Rais Magufuli anajaribu kuifutia CCM dhambi zake

Rais Magufuli anajaribu kuifutia CCM dhambi zake

kavulata

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2012
Posts
13,778
Reaction score
14,214
Tanzania ilipata Uhuru kutoka kwa mkoloni miaka karibu miaka 60 iliyopita. Miaka 60 Ni mingi sana, inatosha kwa wananchi wote kupatiwa maji, umeme, viwanda, hospitali, shule, mabwawa ya umeme na umwagiliaji, reli, barabara kutokana na wingi wa rasilimali zilizoko nchini.

Kwa miaka 60 CCM haikuwapa wananchi maji na sasa wanataka wasifiwe kwa kuwapelekea wananchi maji leo, hawakupeleka umeme na sasa wanataka wasifiwe kwa kupeleka umeme, waliua viwanda sasa wanataka wasifiwe kwa kufufua viwanda, waliua reli sasa wanataka tuwasifu kwa kufufua reli, kwa miaka 60 hawakujenga shule za kutosha sasa wanataka tuwasifu kwa kujenga shule, walianzisha ulaji rushwa sasa wanataka sisi tuwasifu kwa kuuondia rushwa. Hivi ni vitu ambavyo vilikuwa vifanywe na CCM miaka 60 iliyopita ya Uhuru.

Jitihada anazozionyesha leo mh. Rais ni namna tu ya kujaribu kuifutia dhambi CCM. Wana CCM ndio wanaopaswa kumsifu sana kwa kuwafutia dhambi zao kwa wananchi kuliko wananchi wa kawaida.

Natamani mh. Rais angekuwa mgombea kupitia vyama vya upinzani kuliko CCM kwasababu wananchi wanaiona CCM kama chanzo cha shida zote zinazowakabili ambazo Rais JPM anakabiliana nazo leo. Hata angefanya Nini wapinzani wa CCM watakuwepo tu palepale. Ni Heri angetumia chama kingine.
 
Watanzania tumeshuhudia maiti za watanzania wenzetu zikiokotwa kwenye fukwe zikiwa zimefungwa mawe na vyuma na nyingine zikiwa kwenye viroba.

Watanzania, tumeshuhudia wenzetu wakitekwa na kupotezwa, wafanyabiashra wakifilisiwa,.

Tumeona ndugu na jamaa zetu wakifunguliwa makesi makubwa na yasiyo na dhamana.

Huyu mtu hatufai kabisa.
 
Miaka yote tangu tupate uhuru Magufuli hakuwa raisi , na maraisi wote waliopita walifanyiwa tathmini. Tunampima kwa miaka mitano ya uraisi wake
 
Miaka yote tangu tupate uhuru Magufuli hakuwa raisi , na maraisi wote waliopita walifanyiwa tathmini. Tunampima kwa miaka mitano ya uraisi wake
Wananchi wanaipima CCM sio Magufuli. Kwanini CCM imefanya na haikufanya hivi, vile, hiki, kile, haya, Yale hadi leo?

Wananchi wanajiuliza kwanini CCM inatumia njia za wazi na za Siri, zinazofahamika na zisizofahamika kulazimisha kubaki madarakani?.

Kwanini CCM Ni lazima ishinde bila kufikiria hatima (consequences) za kulazimisha kushinda.

Ukiangalia na kutafakari kwa makini CCM ndio itakayokuwa chanzo Cha kuvurugika kwa amani na utulivu wa nchi yetu huko mbeleni, watu wa CCM hawajali nini kitalikumba taifa Kama wataendelea kushinda nje ya visanduku vya kura.

Wanachokisahau CCM wanajeshi Ni raia pia wa Tanzania ambao mama zao Ni waoka vitumbua Kama mama wengine ambao wanahitaji maji, elimu, umeme, heshima na kulindwa kwa kura zao walizozitumbukiza kwenye visanduku vya kura.

Na mbaya zaidi kuliko yote hakuna Rais anayetaka CCM imfie mikononi mwake, hivyo kila goti litapigwa ili CCM ishinde.
 
Back
Top Bottom