Rais Samia aambiwe ukweli, wanaotugawa kwa siasa hapa nchini ni CCM wenyewe, kusema tusiwakubali wanaotugawa ni kukiri CCM hawafai tena!

Rais Samia aambiwe ukweli, wanaotugawa kwa siasa hapa nchini ni CCM wenyewe, kusema tusiwakubali wanaotugawa ni kukiri CCM hawafai tena!

Synthesizer

Platinum Member
Joined
Feb 15, 2010
Posts
12,699
Reaction score
22,598
Sijua kama Raisi Samia alitafakari kina cha maneno aliyotamka akiwa huko Songea, pale aliposema Watanzania twapaswa kuwakataa wale wanaotaka kutugawa kwa sababu za kisiasa au tofauti za kiitikadi.

Mtu yeyote mwenye kutafakari sana ataona kama kuna wanasiasa ambao wamefanikiwa sana kutugawa Watanzania, basi ni CCM ndio waliofanya hivyo, na wanazidi kufanya hivyo. Huko nyuma, katika tawala za Mwinyi, Mkapa na hata Kikwete kwa kiasi fulani, kuwa mwanachama wa CCM au chama cha upinzani haikuwa tatizo, lakini mambo yalibadilika sana kuanzia utawala wa Magufuli na Samia, na Samia amekuwa akiendeleza ubaguzi huu wa kisiasa baada ya kuonekana kama anaanza vizuri mwanzoni.

Kila mtu anajua, wakati wa Raisi Magufuli, na Samia akiwa makamu wake, wanachama wa vyama vya upinzani walionekana kama maadui. Hata katika matukio ya kijamii, uongozi wa CCM haukutaka kabisa kuwapa ushirikiano na lilikuwa kosa kwa kiongozi wa CCM kumtembelea mgonjwa wa chama cha upinzani, au kiongozi yeyote wa CCM kutoa ushirikiano kwa viongozi wa upinzani. Na sasa hatimaye Raisi Samia anaonekana ameshawishiwa na viongozi wake wa CCM kufuata nyayo za Magufuli ikiwa anataka CCM waendelee kubaki madarakani, na sasa amebadilika na kusababisha mgawanyiko na chuki ambayo haishii kwenye mgawanyiko wa kisiasa tu bali kwenye Uzanzibar na Utanganyika.

Pia soma: Rais Samia: Tusikubali kugawanywa kwa sababu za kisiasa

Katika maeneo yenye wabunge wa upinzani, CCM wameonyesha wazi kwamba uongozi wao hautayapa kipaombele katika kuwapa huduma na fedha za maendeleo. Mkoa wa Mbeya ukiwa chini ya mbunge Sugu ulitengwa na serikali waziwazi, na umeanza kupewa mafungu ya miradi baada ya Tulia kumuondoa Sugu kwenye kiti cha Ubunge.

Mara nyingi viongozi wa CCM bila aibu wamesema ukitaka mambo yako yafanikiwe lazima uwe upande wa CCM. Hata mawaziri, wakuu wa Polisi, nk, wametoa matamko kuonyesha CCM inavyohujumu vyama vya upinzani. Na hata mifumo ya Mahakama na Polisi nchini, CCM wamehakikisha inatoa upendeleo kwa wale walio upande wa CCM zaidi ya wale walio upande wa vyama vya upinzani. Viongozi wa vyama vya upinzani wanapohamia CCM wanapewa majukwaa wawatukane na kuwakebehi viongozi wa upinzani na vyama vyao, na hata kuambiwa maneno ya kusema katika majukwaa ya CCM.

Kuhusu vyombo vya dola, CCM wamevifanya kuwa watumishi wao binafisi au watumishi wa CCM na sio serikali, iwe Polisi, Usalama wa Taifa na hata wanajaribu kuwarubuni Jeshi la Wananchi (JW), kuwafanya wawaone watu wa vyama vya upinzani ni maadui ndani ya nchi wao wenyewe Tanzania! Wamekuwa wakivijanza propaganda vyombo hivi kiasi kwamba sasa imefikia vinapotumwa kwenda kufanya kazi dhidi ya watu wa upinzani, ni kama wanapelekwa kupambana na maadui toka nje ya Tanzania!

Huko Bungeni ndio kubaya hata zaidi. Spika Tulia ameufanya Uspika kama nafasi ya kazi ndani ya CCM chini ya Mwenyekiti wa CCM Raisi Samia, na wajibu wake ni kwa wabunge wa CCM na sio wabunge wote. Amefanya kila jitihada kuwabeza na kuwakandamiza wabunge wachache wa upinzani walio Bungeni.

Sasa Raisi Samia, acha tukuambie ukweli. Wewe na kundi lako la CCM ndio mnaotugawa sana Watanzania kwa sababu za kisiasa na tofauti za kidini. Na mbaya zaidi, mnasababisha mgawanyiko huu uende hadi kwenye Uzanzibarri na Utanganyika na kuukuza siku hadi siku. Kama kuna watu wa kutowakubali hapa nchini, basi ni nyie watu wa CCM. Mnaipeleka nchi hii sehemu mbaya sana huku mkijidanganya na nyimbo za Tanzania ni nchi ya amani! Shame on all of you!!!
 
