Rais Magufuli: Hakuna Lockdown kwa Dar wala Tanzania, NEVER! Tusiwatishe watanzania, hofu ni ugonjwa mkubwa kuliko Corona

Ajabu kidogo, watu wenye ufahamu wamekaa kulalamika kwenye mitandao wakati maelekezo ta WHO yapo na wanaweza kuyapata humu mitandaoni. Vaa maski, epuka misongamano, osha mikono kila wakati, waelezee uwapendao umuhimu wa haya na endelea na maisha.
Magufuli nampenda sana rais wangu, kukiwa na corona yeye huwa anajiepusha na misongamano kwa kwenda zake chato kujipa pumziko.
 
Hata siku moja usisubutu kuamini ndimi ya polirician. Never. Wewe fanya kilicho chema kwako ambacho hakivunji sheria ya nchi. Ukiegemea ndimi za kisiasa unadondoka.
Fanya kama unavyofanya ukibanwa na haja, sijawahi kusikia mtu anasubiria aambiwe na mwingine tena kimya kimya.
 
Fanya kama unavyofanya ukibanwa na haja, sijawahi kusikia mtu anasubiria aambiwe na mwingine tena kimya kimya.
Kabisa mkuu. Mimi nilitegemea sisi tunaojifanya wasomi tumeshaelimisha hata ndugu na majirani wavae mask. Yaani mzee baba angeshhtuka watanzania wamevaa mask hasa mijini. Lakini hakuna kitu. Tufanyeje?
 
Mwanasiasa akisema sasa hivi ni saa sita mchana usikubali, toka nje ukahakikishe kama kweli jua liko utosini
Hahahaha. Mkuu umenena. Yaani hawa watu ni kuwaogopa kama Black Mamba.
 
Kabisa mkuu. Mimi nilitegemea sisi tunaojifanya wasomi tumeshaelimisha hata ndugu na majirani wavae mask. Yaani mzee baba angeshhtuka watanzania wamevaa mask hasa mijini. Lakini hakuna kitu. Tufanyeje?
Si ndio hapo utamsubiri aje akuambie nenda uwani kajisaidie !
 
Saiv tutakaa tu no way out kashaletewa na mabalozi wabobezi tusubiri
 
Kauli ya kukejeli lockdown na kwamba sisi tuendelee kulima ili tuje tuwauzie chakula walioko lockdown ndiyo ilifanya Kenya izuie mahindi yetu kwa kisingizio cha sumu kuvu.
Nani aliyeumia? Wakulima na wafanyabiashara wetu!
Mahindi wanaweza kununua kokote!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…