Chakaza
JF-Expert Member
- Mar 10, 2007
- 40,455
- 73,145
Nimesikitishwa sana na kauli iliyotolewa na Tume ya Haki za Binadamu iliyo chini ya Jaji anayeheshimika kuhusu hukumu ya RC wa Arusha na kwamba mpaka dakika hii hujachukua hatua yeyote.
Huku ni kuonyesha dharau kwa mamlaka hiyo ambayo ipo kikatiba na chombo kikubwa cha msaada kwako katika utendaji wa kazi zako za kuhakikisha haki zinatendeka nchini.
Huyu Makonda mna nini naye? Au ana siri gani kiasi hata atuhumiweje kwenye mambo yasiyo faa awamu hii ya Tano (maana kwa uhalisia sio ya sita bali ya tano tuliyoichagua)bado itamlinda? Matumizi mabaya ya madaraka kwa viongozi wengine wameshapelekwa jela, lakini huyu "mtoto wako kipenzi" kama alivyojiita hadharani tena mbele yako haguswi, kunani?
Tunataka mama Samia ukistaafu 2025 au 2030 upumzike na wajukuu bila kuacha makando kando yatakayo kunyima raha màana wakati huo huna mamlaka ya kumzuia kukusema.
Huku ni kuonyesha dharau kwa mamlaka hiyo ambayo ipo kikatiba na chombo kikubwa cha msaada kwako katika utendaji wa kazi zako za kuhakikisha haki zinatendeka nchini.
Huyu Makonda mna nini naye? Au ana siri gani kiasi hata atuhumiweje kwenye mambo yasiyo faa awamu hii ya Tano (maana kwa uhalisia sio ya sita bali ya tano tuliyoichagua)bado itamlinda? Matumizi mabaya ya madaraka kwa viongozi wengine wameshapelekwa jela, lakini huyu "mtoto wako kipenzi" kama alivyojiita hadharani tena mbele yako haguswi, kunani?
Tunataka mama Samia ukistaafu 2025 au 2030 upumzike na wajukuu bila kuacha makando kando yatakayo kunyima raha màana wakati huo huna mamlaka ya kumzuia kukusema.