Mkalukungone mwamba
JF-Expert Member
- Aug 29, 2022
- 862
- 1,755
Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amewaomba Wakazi wa Ukonga kumshika Mbunge wa Jimbo hilo ambaye pia ni Waziri wa Habari, Teknolojia ya Habari na Mawasiliano, Jerry Silaa kwakuwa ni Waziri anayefanya kazi vizuri.
Rais Samia amesema hayo leo August 01,2024 akiwa Pugu njiani kuelekea Dodoma kwa treni ya SGR.
“Nawashukuru Wakazi wa Ukonga mmenipa Kijana mzuri sana Jerry Silaa, nilianza nae kwenye Sekta ya ardhi, mmeona kazi kubwa aliyoifanya kwenye ardhi, kazi ya kuendesha clinic za kutosha kutatua kero za ardhi Tanzania, sasa kwa kazi kubwa aliyoifanya nimeona sasa nimkabidhi vyombo vya habari na propaganda zetu zote za Tanzania”
“Kwahiyo sasa Mbunge wenu yupo kwenye vyombo vya habari, kazi hizi ni kubwa Ndugu zangu inawezekana
Mbunge wenu anakaa wiki tatu nne hajaonekana lakini mjue yupo kazini kunisaidia kuijenga Tanzania, kwahiyo nawashukuru sana nakuombeni mshikeni mkono tuendelee na kazi ya maendeleo kwenye Jimbo”
Rais Samia amesema hayo leo August 01,2024 akiwa Pugu njiani kuelekea Dodoma kwa treni ya SGR.
“Nawashukuru Wakazi wa Ukonga mmenipa Kijana mzuri sana Jerry Silaa, nilianza nae kwenye Sekta ya ardhi, mmeona kazi kubwa aliyoifanya kwenye ardhi, kazi ya kuendesha clinic za kutosha kutatua kero za ardhi Tanzania, sasa kwa kazi kubwa aliyoifanya nimeona sasa nimkabidhi vyombo vya habari na propaganda zetu zote za Tanzania”
“Kwahiyo sasa Mbunge wenu yupo kwenye vyombo vya habari, kazi hizi ni kubwa Ndugu zangu inawezekana
Mbunge wenu anakaa wiki tatu nne hajaonekana lakini mjue yupo kazini kunisaidia kuijenga Tanzania, kwahiyo nawashukuru sana nakuombeni mshikeni mkono tuendelee na kazi ya maendeleo kwenye Jimbo”