Rais Samia akutana na Rais wa China, Xi Jinping na ujumbe wake

Rais Samia akutana na Rais wa China, Xi Jinping na ujumbe wake

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
GWnD2AKWIAAOWDZ.jpg
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan amefanya mkutano na Rais wa China, Xi Jinping pamoja na ujumbe wake mapema leo, Septemba 4, 2024 katika ukumbi wa The Great Hall of the People jijini Beijing.

Rais Samia amefanikiwa kuimarisha mahusiano ya kidiplomasia ya Tanzania na nchi muhimu duniani ikiwepo China tangu alipoingia madarakani Mwaka 2021.
GWnD18eaoAAuMGu.jpg

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Rais Jamhuri ya Watu wa China, Xi Jinping katika Ukumbi wa The Great Hall of the People kabla ya kuanza mazungumzo Jijini Beijing, tarehe 4 Septemba, 2024.
Kwa Mwaka huu wa 2024 Rais Samia na Xi Jinping wamejadiliana kuimarisha uhusiano wetu mzuri uliodumu zaidi ya miaka 60.

Vilevile baada ya kikao hicho Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais Jamhuri ya Watu wa China Mhe. Xi Jinping pamoja na Rais wa Zambia Mhe. Hakainde Hichilema walishuhudia uwekaji saini wa hati ya makubaliano ya kuboresha reli ya TAZARA.
GWnFKqfacAAo1Qb.jpg

GWnFKqea4AEd3HD.jpg

GWnFKqdbYAAX6VT.jpg

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan na ujumbe wake wakiwa kwenye kikao cha pamoja na Rais wa Jamhuri ya Watu wa China, Xi Jinping na ujumbe wake katika ukumbi wa The Great Hall of the People jijini Beijing, tarehe 4 Septemba, 2024.
 
"DEBT TRAP" na hizi njaa zetu tutadaiwa mpaka Maiti zutadaiwa ngoja tusikie "Kodi ya kufa" au "Ushuru wa kukata roho" nk.
Rasilimali nyingi zitaondoka TUNAINGIZWA KWENYE MITEGO YA MADENI.
 
Back
Top Bottom