CCM wanachokijua wao ni taifa lote rika zote na jinsia zote ni wanachama wake,wanadhani wanaojiita wapinzani hawafiki hata 1mill ndiyo maana utakuta wanatoa nasaha kama hizo.
 
CCM wanachokijua wao ni taifa lote rika zote na jinsia zote ni wanachama wake,wanadhani wanaojiita wapinzani hawafiki hata 1mill ndiyo maana utakuta wanatoa nasaha kama hizo.
Kuna siku watakuja kuwa history tu, walikuwepo KANU Kenya, walikuwapo UNIP Zambia; wako wapi?
 
Kuna siku watakuja kuwa history tu, walikuwepo KANU Kenya, walikuwapo UNIP Zambia; wako

Kuna siku watakuja kuwa history tu, walikuwepo KANU Kenya, walikuwapo UNIP Zambia; wako wapi?
Ngoja ni komenti hapa maana uzi wanafuta!
Iko hivi, wala msiumize vichwa. 2025 atashinda/watashinda, lakini 2027 Mungu atatoa nafasi nyingine tena kama ya 2021. Makamu hatokubalika na wajeda maana wataona ni pandikizi toka nchi jirani (na walishaonya), vice atashupaza shingo halafu jamaa watapita nae bila kificho. Utafuata utawala wa mpito kisha uchaguzi wa kidemokrasia. Yule waliyemuumiza sana awamu ile atakamata nchi akitokea upande wa pili wa timu hasimu.
Inatosha kwa leo.
 
Ngoja ni komenti hapa maana uzi wanafuta!
Iko hivi, wala msiumize vichwa. 2025 atashinda/watashinda, lakini 2027 Mungu atatoa nafasi nyingine tena kama ya 2021. Makamu hatokubalika na wajeda maana wataona ni pandikizi toka nchi jirani (na walishaonya), vice atashupaza shingo halafu jamaa watapita nae bila kificho. Utafuata utawala wa mpito kisha uchaguzi wa kidemokrasia. Yule waliyemuumiza sana awamu ile atakamata nchi akitokea upande wa pili wa timu hasimu.
Inatosha kwa leo.
Aaah, Mkuu, yana ukweli haya? Ni katiba ipi itatumiwa 2027 kwamba wajeda wasimkubali makamu, kama kweli hilo litatokea?
 
Spoke uvumilivu na ukimya wetu ndio vinavyofanya ccm iendelee kuwa hai
 
Spoke uvumilivu na ukimya wetu ndio vinavyofanya ccm iendelee kuwa hai
 
Aaah, Mkuu, yana ukweli haya? Ni katiba ipi itatumiwa 2027 kwamba wajeda wasimkubali makamu, kama kweli hilo litatokea?
Mkuu, Mabeyo alifuata katiba ile 2021 lakini matokea yake leo hata yeye mwenyewe anajutia uamuzi ule. Ni kama Jiwe ambavyo hakufuata katiba katika utawala wake, leo hii mfuasi wake nayeye anasigina katiba mchana kweupe kwa kumcopy mtangulizi wake.

Ndivyo itavyokuwa 2027, hakuna katiba itakayofutwa baada ya hayo niliyosema kutokea, maana mwenyewe ashawaambia ni kakijitabu tu!

Niliandika kuhusu kitakachotokea kwa Jiwe 2021 kwa id nyingine wakafuta, lakini yalitimia. Tunza comment yangu mkuu.
 
Mkuu, Mabeyo alifuata katiba ile 2021 lakini matokea yake leo hata yeye mwenyewe anajutia uamuzi ule. Ni kama Jiwe ambavyo hakufuata katiba katika utawala wake, leo hii mfuasi wake nayeye anasigina katiba mchana kweupe kwa kumcopy mtangulizi wake.

Ndivyo itavyokuwa 2027, hakuna katiba itakayofutwa baada ya hayo niliyosema kutokea, maana mwenyewe ashawaambia ni kakijitabu tu!

Niliandika kuhusu kitakachotokea kwa Jiwe 2021 kwa id nyingine wakafuta, lakini yalitimia. Tunza comment yangu mkuu.
Yajayo yanafuvutia, na yanaweza kuja kuwa ya kuishangaza dunia! Na kama nilivyosema, Mabeyo anatudanganya alifanya vile kulinda Katiba, sasa swali ni kwamba, kwa nini anachagua vipengele vya Katiba atakavyolinda? Vipengele vingine vya Katiba vinapokiukwa kwa makusudi, mbona humwoni kusimama na kuvitetea?
 
Yajayo yanafuvutia, na yanaweza kuja kuwa ya kuishangaza dunia! Na kama nilivyosema, Mabeyo anatudanganya alifanya vile kulinda Katiba, sasa swali ni kwamba, kwa nini anachagua vipengele vya Katiba atakavyolinda? Vipengele vingine vya Katiba vinapokiukwa kwa makusudi, mbona humwoni kusimama na kuvitetea?
Zetu dua mkuu, tulipata uhuru wa "bendera" bila kumwaga damu, ndivyo tutakavyopata uhuru wa kweli bila kumwaga damu za wengi ingawa damu za wapinzani wa serikali hii dhalimu, zinalipia uhuru huo.
 
Back
Top Bottom