Rais Samia amemteua Brigedia Jenerali Yohana Ochalla Mabongo kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Posta Tanzania (TPC)

Rais Samia amemteua Brigedia Jenerali Yohana Ochalla Mabongo kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Posta Tanzania (TPC)

sajo

JF-Expert Member
Joined
Nov 8, 2010
Posts
3,474
Reaction score
6,195
Rais Samia amemteua Brigedia Jenerali Yohana Ochalla Mabongo kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Posta Tanzania (TPC). Jenerali Mabeyo kwa sasa ana umri wa miaka 65, inawezekana ndiyo anastaafu na maandalizi ya mrithi wake yameanza.

Inasemwa kuwa mtu anayeshika nafasi ya CDF ni mwenye cheo cha Brigedia Jenerali, ambapo ikiwa Rais hawataki wenye vyeo hivyo kushika nafasi hiyo basi option aliyonayo ni kuwaondoa watu hao jeshini ili kumpa unafuu wa kuongoza jeshi mtu atayemteua kushika nafasi ya CDF. JPM baada ya kumteua Mabeyo inasemwa kuwa Mabeyo alipata upinzani kutoka kwa mabrigedia wengine na ndipo wakaondoshwa jeshini kwa kupewa teuzi sehemu mbalimbali ili Jenerali Mabeyo aongoze jeshi vyema.

Uteuzi wa Brigedia Mabongo inaweza kuwa ndio utekelezaji wa OPTION ya kuwaondoa watu hawa jeshini na pia inaweza kuwa ishara kuwa CDF mpya atapatikana karibuni. Ingawa sijui kama uteuzi wa huyu brigedia unamuondoa jeshini (kwa maana ya kuendelea na majukumu ya kila siku ya kijeshi) au la. Wenye uelewa na haya mambo tupeni ufafanuzi.

20220228_134227.jpg
 
Uenyekiti wa bodi sio ajira, kwa mwaka mnaweza kukutana mara nne. Je ndio itamfanya ashindwe kutekeleza majukumu yake ya sasa?
Ndio tueleweshane mkuu. Kwamba anaweza kushika vyote kwa mara moja?
 
Yule mwenye uthubutu wa kujenga viwanda vya barakoa, vidonge, na gloves kwa muda mfupi wa msd anafaa
Daktari wa binadamu? No way! Hao huwaga ni raia tu, degree zinawabeba. Daktari wa binadamu hawezi kuwa CDF hata iweje.
 
Kwanza si kweli kuwa mwenye sifa ya kuwa CDF ni ofisa wa cheo cha brigedia jenerali. Huyo ni one star general, ndiye the most junior katika ujenerali. CDF ni four star general, na mara nyingi hupandishwa cheo hicho akitokea cheo cha Lt Gen ambaye ni three star general.
 
Tokea Jeshi liwekewe muundo wa kuongozwa na Four stars general haijawahi kutokea CDF akapewa Brigedia jenerali yeyote yule na sidhani kama itakuja tokea

CDF wametokeaga Meja jenerali na luteni jenerali yaani hiyo kuwa Brigedia jenerali tu inamaana wewe ni mtu mgeni katika uongozi wa juu jeshini
 
Rais Samia amemteua Brigedia Jenerali Yohana Ochalla Mabongo kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Posta Tanzania (TPC). Jenerali Mabeyo kwa sasa ana umri wa miaka 65, inawezekana ndiyo anastaafu na maandalizi ya mrithi wake yameanza.

Inasemwa kuwa mtu anayeshika nafasi ya CDF ni mwenye cheo cha Brigedia Jenerali, ambapo ikiwa Rais hawataki wenye vyeo hivyo kushika nafasi hiyo basi option aliyonayo ni kuwaondoa watu hao jeshini ili kumpa unafuu wa kuongoza jeshi mtu atayemteua kushika nafasi ya CDF. JPM baada ya kumteua Mabeyo inasemwa kuwa Mabeyo alipata upinzani kutoka kwa mabrigedia wengine na ndipo wakaondoshwa jeshini kwa kupewa teuzi sehemu mbalimbali ili Jenerali Mabeyo aongoze jeshi vyema.

Uteuzi wa Brigedia Mabongo inaweza kuwa ndio utekelezaji wa OPTION ya kuwaondoa watu hawa jeshini na pia inaweza kuwa ishara kuwa CDF mpya atapatikana karibuni. Ingawa sijui kama uteuzi wa huyu brigedia unamuondoa jeshini (kwa maana ya kuendelea na majukumu ya kila siku ya kijeshi) au la. Wenye uelewa na haya mambo tupeni ufafanuzi.

View attachment 2134005
Nani amekwambia kuwa mwenyekiti wa bodi unapoteza nafasi yako nyingine?
 
Kwanza si kweli kuwa mwenye sifa ya kuwa CDF ni ofisa wa cheo cha brigedia jenerali. Huyo ni one star general, ndiye the most junior katika ujenerali. CDF ni four star general, na mara nyingi hupandishwa cheo hicho akitokea cheo cha Lt Gen ambaye ni three star general.
Mleta mada kachemka, hajui vyeo vya kijeshi.
 
Back
Top Bottom