Rais Samia aendelee Kuonyesha Umahiri Wake Kiuongozi. Tanzania ina Mfumuko Mdogo Wa Bei kwa Nchi Zote Afrika Mashariki

Rais Samia aendelee Kuonyesha Umahiri Wake Kiuongozi. Tanzania ina Mfumuko Mdogo Wa Bei kwa Nchi Zote Afrika Mashariki

Lucas Mwashambwa

JF-Expert Member
Joined
Jul 28, 2022
Posts
28,722
Reaction score
20,610
Ndugu zangu Watanzania,

Rais wetu Mpendwa na Jemedari wetu kipenzi cha watanzania Mheshimiwa Daktari Mama Samia Suluhu Hasssan Mama wa shoka, chuma cha Reli, shujaa wa Afrika, jasiri muongoza njia, simba wa nyika, komandoo wa vita, nyota ya matumaini na nuru ya wanyonge.

Anaendelea kuonyesha Umahiri Wake Kiuongozi katika jumuiya ya Afika mashariki na Bara zima kwa ujumla wake. Sera zake kiuchumi na mipango yake ya uchumi imeendelea kuimarisha uchumi wetu pamoja na kudhibiti mfumuko wa Bei hapa Nchini.

Ambapo Tanzania imeonekana kitakwimu kuwa na mfumuko wa chini sana wa Bei ukilinganisha na Nchi zote za ukanda huu wa Afrika mashariki. Hii maana yake inaleta unafuu na ahueni ya kimaisha kwa watanzania. Ikumbukwe ni wakati huu wa Rais Takwimu zimeonyesha Tanzania ikipanda nakufanya vizuri kabisa katika Nchi zilizotembelewa na wageni yaani watalii .ambapo sasa idadi imepanda kutoka millioni 1.8 mpaka Millioni 5 na Pointi.

Hii ikiwa ni matunda ya Royal Tour ambayo ilifanywa na kuongozwa na Rais wetu Mpendwa katika kuvitangaza vivutio mbalimbali vya utalii vilivyopo hapa Nchini. Jambo ambalo limeendelea kuwavutia watu mbalimbali kutoka kila kona ya Dunia kuja na kuitembelea Nchi yetu.
Screenshot_20250302-192521_1.jpg


Kazi iendelee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa Maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa, Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
 
Hii taarifa yako ni nzuri sana,tunaomba utupatie na jarida la kimataifa lililoandika kuhusu mfumko mdogo wa bei kwa Tanzania.
Kwa hiyo wewe unasubiri jarida la kimataifa likuandikie Mambo yako Mwenyewe? Kwamba sisi hatuna akili ya kuandika na jarida la kimataifa likachukua kutoka kwetu? Kwanini watanzania mnajidharau kiasi hicho? Kwanini mnajidunisha kama watumwa ? Kwanini mnakuwa watumwa wa akili kiasi hicho?
 
Kwa hiyo wewe unasubiri jarida la kimataifa likuandikie Mambo yako Mwenyewe? Kwamba sisi hatuna akili ya kuandika na jarida la kimataifa likachukua kutoka kwetu? Kwanini watanzania mnajidharau kiasi hicho? Kwanini mnajidunisha kama watumwa ? Kwanini mnakuwa watumwa wa akili kiasi hicho?
Sawa. Wewe genius tupatie data ulizopika hapa.
 
"Hakuna umadikini mbaya kama umadikimi wa Fikra"

Jk Nyerere.
 
Huyo bibi mwenyew hata haelewi kitu kuhusu uchumi ni mambo yanajiendea tu ilimradi!
 
Back
Top Bottom