Rais Magufuli ameshatimiza ndoto mbili za mwalimu Nyerere, kuhamia Dodoma na Stiegler's Gorge. Bado ndoto moja!

Rais Magufuli ameshatimiza ndoto mbili za mwalimu Nyerere, kuhamia Dodoma na Stiegler's Gorge. Bado ndoto moja!

johnthebaptist

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2014
Posts
97,869
Reaction score
171,716
Mwalimu Nyerere kama kiongozi alikuwa na ndoto zake na miongoni mwa ndoto hizo ni pamoja na Kuhamishia makao makuu ya serikali Dodoma, pili kumiliki njia kuu za uchumi na tatu kuwa na bwawa kubwa la kuzalisha umeme Stieglers Gorge.

Katika uongozi wake kama Rais, Dr Magufuli ameweza kuhamishia makao makuu ya serikali kwenda Dodoma.

Pili amefanikisha ujenzi wa bwawa la Stieglers Gorge ambapo mkandarasi ameshapatikana na mkataba umesainiwa.

Tatu, Rais Magufuli ameshaanza kuhakikisha serikali inakuwa na umiliki katika njia kuu za uchumi, amefufua ATCL, TRC inaimarishwa na taasisi nyingine za miundombinu zinaimarishwa na hii ndio ndoto ambayo Nyerere aliifanikisha lakini mabeberu wakaitibua kwa kugawana mashirika yetu karibia yote.

Nina imani Rais Magufuli ataikamilisha ndoto hii ya mwalimu Nyerere.

Naomba niishie hapo!
 
Yaani kipi cha kumsifia? Yaani Mwl. Nyerere aote alafu Magufuli aje kufanyia kazi ndoto za mtu! Moja ni kuonesha yeye hakuwahi kuwa na ndoto wala maono!

Kinacho chekesha mpaka sasa hajawahi kutuambia anataka kuifanyia nini Tanzania. Kila akiamua anajipya bora angekuwa na jambo moja la kuifanyia nchi aliloona litaa na kudumu milele, kupambana na kila kona kuna atashutuka muda umeisha na hakuna alichofanya.
 
Watu wenye fikra za kisoshalisti kazi mnayo, usoshalisti ulishakufa duniani kote maana ulishindwa vibaya mno.

Amebaki Korea kaskazini ambae kiongozi wa dola ya kisoshalisti anaishi kwa anasa akitumia hela za nchi na walipakodi, mtapata tabu sana huo ujamaa ni wa ovyo na ulisha jifia.
 
Mwalimu ajawahi kuwa na ndoto izo

Ndoto zake zilikuwa kumaliza ujinga, maradhi na umaskini na jpm hajafanikiwa hata robo juu ya hayo.

Hyo kuhamia dodoma, kuwa na umeme yalikuwa mawazo yake ila si ndoto.
 
Alisema mwezi wa kumi na mbili anahamia dodoma, amebakisha wiki mbili hapa mjini asijisahaulishe.
 
Back
Top Bottom