Rais Samia aridhia kuuza nyumba za Magomeni Kota kwa utaratibu ya mpangaji mnunuzi, watarejesha gharama za ujenzi bila ardhi

Rais Samia aridhia kuuza nyumba za Magomeni Kota kwa utaratibu ya mpangaji mnunuzi, watarejesha gharama za ujenzi bila ardhi

Magazetini

JF-Expert Member
Joined
Aug 16, 2014
Posts
593
Reaction score
1,712
Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan ameridhia kuuziwa wananchi nyumba za Magomeni Kota kwa utaratibu wa mpangaji mnunuzi kwa kurejesha gharama za ujenzi pekee bila gharama za ardhi.

Rais Samia kasema wakitoza ardhi wahusika watashindwa kuzinunua. Pia Rais amesema wanaweza kuanza kulipa sasa polepole itakuwa vizuri ili kuwawezesha TBA kumalizia sehemu iliyobakia.

Awali waziri na msemaji wa Magomeni Kota walimkumbusha Rais Samia juu ya ahadi ya Serikali kuwa waliahidiwa kuuziwa nyumba husika kwa utaratibu wa mpangaji mnunuzi.

Mbunifu wa majengo na mtendaji mkuu TBA, Daud Kondoro amesema ujenzi ulianza Oktoba 1, 2016 kufuatia maelekezo ya Serikali yaliyotolewa Septemba ambapo iliazimia kujenga nyumba kwa wakazi 644 waliokuwa wakiishi katika nyumba za awali. Zimetumika jumla ya bilioni 52.19 kama gharama za ujenzi.

Eneo la Magomeni Kota lina viwanja vitatu vyenye jumla ya hekta 12.9 sawa na ekari 32 ambapo TBA pia imetumia vyanzo vyake vya mapato kujenga soko kwa wakazi wa eneo hilo ambapo imejenga Magomeni Kota Machinga centre kwa ajili ya wafanyabiashara ndogo ndogo pia inaendelea kujenga Magomeni Kota shopping centre.

Mwaka 2016 Rais Magufuli alifuta hati za Magomeni kota na kuhitimisha ugomvi wa miaka mingi suluhusho likiwa wakazi kuzinunua kwa bei nafuu ya jengo baada ya Serikali kumaliza ujenzi, pia kutolipa kodi miaka mitano wakati wakilipa deni.

Pia, Soma=> DAR: Rais Magufuli afuta hati na mikataba yote ya ardhi ya Magomeni Kota
 
Ndio nyumba za serikali kama zile za Magufuli?
 
Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan ameridhia kuuziwa wananchi nyumba za Magomeni Kota kwa utaratibu wa mpangaji mnunuzi kwa kurejesha gharama za ujenzi pekee bila gharama za ardhi.

Rais Samia kasema wakitoza ardhi watashindwa kuzinunua. Pia Rais amesema wanaweza kuanza kulipa sasa polepole na wakianza sasa itakuwa vizuri ili kuwawezesha TBA kumalizia sehemu iliyobakia.

Awali waziri na msemaji wa Magomeni Kota walimkumbusha Rais Samia juu ya ahadi ya Serikali kuwa waliahidiwa kuuziwa nyumba husika kwa utaratibu wa mpangaji mnunuzi
Hapo majina yataingia yale yale ya akina Kikwete na wengine hao watabaki kuwa wapangaji tu
 
Ndio nyumba za serikali kama zile za Magufuli?

Hizi za wanyonge wanauziwa uhalali wa nyumba wakati zile nyumba za serikali za Osterbay , Masaki, Ocean road etc wao waliuziwa mazimaa Ardhi na Nyumba kwa bei siri na hati wakatengenezewa
 
Hizi za wanyonge wanauziwa uhalali wa nyumba wakati zile nyumba za serikali za Osterbay , Masaki, Ocean road etc wao waliuziwa mazimaa Ardhi na Nyumba kwa bei siri na hati wakatengenezewa
Ule ulikuwa ni uzembe ambao HAUTAJIREJEA, wamejifunza!
 
Wapatieni pia Watumishi wa Serikali nao wafaidi kama wale wa enzi ya Mkapa na Magufuli wa Ujenzi (watawashukuru wanapoendelea kutumika)
 
Ina maana ni lease holder bado ni serikali, mnunuzi hana uhuru wa kufanya mageuzi ya matumizi ya jengo mpaka apate kubali kutoka kwa lease holder.
 
Magufuli kajenga kwa hela yake? Acha uzwazwa
Acha uzwazwa basi, huwa mnasema mama katoa, kwani hizo pesa zipo mfukoni mwake?

Waziri wa fedha na makatibu wakuu wote mnawafanya wafagizi!
 
Kwanini pesa zetu zinaenda kujenga maghorofa Zanzibar na wanapewa bure sisi huku tunauziwa?
 
Inamaana ni lease holder bado ni serikali, mnunuzi hana uhuru wa kufanya mageuzi ya matumizi ya jengo mpaka apate kubali kutoka kwa lease holder.
Kinachonimaliza nguvu Tanzania ni ile Rais anapojigeuza kama computer ya kupanga na kufanya kila kitu. Mpaka amri ya nyumba zitumike na ziuzwe namna gani Rais anaingilia.
 
Back
Top Bottom