Rais Samia achangia shilingi milioni kumi mfuko wa yatima na wajane mkoa wa Dodoma

Rais Samia achangia shilingi milioni kumi mfuko wa yatima na wajane mkoa wa Dodoma

BWANKU M BWANKU

JF-Expert Member
Joined
Jan 12, 2019
Posts
377
Reaction score
435
RAIS SAMIA SULUHU HASSAN ACHANGIA SHILINGI MILIONI KUMI MFUKO WA YATIMA NA WAJANE MKOA WA DODOMA.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan amechangia shilingi milioni kumi katika mfuko wa kuwahudumia mayatima na wajane mkoa wa Dodoma.

Mchango wake huo umewasilishwa kwa niaba yake na Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Itikadi na Uenezi Ndugu Shaka Hamdu Shaka katika dua maalum, mashindsno ya Qur'an na iftari iliyoandaliwa Jumapili 03 April 2022 katika ukumbi wa PSSSF Jijini Dodoma.

Ikiwa ni kuadhimisha mwaka mmoja wa uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan tokea kuweko madarakani.

Pamoja na mchango huo amekabidhi chakula na mahitaji vituo vya watoto yatima na wajane katika wilaya za mkoa wa Dodoma.

#RamadhanMubarak
#KaziIendelee

FB_IMG_1649021551706.jpg

FB_IMG_1649021547926.jpg

FB_IMG_1649021538886.jpg

FB_IMG_1649021544330.jpg

FB_IMG_1649021534905.jpg


FB_IMG_1649021529932.jpg
 
Back
Top Bottom