwani ndege zinazonunuliwa zinawalenga wanyonge au watanzaania wa kawaida?
Warudishwe wote waliokuwa wanafanya vyema hadi mashirika yaanze kujiendesha kibiashara ndipo nyie wa kawaida mtafikiriwa
 
Jiwe a.k.a Hawafu akakurupuka na Maguvu yake akamtengua Leo anamrudisha tena hata Muhongo nae atarudi tu
 
Hilo ni swali zuri sana Mkuu. Trillions zimetumika kwa miradi ya gesi, huyo nduli kuingia kaachana nayo karukia Stiegler!!! Sababu kubwa ni upigaji tu Mkuu, hakuna sababu ya maana.

 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…