Rais mstaafu wa DR Congo, Joseph Kabila apokonywa walinzi

Rais mstaafu wa DR Congo, Joseph Kabila apokonywa walinzi

Freed Freed

JF-Expert Member
Joined
Jun 27, 2017
Posts
6,547
Reaction score
7,167
Rais mstaafu wa Congo DR, Joseph Kabila Kabange apokonywa walinzi wa kikosi cha jeshi waliokuwa wakimlinda na kupewa ulinzi wa Polisi wa kawaida.

Haijulikani sababu ya uamuzi huu uliofanywa na Serikali ya Felix Tshekedi. Siku za karibuni wawili hao wamekuwa katika mgogoro wa madaraka.

Habari zaidi zinasema Kabila amekimbilia Dubai baada ya hatua hizo.

Chanzo: Radio DW.
 
Hawa jamaa Amani wataendelea kuiskia redioni...jamaa anasahu kua Kabila bado ana influence Jeshini. Now wamemuondolea ulinzi atahisi wanataka kumuua, to protect himself atataka kufanya mapinduzi...then machafuko yataanza upyaaa
 
Sasa unaweza kuona kwanini baadhi ya Nchi Rais anagoma kuondoka madarakani na anataka afie pale.

Hana uhakika na maslahi/maisha yake baada ya kuachia ngazi kwa kuwa hakuna institutions zenye mifumo imara na takwa la Rais ndio inakuwa sheria
 
Hawa jamaa Amani wataendelea kuiskia redioni...jamaa anasahu kua Kabila bado ana influence Jeshini. Now wamemuondolea ulinzi atahisi wanataka kumuua, to protect himself atataka kufanya mapinduzi...then machafuka yataanza upyaaa
Kwa siasa za DRC, kabila kwa sasa hana nguvu hiyo hata jeshini, toka tshekedi aingie madarakani, kuanzia wanajeshi wa ngazi ya juu, aliwafanya wakamtii, na juzi juzi alipowaachia wale watuhumiwa (wanajeshi) waliotuhumiwa kumuua laulent kabila, ndio kabisaa!

Na wananchi na ndio maana hata wanachama wake waengi waliokuwa wakimuunga mkono bungeni, wameshamkimbia!!kwani alijua kabisa kama FAYURU, angetangazwa kuwa mshindi, angetaka kulipiza kisasi haraka, na hapo congo ingeingia vitani!!lakini kwa afanyavyo tshekedi, ameshamaliza nguvu kabila!!na wananchi wengi wa congo ndicho walichokuwa wakikitaka!!kwani bila kufanya hivyo mambo yangeendelea kuwa vile vile tu!!
 
Hawa jamaa Amani wataendelea kuiskia redioni...jamaa anasahu kua Kabila bado ana influence Jeshini. Now wamemuondolea ulinzi atahisi wanataka kumuua, to protect himself atataka kufanya mapinduzi...then machafuko yataanza upyaaa
Kabila huko jeshini,police,usalama kote huko vibaraka wake wameshapanguliwa balaa na bungeni kama ulivyoona kilichotea ameshamalizwa.

Tusubiri kifuatacho ITV.
 
Kabila huko jeshini,police,usalama kote huko vibaraka wake wameshapanguliwa balaa na bungeni kama ulivyoona kilichotea ameshamalizwa.

Tusubiri kifuatacho ITV.
Huwezi pangua wanajeshi walipangwa kwa miaka 18 kwa muda wa miaka miwili...Pia Wanajeshi hawawezi kua Loyal kwa wanasiasa bali kwa wanajeshi wenzao na kwao Kabila ni mwenzao, thus why wanasiasa hua wanajitahidi kuweka ma Generali wanaokubalika Jeshini ukifeli hapo mapinduzi ni nje nje.
 
Huwezi pangua wanajeshi walipangwa kwa miaka 18 kwa muda wa miaka miwili...Pia Wanajeshi hawawezi kua Loyal kwa wanasiasa bali kwa wanajeshi wenzao na kwao Kabila ni mwenzao, thus why wanasiasa hua wanajitahidi kuweka ma Generali wanaokubalika Jeshini ukifeli hapo mapinduzi ni nje nje.
Naona Kabila wanamchukulia poa tu.
 
Tshekedi sasa afanye kazi akili ikiwa imetulia sababu wafuasi wa bwana kabila Bungeni wanaikwamisha serikali ya rais Felix tsheked kwa wingi wao, Lakini tangu serikali ya muungano ilipovunjika kabila na wafuasi wake wamekua wakihaha.
 
Back
Top Bottom