Rais Samia ateua Wenyeviti na Makamu Wenyeviti wa Bodi za TMA, Mkonge na Tume ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi

Rais Samia ateua Wenyeviti na Makamu Wenyeviti wa Bodi za TMA, Mkonge na Tume ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan amefanya uteuzi wa Wenyeviti na Makamu Wenyeviti wa Bodi kama ifuatavyo:

i) Amemteua Jaji Mshibe Ali Bakari kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (Tanzania Meteorological Authority - TMA) na amemteua Dkt. Emmanuel Jonathan Mpeta kuwa Makamu Mwenyekiti wa Bodi hiyo.

ії) Amemteua Balozi Adadi Mohamed Rajab kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Tume ya Ulinzi wa Taarifa binafsi na amemteua Bi. Fatma Mohamed Ali kuwa Makamu Mwenyekiti wa Bodi hiyo.

iii) Amemteua Bw. Theobald Maingu Sabi kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Bodi ya Mkonge, Tanzania.

Uteuzi huu umeanza tarehe 10 Desemba, 2023.
IMG_9329.jpeg
 
Huyu mama kutoka Zenjibia na utawala wake ni mwendo wa teuzi tu.Hakika taifa hili halina viongozi.
 
Back
Top Bottom