Rais Mwinyi atengua kauli yake, asema Tanzania sasa ni vinyozi, sio kichwa cha mwendawazimu tena

real G

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2013
Posts
5,227
Reaction score
5,299


Rais Mstaafu wa awamu ya pili Ali Hassan Mwinyi amekiri kufuta kauli yake iliyodumu kwa takribani miaka 30 kuwa Tanzania ni kichwa cha mwendawazimu na haitakaa ifanye vizuri kwenye michezo.

Mwinyi ambaye alikuwa mgeni rasmi kwenye mchezo wa kwanza wa hatua ya awali kati ya Simba SC dhidi ya Gendarmerie ya Djibouti, baada ya mchezo alisema kiwango cha mpira nchini kwasasa kimekua hivyo anafuta kauli yake.

''Mchezo umekuwa mzuri na sasa nafuta lile neno (Tanzania ni kichwa cha Mwendawazimu anayejifunza kunyoa atunyoe sisi) lakini sasa sisi ndio vinyozi'', alisema.

Katika mchezo wa jana Simba SC iliibuka na ushindi wa mabao 4-0 hivyo kujiweka vizuri kwenye mchezo wake wa marudiano huko Djibouti. Yanga pia ilishinda dhidi ya St. Louis ya Shelisheli.

Yanga inayocheza klabu bingwa Africa itasafiri kwenda Shelisheli kwaajili ya mchezo wake wa marudiano Februari 20 huku Simba inayoshiriki Kombe la Shirikisho nayo itasafiri kuelekea Djibouti kwaajili ya mchezo wa Februari 20 au 21.

Chanzo: EATV
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…