Rais Samia aanza kurekodi kipindi maarufu cha ‘Royal Tour’ kuitangaza Tanzania kimataifa kupitia vivutio ya utalii

Huko kwenu ubao unasoma ngapi ?
 
Safi sana, ni kitu kipya chenye mvuto wa kipekee kwa Rais kutangaza.
Hakika Rais ameamua kuingia field.
Mawaziri, Manaibu na watendaji wengine wa taasisi za Serikali acheni kujifungia maofisini, tokeni, kuweni wabunifu ktk kutatua changamoto mbalimbali.
 
Watanzania hawana shukrani wanasema Huyu mama hajafanya kitu chochote cha maana tangu aingie ikulu. Hili analolifanya kwao si lolote si chochote!!. Aliyeturoga japo tuonyeshwe kaburi lake tuweze kuomba kwa nguvu zetu zote.
 
Useme wewe! Maana wewe ndo umesema democrasia ndo inayoitangaza nchi!
Sera ya Rwanda ya mambo ya nje ni tofauti kabisa na Sera ya Tanzania ya mambo ya nje.Tanzania huwa inachukulia wazungu kama threats(mabeberu) wakati Rwanda huwa inachukulia wazungu kama fursa.

Hivi ni vitu viwili tofauti.Huwezi kulinganisha vitu viwili tofauti.Kwa hili huwezi kuilinganisha Tanzania na Rwanda.Jifunze kulinganisha vitu.
 
Watanzania hawana shukrani wanasema Huyu mama hajafanya kitu chochote cha maana tangu aingie ikulu. Hili analolifanya kwao si lolote si chochote!!. Aliyeturoga japo tuonyeshwe kaburi lake tuweze kuomba kwa nguvu zetu zote.
Aliyewaroga atafutwe Kweli!

kila siku wanamsifia Kagame hapa kuwa anaibrand nchi yake vizuri na sasa inakamata Africa kiuchumi. Akifanya Samia ni malalalmiko tu na kulaumu. Hawa watu aliyewaroga atafutwe kwa Kweli.
 
Wapi tumesema Sera yetu ya mambo ya nje inawachukulia wazungu kama mabeberu/ threat??

Umeishia darasa la ngapi we mtu?
 
Wapi tumesema Sera yetu ya mambo ya nje inawachukulia wazungu kama mabeberu/ threat??

Umeishia darasa la ngapi we mtu?
Useme wewe kama nani?Wewe ndiye Serikali ya CCM?Wapi nimesema kuwa wewe au mimi tumesema kuwa tunachukulia wazungu kama threats?Unajua kusoma?

Nilichosema hapo juu ni kwamba serikali ya Tanzania huwa inachukulia wazungu kama threats(mabeberu).
Sijasema kuwa wewe au mimi huwa tunachukulia wazungu kama threats.
 
Nimeshangaa kuona nchi kama Mozambique inatembelewa na watalii wengi kuliko Tzn na iko top 5 ya Afrika.

Sijawahi ona kivutio chochote kutoka hiyo nchi kimeongoza duniani,Tzn hapa tuna mbuga na milima na beach za Zanzibar na top hotel vina feature kwenye List ya Dunia lakini tunachoambulia ni matusi.Mozambique kabla ya Covid 2018 ilipokea wageni 2.7 Mil.Tzn tunakwama wapi?
 
Haya ni maajabu ya DUNIA yanayotokea Tanzania

Watu wa zamani hawakufanya mamosa kusema

"Chema kinajiuza, na kibaya kinajitangaza.."

Waziri wa maliasili, waziri wa mabo ya nje na bodi ya utalii Tanzania wako wapi hadi Raisi mwenyewe anajichukulia wajibu wa kuitangaza wakati wapo wanaolipwa kwa kazi hiyo?

Mh Rais anashauriwa aachane na hatua hiyo maana baadhi hawatahangaika kutazama makala hizo, anatakiwa kuwawajibisha watendaji kama anadhani kuna pahala wamesinzia au kubweteka.

Utalii utaendela kuporomoka kwa kasi sana wakati walitakiwa wahamasishe watanzania wa kawaida kutembelea sehemu za vivutio kwa gharama nafuu na taratibu zilizoboreshwa mahali husika badala ya kuweka sharti kwamba ni lazima mteja awe amelipia kwenye ofisi mkoani na kupewa 'control number' ya malipo hayo kitu ambacho ni usumbufu usio wa lazima.

Malipo yafanyike sehemu husika mtu anapotembelea sio kumwingizia gharama za kukatisha tamaa.
 
HILI NALO NI TATIZO
AU NDO KASHAJIPA UWAZIRI WA UTALII NA MALIASILI...
ataingizwa kwenye orodha ya maraisi vituko waliowahi kutokea ulimwenguni.
 
Mlitaka afanyaje kwa mfano??!!
Aliyewaroga atafutwe Kweli!

kila siku wanamsifia Kagame hapa kuwa anaibrand nchi yake vizuri na sasa inakamata Africa kiuchumi. Akifanya Samia ni malalalmiko tu na kulaumu. Hawa watu aliyewaroga atafutwe kwa Kweli.
tena mr slim mabeberu wakienda nchini anawaendesha mwenyewe kwenye gari yake na kuwatembeza kwenye vivutio...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…