Rais Magufuli: Hakuna Lockdown kwa Dar wala Tanzania, NEVER! Tusiwatishe watanzania, hofu ni ugonjwa mkubwa kuliko Corona

Habari zenu wana jf.lengo la hii thread nilitaka kuuliza kuhusiana na hii hoja ambayo imetolewa na c.c.m chini ya rais magufuli juu ya kutotoa amri ya watanzania kubaki nyumbani(lockdown) watuhumiwa wakubwa wa ni upande wa upinzani ndio waliotoa hoja hii.naombeni toka kwenu mnijuze ni nani na lini kiongozi wa upinzani alitowa tamko hili.
 
Mbowe Ndio analilia lockdown Mkuu

Km unavyojua Mbowe Ndio kabeba akili za makamanda wote nao wakadandia
 
Ni jambo jema sana!

Huu ndio mkutano siyo ule wa Mbowe uliotaka kutuharibia maombi ya kitaifa!
Ni vyema ukavua hilo shuka la upumbavu ulilojifunika labda ndio utajua hali halisi ya yanayoendelea nchini!
hali ni mbaya sana, watu wanzidi kuteketea, acha kuandika ujingakila kukicha!
 
Kwa akili zako unaona umeandika points? tatizo la wa TZ ni ujinga wa wengi!
 
Ajabu kidogo, watu wenye ufahamu wamekaa kulalamika kwenye mitandao wakati maelekezo ta WHO yapo na wanaweza kuyapata humu mitandaoni. Vaa maski, epuka misongamano, osha mikono kila wakati, waelezee uwapendao umuhimu wa haya na endelea na maisha.
 
Naona mambo yamepamba moto , hata kwenye ofisi Za Serikali wamerudisha mandoo ya kunawia
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…