Rais Putin na mwenzake wa Ukrain Zelensky kukutana huko Ufaransa

Rais Putin na mwenzake wa Ukrain Zelensky kukutana huko Ufaransa

Nyendo

JF-Expert Member
Joined
Jun 4, 2017
Posts
1,336
Reaction score
4,731
Kwa mara ya kwanza leo katika kipindi cha miaka mitatu kutafanyika tena kile kinachoitwa Mkutano wa Kilele wa Normandy kuhusu mzozo wa mashariki mwa Ukraine.

Mkutano huo ulioandaliwa na Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron na Kansela wa Ujerumani Angela Merkel utawaleta pamoja Rais wa Urusi Vladimir Putin na mwenzake wa Ukraine Volodymyr Zelensky.

Hii ndiyo itakayokuwa mara ya kwanza kabisa kwa Putin kukutana na Zelensky ana kwa ana. Hatua kupigwa katika mkutano huo wa kilele itategemea pakubwa kuhusiana na iwapo Urusi na Ukraine watakubaliana kuhusiana na maandilizi ya uchaguzi katika maeneo yanayozozaniwa ya wale wanaotaka kujitenga.
 
Huwa najiuliza Putin akizeeka au akifariki, Russia itampata kiongozi mjanja na mwerevu kama yeye? Je kiongozi atakayekuja hatowafarakanisha warusi?
Hata Mimi Niliwahi Jiuliza Mkuu Ila Nikakumbuka Kuna Huyu Mwamba Wakuitwa MEDVEDEV Nikafikia Huu Mwafaka yakwamba RUSSIA Itatoka Katika Mikono Salama Naitaenda Kwemye Mikono Misalama Zaidi
 
Hata Mimi Niliwahi Jiuliza Mkuu Ila Nikakumbuka Kuna Huyu Mwamba Wakuitwa MEDVEDEV Nikafikia Huu Mwafaka yakwamba RUSSIA Itatoka Katika Mikono Salama Naitaenda Kwemye Mikono Misalama Zaidi
Ngoja tuone ila nawasiwasi kama USA atakuja kuingilia tena siasa za Russia
 
Ngoja tuone ila nawasiwasi kama USA atakuja kuingilia tena siasa za Russia
Sidhani kama serikali ya Urusi na vyombo vyake vya usalama hawajalitazamia hili! Pengine anaweza akatokea aliyemzuri zaidi ya Putin ambaye Dunia haikuwahi kumuona na kumtarajia au haikuwahi kumtarajia.

Dmitry Peskov naye anaonekana yupo vizuri ila umri wake naona kama umekwenda.
 
Wanachokifanya ni kipi? Wakati hao EU ndiyo wachawi wenyewe? Wamemtumia msaliti Zelensky kwa mwamvuli wao wa NATO na kuleta mgogoro Ukraine.
 
Back
Top Bottom