Rais Samia anatarajiwa kufanya ziara ya siku sita mkoani Morogoro mwanzoni mwa mwezi Agosti

Rais Samia anatarajiwa kufanya ziara ya siku sita mkoani Morogoro mwanzoni mwa mwezi Agosti

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Joined
Jul 13, 2013
Posts
60,660
Reaction score
121,325
1722577933395.png

Rais Samia

Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kufanya ziara ya siku sita mkoani Morogoro mwanzoni mwa mwezi Agosti mwaka huu.

Akitoa taarifa ya ziara ya Rais Samia, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Adam Malima amesema ziara hiyo itaanza Agosti 2- 7 mwaka huu.

Kwa mujibu wa mkuu wa mkoa huyo, katika ziara hiyo, Rais Samia anatarajiwa kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo ndani ya mkoa ikiwemo ya ujenzi vituo vya afya,kilimo na viwanda.

Chanzo: azamtvtz

Haiwezekani Mkoa ambao uko Jirani na Dar es Salaam miaka nenda rudi hauna Maendeleo na uko vile vile tu. Nyumba nyingi maeneo ya Mjini bado ni za Udongo na Chakavu, Miundombinu inatia Aibu ila Kutwa tu Wakazi wa Mkoa wanapishana tu Milimani kwenda kwa Waganga Kurogana.

Nina Uchungu na huu Mkoa kwakuwa ni Mkoa ambao Ukoo wangu Mmoja umelowea hapo na Kuota Mizizi yake pia.

Cc: Mdogo wangu wa damu kabisa steveachi

PIA SOMA
- Rais Samia kufanya ziara Morogoro kuanzia Julai 7, 2021

UPDATE
- Ziara ya Rais Samia Agosti 1, 2024 yasimamisha shuguli za kiuchumi jijini Dar es Salaam
 
Bila kusahau kuwa viongozi wengi waandamizi na watarajiwa wanapata na wamepata elimu hapo kwenye vyuo vikuu Sokoine, Mu, St. Joseph na Mzumbe.

Wameishi hapo na wengine wamezalisha na kuzaa watoto hapo, wapaangalie Kwa jicho la maendeleo asee.
 
Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kufanya ziara ya siku sita mkoani Morogoro mwanzoni mwa mwezi Agosti mwaka huu.

Akitoa taarifa ya ziara ya Rais Samia, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Adam Malima amesema ziara hiyo itaanza Agosti 2- 7 mwaka huu.

Kwa mujibu wa mkuu wa mkoa huyo, katika ziara hiyo, Rais Samia anatarajiwa kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo ndani ya mkoa ikiwemo ya ujenzi vituo vya afya,kilimo na viwanda.

Chanzo: azamtvtz

Haiwezekani Mkoa ambao uko Jirani na Dar es Salaam miaka nenda rudi hauna Maendeleo na uko vile vile tu. Nyumba nyingi maeneo ya Mjini bado ni za Udongo na Chakavu, Miundombinu inatia Aibu ila Kutwa tu Wakazi wa Mkoa wanapishana tu Milimani kwenda kwa Waganga Kurogana.

Nina Uchungu na huu Mkoa kwakuwa ni Mkoa ambao Ukoo wangu Mmoja umelowea hapo na Kuota Mizizi yake pia.

Cc: Mdogo wangu wa damu kabisa steveachi
Labda Morogoro ya Mabwepande,ya sasa hv ni 💥💥 sana mkuu,tena sasa hv mji umehamia Msamvu sio kule mjini ambako mara ya mwisho ulivyokuja kumtembelea babu ukaishia Kahumba,sasa hv kuna viwanja bab kubwa.

Karibu sana Moro
 
Gharama ya kuhudumia msafara kwa wiki nzima inatosha kufanya maendeleo makubwa sana ikiwemo kuboresha miundombinu ya afya, maji, barabara na elimu. Utadhani mkoa wa Morogoro hauna kiongozi wa serikali.
 
Back
Top Bottom