Rais Mkapa ana ugomvi na Kiswahili chetu?

Mitaa ya Mwembetogwa "maswala" ni vipipi vya mateja, kwa hiyo naweza kuwa naongea Kiswahili cha Mwembetogwa vile vile.

Unaongea Kiswahili cha Mwembetogwa ulipozungumzia hotuba ya Mkapa?
Kweli Mkapa arosto yeye na sera zake
 
Unaongea Kiswahili cha Mwembetogwa ulipozungumzia hotuba ya Mkapa?
Kweli Mkapa arosto yeye na sera zake

Unapoandika "Unaongea Kiswahili cha Mwembetogwa ulipozungumzia hotuba ya Mkapa?"

Unakuwa hujaandika kiswahili chochote kinachojulikana. Labda hiki kipya maana hata Mwebetogwa mateja "wakidevela" hawaongei kama hiki 🙂
 

Umenikumbusha.

Kuna producer mmoja wakuitwa Michael Carter, ana promo yake moja "Radio Mbao" (I am not kidding, there is a "Radio Mbao" on Tune In based on a website) jamaa ananifurahisha sana akipiga hiyo promo, nafikiri hii ndiyo accent ya kibongo halisi , jamaa anakwambia "You are lisiseningi to radio mbao" saa nyingine naona kama anafanya makusudi vile!!
 
Unapoandika "Unaongea Kiswahili cha Mwembetogwa ulipozungumzia hotuba ya Mkapa?"

Unakuwa hujaandika kiswahili chochote kinachojulikana.

Kinachojuulikana na nani? Au ndio kusema Kiranga ana mamlaka ya kuvijua 'Viswahili' vyote?

😛
 

Tatizo letu watanzania ( samahani kwa kujumuisha Watanzania haina maana hiyo sana) hatujui thamani ya kitu chochote ambacho tuna haki nacho ya kujivunia, lugha tatizo mojawapo, Madini ni kama tunayagawa kwa kusingizia wawekezaji, uvuvi ni zero zaidi ya ngwanda za pale ferry, mbuga ukipitia kenya ndiyo utaziona vizuri, mlima kilimanjaro upo tanzania lakini ukiwa Kenya ndiyo utauona vizuri, kwa ufupi Rais Mstaafu kachemka kuongea kiingereza kwa sababu ya aina yoyote ile, nikiwa na maana kama balozi wa Japan katumia kiswahili kuonyesha heshima kwa Watanzania basi Mkapa alitakiwa aongee Kijapani kuonyesha heshima kwa Wajapani, kwa ufupi Viongozi wetu hawapo makini kwa chochote bora tulichojaaliwa watanzania na Muumba, na ndiyo hiyo kuwa sababu tosha ya nchi yetu kubakia na kuringa kwa kuwa nchi ya tatu duniani kupatiwa misaada ambayo nayo pia inaishia kwenye WARSHA ENDELEVU KWA MUSTAKABALI WA MKUKUTA, ni maudhi tu.
 


Hii ni mbinu ya hawa wazee waliojawa na fikra za kikoloni kuendelea kuwatawala watanzania.Wanajua fika ukitoa machapisho /hotuba kwa lugha ya kigeni unapunguza idadi ya watu wenye uwezo wa kuhoji.
 
Mitaa ya Mwembetogwa "maswala" ni vipipi vya mateja, kwa hiyo naweza kuwa naongea Kiswahili cha Mwembetogwa vile vile.

mkuu hii mwembetogwa ya wapi..Iringa au siyo? maeneo ya kule nyuma ya stendi na highland cinema, dah kweli wakati umekwenda.
 
mkuu hii mwembetogwa ya wapi..Iringa au siyo? maeneo ya kule nyuma ya stendi na highland cinema, dah kweli wakati umekwenda.

Huyu keshakula chumvi nyingi, Mwembetogwa anayoizungumzia yeye ni pale Fire, Dar es Salaam :thinking:
 
Huyu keshakula chumvi nyingi, Mwembetogwa anayoizungumzia yeye ni pale Fire, Dar es Salaam :thinking:

Umezibuka wewe!

Unanikumbusha mbali sana enzi hizo wazee wazee kweli.Chaurembo akishika tama kila mtu shurti kumsikiliza. Chamgui akianza kukuhadithia habari za mtume utafikiri alikuwa naye katika safari zake. Changeda babu mwenyewe alishakuwa mzee sana, lakini akikuhadithia habari za mipambano wa Wajerumani Tanga vita vikuu vya kwanza, utafikiri Jemadari alikuwa yeye.

Tulikuwa tunakula kashata na kunywa kahawa na Juliasi pale, enzi hizo kijana mdogo tu, haongei sana, anavaa kaptura bado ana kasumba za Kiskochi na UFabiani. Tukamwambia "Juliasi, wewe umetoka shamba ukaenda Uskochi moja kwa moja, habari za hapa Mwembetogwa wanaovaa vikaputura ni watoto wadogo tu" basi nusura tugombane pale.

Na kuanzia siku hiyo Juliasi akahama mpaka na kikao, akawa mtu wa kukaa sana New Street na hatimaye Magomeni. Lakini New Street tulijua kuna shughuli za siri zikiendelea, badaye sana ndiyo tukajua mambo ya harakati za uhuru.

Ujumbe aliupata, maana vikao vyote vya bao na kina Abdulwahid kuanzia siku hizo mpaka siku za bao la Baba Wandema Msasani Juliasi hakuvaa vikaputula tena, alipoulizwa akadai Dar-es-salaam mbu wamezidi. Huku akicheka kwa bashasha kuonyesha utani mwingi.

Mwembetogwa ya Iringa nilifika siku zile walipomuua yule mwalimu mkuu pale, lakini ninayoiongelea mie ni hii ya pale panapoiwa "Faya".

I'm just messsing with y'all.
 

Hahaha Kiranga unan'dai!
 

Hivi wewe Kiranga ni Linguist au mtu wa vipi ? Maana ni mtata sana inapokuja kwenye masuala la lugha iwe ya Kiinglishi au Kiswahili... Ninaposema mtata naomba nieleweke sio katika hasi bali chanya. Kwenye ile lugha ya wenzetu ya kigeni nakukubali kwa hii ya kwetu sina comment maana nayo bado inaonekana kuwa ni ya kigeni kwa wengine wengi ya wazawa Watanzania kama mimi.. Wengi bad hatujui Kiswahili fasaha. Sasa sijui tutakuwa wageni wa nani maana English matatizo basi hata Kiswahili nacho? We need to be serious on serious issues like national language...
 
Yote uliyosema juu ya Mkapa na huyu limbukeni wetu ni sawa kabisa. Wananadhania kusema Kiingereza ndiyo elimu badala ya fikra. Afadhali hata Nkapa ana fikra kuliko huyu tulie nae.
Npenda kukusahihisha kdogo: Kifursi hakiongewi Iran pekee. Kinaongewa pia Afghanistan, Tajikstan, na baadhi ya sehemu za Turkmenstan,Azarbeijan.......
Fanya utafiti kabla ya kuandika mambo usiyo na uhakika nayo.
 
Kumbe hili "swala", oops!, "suala" mmeshaliongelea kitambo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…